Skip to main content

Posts

Showing posts from April 26, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Miaka minne ya Rais Samia Arumeru yapokea shilingi Bilioni 100.6 za maendeleo

   📌 Dkt. Biteko asisitiza Watanzania wasijaribu kuchezea amani 📌 Dkt. Biteko awataka Watanzania kuenzi, kudumisha Muungano  Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema wananchi wa wilayani Arumeru, mkoani Arusha na Watanzania kwa ujumla wana kila sababu ya kumshukuru na kumuombea Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini. Dkt. Biteko amesema hayo leo Aprili 25, 2025 katika mkutano wa hadhara uliofanyika Tengeru Wilaya ya Arumeru, Mkoa wa Arusha ambapo amesema katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Dkt. Samia wilaya ya Arumeru imepokea zaidi ya shilingi bilioni 100 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. “Arusha DC imepata fedha kiasi cha shilingi bilioni 49.6 na Wilaya ya Arumeru imepokea zaidi ya shilingi bilioni 51 kwa ajili ya shughuli na miradi mbalimbali ya maendeleo,” amesema Dkt. Bitek...

Wabunge Tanga watuma salamu kwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan*

  📍 Wazipitisha kwa Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar  📍 Wasema Tanga ipo salama, wasubiri uchaguzi ufike wampe kura za mafuriko Na wandishi Wetu, Tanga  WABUNGE wa mkoa wa Tanga, wamempa salamu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Zubeir Ali Maulid afikishe salamu kwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwamba majimbo yote 15 ya mkoa huo yatakuwa na wabunge wa CCM. Aidha, wabunge hao pia wamesema wanasubiri uchaguzi ufike mwezi Oktoba mwaka huu ili wananchi wa Tanga waongoze kwa kumpa kura nyingi Rais Dkt Samia. Akizungumza kwa niaba ya wabunge hao kwenye uwekaji jiwe la msingi jengo la soko la Machinga Jijini Tanga, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii na mbunge wa Mkinga, Dastan Kitandula alimuomba spika huyo apeleke salamu kwa Rais kwamba mkoa huo kupitia wabunge hao umejipanga kuendelea kuifanya Tanga kuwa ya kijani. Alisema wanamshukuru Rais kwa kazi kubwa aliyoifanya katika mkoa huo kwa kuipatia miradi ya maendeleo karibu kila kijiji hatua ambayo imeleta tija kw...

Mchengerwa: Tuulinde Muungano kwa vizazi vyetu

  OR-TAMISEMI Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa wito kwa Watanzania kuuenzi Muungano kwa ajili ya kudumisha amani, umoja na udugu huku akipendekeza kuanzishwa kwa wiki maalum ya Muungano kwa shule zote nchini ili kukuza uelewa wa wanafunzi kuhusu historia ya Muungano. Mhe.Mchengerwa ameyasema hayo katika kijiji cha Sangambi mkoani Mbeya baada ya kukagua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi ya maendeleo yenye thamani ya Sh.bilioni 40 huku wananchi wakimpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa. Amehamasisha wasanii na waandishi kuendeleza simulizi za mshikamano wa kitaifa ili kudumisha Muungano huku akiwaasa wazazi kuwaelimisha vijana juu ya thamani ya Muungano. Amesisitiza kuwa Tanzania ni mfano wa amani barani Afrika, tofauti na mataifa mengine yaliyogubikwa na migogoro na kwamba Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikuwa wa kweli, wa kiitikadi na kimaadili, na umeleta mafanikio makubwa kwa taifa. Waziri Mchengerwa ampongeza...

Majaliwa mgeni rasmi katika mdahalo wa fursa za maendeleo ya ushirika

  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Aprili 27, 2025 ni mgeni rasmi katika Mdahalo wa upatikanaji Mitaji ya Fedha na Fursa za Maendeleo ya Ushirika, mdahalo huo unafanyika katika ukumbi wa mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma. Awali wakati akitembelea mabanda ya maonesho, Mheshimiwa Majaliwa alizindua mradi wa kwanza wa utekelezaji wa Programu ya BBT(BBT PROJECT 1) . Pia alizindua ramani ya Shoroba za Kilimo nchini.