Na Ada Ouko GMTV Musoma. JESHI la polisi mkoa wa Mara linawashikilia watu watatu wa familia moja wakazi wa Mtaa Nyabisare Kata ya Bweri kwa tuhuma za mauaji ya Chacha Mwita (55) ambaye alikuwa ni Baba mzazi wa familia hiyo. Kamanda wa polisi mkoa wa Mara amethibitisha kutokea kwa tukio hilo Agosti 20,2025 na kuwataja watuhumiwa hao kuwa ni Matiku Chacha Manyengo(22), Mwajuma Chacha Nyamsiwa(45) na Manyengo Chacha Manyengo(26) ambapo walikuwa wakifanya shughuli za kilimo. "Agosti 14,2025 Jeshi la polisi mkoa wa Mara lilipokea taarifa kutoka kwa watuhumiwa hao kuhusu kupotea kwa ndugu yao ambaye ni mume wa Mwajuma pia ni Baba mzazi wa watumiwa Matiku na Manyengo, mara baada ya kupata taarifa hiyo Jeshi la polisi mkoa wa Mara lilianza uchanguzi mara moja" Amesema Lutumo. Katika uchunguzi wa tukio hilo Kamanda Lutumo amesema jeshi hilo lilibaini kuwa Julai 29, 2025 saa tatu asubuhi nyumbani kwa marehemu kulitokea ugomvi baina ya marehemu na mke wake, ambapo watoto wa marehemu w...