Na Mwandishi Wetu, Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Profesa Riziki Shemdoe, ameipongeza Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma kwa kuandaa mpango wa kuwapeleka walimu 40 kwenda kusoma Korea Kusini, akieleza kuwa ni hatua muhimu ya kuimarisha ubora wa elimu nchini. Akizungumza katika Mkutano wa Wadau wa Elimu Mkoa wa Dodoma uliofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini hapa, Waziri Shemdoe alisema mpango huo unaendana na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha sekta ya elimu nchini. “Mpango huu unaonyesha dhamira ya kweli ya kuboresha elimu kupitia uwekezaji kwa walimu. Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi kama hizi,” alisema Profesa Shemdoe. Mkutano huo uliandaliwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule, kwa lengo la kuhamasisha walimu, wanafunzi na watendaji wa halmashauri kuongeza juhudi katika kuboresha ufaulu wa elimu mkoani humo. Akizungumza katika mkutano huo, Senyamule alisema mafanikio y...
Marato tv - Sauti ya Jamii