Skip to main content

Posts

Showing posts from July 18, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii
Mbunge wa jimbo la Chalinze na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe.Ridhiwani Kikwete leo Amefanya mkutano Kiwangwa na kuwapongeza wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha kwa mfumo wa Kidijitali Hata hivyo Mhe. RIdhiwani Amezunguka katika matawi mbalimbali na kuzungumza na wanachama wapya wa CCM na kuwasisitiza wananchi kuhusu uandikishaji wa kadi za kupiga kura kwaajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa vijiji na vitongoji pamoja na uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 . Pamoja na kukumbushana na kuwapongeza Wananchi , Ndugu Kikwete  amewakumbusha  wananchi wa Kiwangwa kuendelea kuiunga Mkono Serikali inayoongozwa na Rais @SuluhuSamia kutokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika maendeleo ya Kata ya Kiwangwa .

Simu Ndogo za Mkononi Kutumika Kuboresha Taarifa za Daftari La Kudumu La Mpiga Kura

Wapiga kura waliopo kwenye Daftari la Kudumu la Wapiga Kura wataweza kutumia simu zao ndogo za mkononi (vitochi au viswaswadu) kuanzisha mchakato wa kuboresha au kuhamisha taarifa zao. Kwa mujibu wa taarifa kwa umma iliyotolewa na Tume na kusainiwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Bw. Kailima Ramadhani leo tarehe 18 Julai, 2024, uamuzi huo wa Tume umetokana na maoni ya wadau wa uchaguzi. “Tume imefanyia kazi maoni na ushauri huo (wa wadau) na kuanzia tarehe 20 Julai, 2024 watu wote wenye simu za kawaida (maarufu kama kitochi au kiswaswadu) na watahitaji kuboresha au kuhamisha taarifa zao, watapata huduma hiyo kwa kupiga USSD Code *152*00# na kubonyeza namba 9 kisha kuendelea na hatua zingine kama itakavyokuwa inaelekezwa kwenye simu husika,” inasomeka sehemu ya taarifa hiyo. Taarifa hiyo imefafanua kuwa mpiga kura anayetumia njia hii atapokea namba maalum (token) kupitia simu yake kisha atalazimika kwenda na namba hizo kwenye kituo anachotarajia kutumia kupi...

Teknolojia ya Ecoroads Yaonesha Mafanikio Katika Ujenzi wa Barabara Nchini

Na. Catherine Sungura-Chamwino Teknolojia ya kisasa ya ujenzi wa barabara kwa kuboresha udongo kabla ya kuweka lami juu  ijulikanayo kama ‘Ecoroads’ imeonesha matumaini katika miezi sita ya majaribio.  Hayo yameelezwa na Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-TAMISEMI anayeshughulikia  miundombinu  Mhandisi Rogatus Mativila mara baada ya kutembelea Barabara  zilizojengwa na teknolojia hiyo yenye urefu wa Km. 6.95 wilayani Chamwino. Mhandisi Mativila amesema kwamba lengo kubwa la kutembelea barabara hizo ni kujionea mafanikio ya matumizi ya teknolojia hiyo ambayo pia inajaribiwa katika wilaya mbalimbali nchini na inatekelezwa  na Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA). “Lengo la kuja kutembelea barabara hii hapa Chamwino ni kuangalia mafanikio ya matumizi ya teknolojia hii ya kisasa ya kuboresha udongo kabla hatujaweka lami juu inayotekelezwa na TARURA”. Amesema teknolojia hiyo pia inafanyiwa majaribio huko Mufindi, Rufiji na maeneo mengine ili kuweza ku...

Polisi Kenya Yapiga Marufuku Maandamano Katika Mji wa Nairobi

Idara ya Huduma ya Polisi nchini Kenya imepiga marufuku maandamano katika mji wa Nairobi na viunga vyake na kutoa hakikisho la usalama katika eneo hilo. Katika taarifa yake iliyotolea Julai, 17, 2024, imekumbusha umma jukumu muhimu la idara hiyo katika usalama wa nchi kulingana na katiba. Hayo yamejiri huku Kenya ikiendelea kushuhudia maandamano ambayo yalianza tangu mwezi Juni, kupinga Mswada wa Fedha 2024. ‘’Nchi yetu imekuwa ikishuhudia hasara kubwa, watu wamejeruhiwa, kupoteza maisha, mali na biashara zimeharibiwa,’’ taarifa ya Idara ya Huduma ya Polisi ilisema. Iliendelea kusema kuwa imepokea taarifa kwamba baadhi ya makundi ya kihalifu yanapanga kutumia vibaya maandamano ya siku ya Alhamisi, Julai 18, 2024 kutekeleza mashambulizi na uhalifu. Idara hiyo ilielezea ukosefu wa uongozi kuwa imefanya kuwa vigumu kufanyika kwa maandamano ya amani katika siku zilizopita. "Kukosekana kwa uongozi katika maandamano yaliyopita kumefanya kuwa vigumu kuhakikisha itifaki za usalama zinafua...

Biden Akutwa na Virusi vya Corona

Rais wa Marekani Joe Biden alithibitishwa kuwa na COVID-19 jana (Jumatano), taarifa kutoka Ikulu ya White House ilisema. " Mapema leo baada ya tukio lake la kwanza huko Las Vegas, Rais Biden alipimwa na kupatikana na COVID-19. Amepewa chanjo na kuongezewa nguvu, na ana dalili zisizo kali", Katibu wa Vyombo vya Habari wa Ikulu ya White House Karine Jean-Pierre alisema katika taarifa. "Atarudi Delaware ambapo atajitenga na ataendelea kutekeleza majukumu yake kwa ukamilifu wakati huo", alisema.