Skip to main content

Posts

Showing posts from June 11, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mavunde azindua SACCOS ya waendesha Pikipiki na Bajaji Dodoma

  Dodoma Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh. Anthony Mavunde amezindua Ushirika wa waendesha Pikipiki na Bajaj Dodoma na kuwataka wasafirishaji hao kutumia fursa hiyo kujiimarisha kiuchumi kupitia mikopo mbalimbali. “Ninawapongeza kwa uamuzi huu wa kuanzisha SACCOS yenu,ni wakati muafaka sasa kuwaona vijana mkimiliki vyombo vya usafiri vya kwenu wenyewe. Kupitia SACCOS hii vijana wengi watabadilisha maisha yao na kujijenga kiuchumi. Nitoe rai kwa viongozi wa SACCOS kuhakikisha mnatumia vizuri mkopo wa asilimia 10 wa mapato ya ndani ya Jiji la Dodoma ambapo mpaka sasa zimetengwa shilioni Bilioni 7 kwa ajili ya kukopesha vikundi vya wakina mama,vijana na watu wenye ulemavu”Alisema Mavunde Naye Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Alhaj Jabir Shekimweri anewataka maafisa wasafirishaji hao kutumia SACCOS kutatua changamoto za msingi za kiuchumi za vijana wengi na kuahidi kwamba serikali itakuwa nao bega kwa bega kuhakikisha inaweka mazingira rafiki ya ufanyaji wa shughuli zao. Kamanda wa Polisi wa...

Mavunde Azindua Saccos ya Waendesha Pikipiki na Bajaj Dodoma

  ▪️Atoa rai SACCOS kuwainua Vijana kupitia mkopo wa Asilimia 10 ▪️Ataka Vijana wamiliki vyombo vyao vya usafiri ▪️Wampongeza Rais Samia kwa ujenzi wa ofisi ya Waendesha Pikipiki na Bajaj Dodoma(UMAPIDO) Dodoma Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh. Anthony Mavunde amezindua Ushirika wa waendesha Pikipiki na Bajaj Dodoma na kuwataka wasafirishaji hao kutumia fursa hiyo kujiimarisha kiuchumi kupitia mikopo mbalimbali. “Ninawapongeza kwa uamuzi huu wa kuanzisha SACCOS yenu,ni wakati muafaka sasa kuwaona vijana mkimiliki vyombo vya usafiri vya kwenu wenyewe. Kupitia SACCOS hii vijana wengi watabadilisha maisha yao na kujijenga kiuchumi. Nitoe rai kwa viongozi wa SACCOS kuhakikisha mnatumia vizuri mkopo wa asilimia 10 wa mapato ya ndani ya Jiji la Dodoma ambapo mpaka sasa zimetengwa shilioni Bilioni 7 kwa ajili ya kukopesha vikundi vya wakina mama,vijana na watu wenye ulemavu”Alisema Mavunde Naye Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Alhaj Jabir Shekimweri anewataka maafisa wasafirishaji hao kutumia S...

Marekani yataka uchunguzi wa kina na wa harakankuhusu kifo cha ojwang

 Marekani imejiunga na Wakenya kulaani kifo cha mwalimu na mwanablogu, Albert Ojwang’, aliyefariki katika hali tata akiwa mikononi mwa polisi. Kupitia taarifa fupi iliyotolewa Jumatano, ubalozi wa Marekani jijini Nairobi ulisema unaunga mkono wito wa uwajibikaji na uwazi katika uchunguzi unaoendelea. “Kwa kuzingatia wasiwasi kuhusu mazingira ya kifo cha Ojwang’, Ubalozi unaunga mkono wito kutoka kwa serikali, wabunge, na wananchi wa Kenya wa kutaka uwajibikaji kupitia uchunguzi ulio wazi,” ilisema taarifa hiyo. Ubalozi pia umetaka Mamlaka Huru ya Kusimamia Utendakazi wa Polisi (IPOA) kupewa uwezo kamili wa kukamilisha uchunguzi wake bila vizingiti. “Ubalozi unahimiza Mamlaka Huru ya Kusimamia Utendakazi wa Polisi (IPOA) kuendesha uchunguzi wake kwa haraka na kwa kina. Tunaitaka pia serikali ya Kenya kuhakikisha IPOA inapata usaidizi na taarifa inazohitaji kutekeleza majukumu yake.” Wakati huo huo ubalozi huo pia ulituma rambirambi kwa familia na wapendwa wa marehemu Ojwang’. “Ubal...

Pigo kwa Upinzani Kenya,Baada ya Mahakama Kuu Kuharamisha Kampeni za Mapema kabla IEBC Kupuliza Kipenga

  KAMPENI za mapema nje ya kipindi kilichotengewa shughuli hiyo ni kinyume cha sheria na kanuni hitajika kwa uchaguzi huru na haki, Mahakama Kuu ya Kenya imeamua. Majaji Hedwig Ong’udi, Patricia Gichohi na Heston Nyaga walisema kuwa kampeni za mapema pia zinasababisha madhara mbalimbali kwa raia. Majaji hao walisema kampeni zinazoendeshwa nje ya kipindi cha uchaguzi zinavuruga haki ambazo raia wanapasa kufurahia kwa mujibu wa katiba. “Bila shaka kipindi cha uchaguzi hushuhudia taharuki za kisiasa, wasiwasi, kauli za kuleta migawanyiko hali inayorudisha nyuma shughuli pana za kiuchumi,” wakasema majaji hao, wakiongeza kuwa ipo haja kwa wanasiasa kukomesha kampeni na wajikite katika masuala ya maendeleo ili kuinua maisha ya raia. Majaji Ong’udi, Gichohi na Nyaga walitoa uamuzi huo katika Kesi iliyowasilishwa na shirika la kutetea haki, Kituo cha Sheria, kabla ya uchaguzi wa mkuu wa 2022. Kulingana na majaji hao, watu wakijikita katika kampeni za kisiasa, aghalabu, husahau majukumu na...

Kishindo Cha Mbunge Mathayo Chatua Kata za Mshikamano,Buhare,Iringo na Kigera

Na Shomari Binda-Musoma  KISHINDO cha ziara ya mbunge wa jimbo la Musoma mjini Vedastus Mathayo kuwashukuru wanachama wa Chama cha Mapinduzi ( CCM) kwa kumchagua uchaguzi wa mwaka 2020. Licha ya kuwashukuru wanachama hao ameelezea namna alivyotekeleza ilani ya uchaguzi kwa kipindi kinachokwenda kumalizika. Katika kituo chake cha kwanza akiwa Kata ya Mshikamano amesema ushirikiano alioupata kutoka kwa wanachama na wananchi ndio uliopelekea kutekeleza ilani ya uchaguzi. Amesema alishasoma utekelezaji huo na mengi yanaonekana na ruhusa aliyoipata bungeni kutoka kwa Spika ni kuja kuwashukuru na kuwaaga na muda ukifika wataonana tena. Mbunge huyo amesema kwenye elimu,afya,maji,miundombinu na masuala ya kijamii yamefanyika na kuondoa kero na changamoto kwa wananchi. Mathayo amesema kwa kuwa wananchi wameonyesha imani kwake  na kumuomba kugombea tena atafanya hivyo muda ukifika kwa kuwa bado anayo nguvu na ari ya kuwatumikia " Hii ni siku ya pili ya ziara yangu ya xiku 4 kuja kuwashu...

Jumuiya ya Ulaya yaipa Veta Bilioni 190 Kuhudumia Vijana

Na Mwandishi Wetu Tanga MKUU wa mkoa wa Tanga, Balozi Dkt Batlida Salha Burian, amekitaka Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) watakaosimamia mradi wa vijana wa (IncluCities) kuhakikisha wanapata vijana watakaokuwa tayari kujifunza na kuuheshimisha mradi huo. Aidha, alisema pamoja na hilo pia wachague vijana kutoka familia masikini ambao watakapojifunza na kufanya kazi watanufaisha familia zao mara baada ya kumaliza mafunzo ambayo yatamuwezesha kuondoka na zana zake za kazi. Akizungumza jana wakati alizindua mradi huo wa IncluCities, Mkuu wa mkoa alisema ni vema VETA wabuni mafunzo ambayo yatamuwezesha kijana akimaliza mafunzo hayo anakwenda moja kwa moja kujiajiri badala ya kusubiri kuajiriwa. "Vijana 350 watakaopata mafunzo ya mradi huu hakikisheni ni wale watakaojifunza kweli, lakini pia tazameni wale wanaotoka familia masikini ili wakimaliza waweze kuzisaidia familia zao kiuchumi," alisema Balozi Dkt Batlida. Alisema nchi zilizoendelea mfano China na Vietnam watoto wao wanajifunz...

Bilioni 3 za Umwagiliaji Kunufaisha zaidi ya Wakulima 490 skimu ya Mkotamo Ruvuma

📍NIRC:Tunduru MKUU WA WILAYA ya Tunduru Simon Chacha,amepongeza Tume ya Taifa ya Umwagiliaji(NIRC), kwa uwekezaji wa zaidi ya shilingi bilioni 3 kwaajili ya ujenzi wa miundo mbinu ya Umwagiliaji katika skimu ya Mkotamo, wilayani Tunduru Mradi huu unatarajiwa kunufaisha wakulima zaidi ya 497, kwa kulima eneo lenye ukubwa wa ekari 867 kwa kilimo cha mpunga na mbogamboga.  Akizungumza katika hafla ya utiaji saini ya ujenzi wa mradi huo, Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Simon Chacha alisema:   > “Kilimo ndicho uti wa mgongo wa uchumi wa wilaya yetu, hivyo serikali imewekeza katika miradi hii ili kuhakikisha wakulima wanapata msaada wa maji wa uhakika”,  Aidha, alibainisha kuwa skimu hii itawapa wakulima uwezo wa kulima mazao kwa mwaka mzima bila kutegemea mvua na hivyo kuongeza uzalishaji wa mazao Kwa upande wake, Mhandisi wa Umwagiliaji Mkoa wa Ruvuma, Lucia Chaula, ameongeza kuwa skimu hiyo inalenga kuimarisha kilimo endelevu kwa kulinda rasilimali za maji na mazingira....