Skip to main content

Posts

Showing posts from February 12, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Majaliwa Aitaka Tarura Kuwasimamia Wakandarasi Binafsi

*▪️Asisitiza Serikali itaendelea kuwawezesha wawekezaji wazawa* *▪️Aeleza mpango wa Serikali wa kukabiliana na ugonjwa wa Malaria nchini* Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameitaka Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) ihakilishe inatoa kandarasi za ujenzi na ukarabati wa barabara kwa wakandarasi wenye uwezo wa kujenga kwa viwango vinavyoendana na thamani ya fedha. Ameyasema hayo leo (Alhamisi, Februari 13, 2025) wakati akijibu swali la Mbunge wa Kinondoni, Abbasi Tarimba  aliyehoji kwanini Serikali isianze kutumia vikosi kazi vya Manispaa au TARURA badala ya wakandarasi binafsi katika ukarabati wa barabara zilizoharibika, katika kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu, bungeni jijini Dodoma. “Tunaitaka TARURA iwasimamie wakandarasi binafsi wanapopewa kazi, wawe na uwezo wa kujenga barabara za kudumu kwa mujibu wa viwango vilivyopo ili barabara ziweze kutumika kwa muda mrefu. ” Amesema kuwa awali mfumo wa ujenzi wa barabara za vijijini uliokuwa unaruhusu Halmashauri kukarabati ba...

Tanzania yatumia wiki ya nishati india kunadi vitalu vya mafuta na gesi asilia nchini

📌 *Lengo ni kuvutia uwekezaji katika Mafuta na Gesi Asilia Bahari kuu na Nchi kavu* 📌 *Dkt. Biteko aipongeza PURA kutumia majukwaa Kimataifa kutafuta wawekezaji*    📌 *Atilia mkazo uendelezaji wa vyanzo vyote vya nishati* 📌 *Vitalu 26 vya Mafuta na Gesi Asilia kunadiwa* *Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati* Serikali kupitia Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli Tanzania (PURA) imeendelea kuhamasisha wawekezaji mbalimbali duniani kushiriki katika Duru ya Tano ya Kunadi Vitalu vya utafutaji wa Mafuta na Gesi Asilia katika Bahari Kuu ya Hindi na Nchi Kavu itakayozinduliwa mwezi Machi mwaka huu. Matangazo ya fursa za uwekezaji kwenye Sekta ya Mafuta na Gesi Asilia yanaendelea kupitia Kongamano na Maonesho ya Wiki ya Nishati ya India yanayofanyika katika Jiji la New Delhi, India tukio ambalo linawashirikisha zaidi ya watu 70,000 kutoka nchi zaidi ya 50 Duniani.  Katika Banda la Tanzania kwenye Maonesho hayo washiriki wengi wamevutiwa na taarifa za k...

Waziri Mkuu Akijibu Maswali ya Wabunge Leo Bungeni Jijini Dodoma

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akijibu maswali ya Wabunge, wakati wa kipindi cha maswali kwa Waziri Mkuu, bungeni jijini Dodoma, Februari 13.2025.

Balozi Dkt Nchimbi Akutana na Viongozi wa Mataifa Manne Wanaowakilisha Nchi zao Hapa Nchini

  1. Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwa kwenye mazungumzo na Naibu Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Mhe. Andrew Lentz, ofisini kwa Balozi Nchimbi, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, leo Jumatano tarehe 12 Februari 2025. 2. Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akizungumza na Balozi wa India nchini Tanzania, Mhe. Bishwadip Dey, walipokutana kwa ajili ya mazungumzo, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, leo Jumatano tarehe 12 Februari 2025. 3. Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akizungumza na Balozi wa Algeria nchini Tanzania, Mhe. Ahmed Djellal, ambaye alifika ofisini kwa Balozi Nchimbi, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM, Lumumba, jijini Dar Es Salaam, kwa ajili ya kuaga, leo Jumatano tarehe 12 Februari 2025. 4. Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akizungumza n...

Waziri Mkuu Akutana Na Ujumbe Wa Wafanyabiashara Kutoka Falme Ya Saudi Arabia

▪️Awaeleza mikakati ya Tanzania katika kuvutia wawekezaji. ▪️Awakaribisha kuwekeza kwenye Sekta ya Nishati   Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali itaendelea kuweka mazingira bora ya uwekezaji nchini ili kuendelea kuwavutia wawekezaji. Ameyasema hayo leo,  (Jumatano 12 Februari 2025) alipokutana na Ujumbe wa Wafanyabiashara kutoka Falme ya Saidi Arabia, Katika Ofisi ndogo ya Waziri Mkuu magogoni jijini Dar es Salaam. Mheshimiwa Majaliwa amesema uhusiano baina ya Tanzania na Saudi Arabia umeendelea kuimarika na kufungua fursa kwa wawekezaji kutoka Saudi Arabia kuwa na wigo wa kuwekeza nchini Tanzania hususan katika sekta za nishati, Kilimo, Viwanda, Mifugo Utalii na biashara. Aidha, amesema Tanzania imeendelea kunufaika na fursa ya kusafirisha bidhaa za mazao na mifugo kwenda nchini Saudi Arabia jambo ambalo limeendelea kukuza uchumi wa nchi. Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa wawekezaji hao kuwekeza katika sekta ya nishati ili kuongeza nguvu kati...