Skip to main content

Posts

Showing posts from August 2, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

SGR Yaongeza Idadi ya Watalii Nchini

Na Zainab Ally-Mikumi. Ikiwa ni Siku moja baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan kuzindua Reli ya Mwendokasi (SGR) watalii ambao ni watumishi wa kada ya ualimu zaidi ya 1000 kutoka mkoa wa Dar es Salaam wametumia usafiri wa reli hiyo kutembelea Hifadhi ya Taifa Mikumi. Ziara hiyo iliyoratibiwa na Ofisi ya mkoa wa Dar es Salaam imelenga kuunga mkono juhudi mbalimbali zinazofanywa na Rais Samia ikiwemo kutangaza vivutio vilivyopo Hifadhi za Taifa ambapo kwa umoja wao walichagua Hifadhi  ya Taifa Mikumi lengo likiwa ni kuunga mkono juhudi za Rais Samia. Katibu Tawala wa mkoa wa Dar es salaam Dkt. Toba Nguvila, amesema kuwa watalii hao ambao ni walimu wa mkoa wa Dar es Saam wameamua kuchangisha fedha zao wenyewe kwa ajili ya kuja kutembelea Hifadhi ya Taifa Mikumi kwa kutumia usafiri wa reli ya kisasa ya SGR lengo likiwa ni kumuunga mkono Rais Samia. “Baada ya Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kuizindua reli hii, walimu wa mkoa wa Dar es Salaam w...

Taarifa ya Wizara ya Afya Kuhusu Ugonjwa Wa MPOX

  🟩 Mpaka sasa Tanzania ni salama na hakuna mgonjwa yoyote aliyepatikana na ugonjwa huo.   🟩 Ugonjwa wa Mpox unaweza kusambaa kutoka kwa mtu mwenye maambukizi kwenda kwa mwingine kwa njia zifuatazo; kupitia maji maji ya mwili ikiwemo mate, matapishi, jasho, mkojo, matone ya mfumo wa njia ya hewa na ngozi kupitia kugusana na kujamiana na mtu mwenye maambukizi ama kutumia vifaa, matandiko au kugusa sehemu zilizo na vimelea vya ugonjwa huu. Aidha, ugonjwa huu unaweza pia kuenezwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu.   🟩 Dalili kuu ya Mpox ni upele, malengelenge au vidonda kwenye mwili hasa, mikono na miguu, kifuani, usoni na wakati mwingine sehemu za siri. Dalili nyingine ni homa, uchovu, maumivu ya kichwa, misuli, mgongo, uchovu na kuvimba mitoki.    🟩 Ugonjwa huu haujaingia nchini, hivyo, ni vyema tukashirikiana kuhakikisha nchi yetu inabaki kuwa salama. Wizara inatoa tahadhari kwa Wananchi wote kuchukua hatua za kujikinga na ugonjwa wa huu kwa k...

Mwambukusi Ashinda Urais TLS 2024/2027

Boniface Mwambukusi ameshinda nafasi ya urais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika(TLS) 2024/2027 Kwa kura 1,274

Rais Samia Azindua Hospitali ya Wilaya ya Gairo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Hospitali ya Wilaya ya Gairo mara baada ya kuanza ziara yake ya kikazi Mkoani Morogoro tarehe 02 Agosti, 2024.

Fursa ya Ziara ya Kibiashara na Uwekezaji Nchini Comoro

Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kwa kushirikina ma Ubalozi wa Comoro pamoja na TPSF na TANTRADE tunapenda kuwaalika kwenye Ziara  ya Kibiashara na Uwekezaji.   Pia wameandaa Kongamano kwa wawekezaji na wafanyabiashara litakalo fanyika tarehe 21 Agosti 2024  katika Ukumbi wa Bunge Jijini Moroni nchini Comoro. Ziara hiyo  italenga Wadau  katika Sekta ya Usafirishaji , Kilimo na Ufugaji.  Ukiwa kama mmoja wa wadau  wa Sekta tajwa tunaomba  tuma taarifa zako ili tuweze kukusajili kwa hatua zaidi ikiwemo kujua gharama zitakazo husika katika Ziara hiyo. Chanzo: TIC