Skip to main content

Posts

Showing posts from April 14, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Deo Mwanyika Aitaka Serikali Kusimamia Vibali kwa Wawekezaji wa Misitu

Na Mwandishi Wetu, Dodoma Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini, Mhe. Deo Mwanyika, ameishauri serikali kutokuwa na haraka kutoa vibali kwa wawekezaji wa sekta ya misitu wasiowekeza katika kuongeza thamani ya mazao ya misitu mkoani Njombe. Akichangia Hotuba ya Waziri Mkuu bungeni jijini Dodoma, Mhe. Mwanyika aliipongeza serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika jimbo hilo, ikiwemo sekta za elimu, afya, maji, barabara, na umeme vijijini. Katika sekta ya maji, Mbunge huyo alibainisha kuwa miradi ya Ijunilo na Livingstone tayari imekamilika na inaendelea kutoa huduma ya maji kwa wakazi wa Mji wa Njombe, hali iliyosaidia kupunguza mgao wa maji. Aidha, miradi ya Hagafilo na ya majitaka inaendelea na itakapokamilika, inatarajiwa kuongeza upatikanaji wa maji kwa wakazi wa mji huo. Kuhusu umeme, alisema vijiji vyote katika jimbo lake tayari vimeunganishwa na huduma hiyo, na kwa sasa juhudi zinaelekezwa katika vitongoji. Alito...

Makalla apokelewa kwa kishindo Mtwara

  MTWARA: Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), CPA Amos Makalla amehitimisha ziara yake katika Mkoa wa Lindi na kupokelewa katika Mkoa wa Mtwara kwa ajili ya kuanza ziara yake mkoani humo. Makalla amewasili na kupokelewa mkoani Mtwara leo Aprili 14,2025 katika Kijiji cha Mpapula na kuelekea katika Ofisi za CCM Mkoa wa Mtwara. Makalla anatarajiwa kuwa na mkutano wa Hadhara katika Uwanja wa Shule ya Msingi Chikongola Mtwara Mjini.

Mbunge Muhongo Ataja Ajira za Nje ya Nchi Kama Fursa Nyingine Kuinua Uchumi

Na Shomari Binda-Musoma.  MBUNGE  wa jimbo la Musoma Vijijini Profesa Sospeter Muhongo ametaja ajira mpya za nje ya nchi kama fursa nyingine ya kuinua uchumi. Hayo ameyasema leo aprili 14 bungeni jijini Dodoma wakati akitoa mchango wake alipokuwa akichangia bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwenye Kikao cha 5 cha Mkutano wa 19 wa Bunge la 12. Amesema ajira za nje ya nchi  ni bidhaa mpya duniani ambayo ambayo mwaka jana 2024 ilikuwa na thamani ya dola za kimarekani bilioni 905. Muhongo amesema sifa ya ajira ni elimu na mafunzo na ajira kubwa inatokana na sekta binaafsi na sio lazima kuajiliwa Tanzania bali mataifa ya Ulaya,Marekani na mengineyo. Mbunge huyo ameyataja meneo manne yakiwemo ya afya na teknolojia ambayo yana nafasi kubwa ya ajira nje ya nchi kwenye sekta binafsi. Amesema umuhimu wa kazi za nje ni vijana kupata ajira na taifa kupata fedha za nje ambazo zitaendelea kuongeza uchumi wa taifa na vijana wenyewe. Awali akitoa mchango wake amezungumzia Sera ya Taifa ya M...

Dr.Wilson Mukama Apongezwa Kwa Kujitoa Kusaidia Jamii Mkoa wa Mara

Na Shomari Binda-GMTV KADA wa Chama cha Mapinduzi ( CCM) Dr.Wilson Maregesi Mukama amepongezwa kwa kuguswa na kusaidia jamii ya mkoa wa Mara maeneo mbalimbali. Mukama amekuwa akisaidia jamii kwenye masuala ya afya,elimu,maji,michezo na masuala mengine kwenye jamii. Hivi karibuni kwenye sekta ya michezo alipokuwa mgeni rasmi akifunga michezo ya Umitashumta mkoa wa Mara wilayani Tarime Dr.Mukama alichangia kiasi cha shilingi milioni 4 kwa timu ya mkoa kwaajili ya zawadi na maandalizi ya timu ya mkoa. Akizungumza na GMTV kuhusiana na namna anavyoguswa na kuchangia Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Bunda kupitia ( UV-CCM) CDE.Fadhili Maneno amesema Chama cha Mapinduzi kinayo hazina ya kutosha ya watu wanaojitoa na kusaidia jamii. Amesema Dr.Mukama amekua akisaidia jamii mara kwa mara kwenye maeneo mbalimbali na amekuwa mfano wa kuigwa. CDE.Fadhili amesema suala la kutoa na kuchangia kwenye jamii sio kila mtu anaweza kufanya hivyo lakini kwa Dr.Mukama amekuwa akifanya hivyo mara zo...

Tanzania Kuwa Mwenyeji Katika Tuzo Za Mwaka 2025

Tanzania imepewa heshima ya kuwa mwenyeji wa hafla ya kutangaza washindi wa Kanda ya Afrika na Bahari ya Hindi, iitwayo "Africa & Indian Ocean Gala Ceremony" itakayofanyika tarehe 28 Juni, 2025 jijini Dar es Salaam. Aidha, Bodi ya Utalii Tanzania kama Taasisi yenye jukumu la kutangaza Utalii nchini ndio itaratibu hafla hiyo. Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo, Aprili 14,2025, jijini Dar-es-Salaam, Mkurugenzi Mkuu Bodi ya Utalii, Ephraim Balozi Mafuru amesema kuwa mchakato wa kupiga kura kwa kanda ya Afrika na Bahari ya Hindi ulifunguliwa rasmi tarehe 11 Machi, 2025 na utafikia tamati tarehe 4 Mei, 2025. Nchi yetu imetajwa katika vipengele zaidi ya 15 ikiwemo Nchi inayoongoza kwa Utalii Afrika (Africa's leading Destination) - Tanzania,Bodi bora ya Utalii Afrika (Africa's leading Tourist Board) - Bodi ya Utalii Tanzania, Kivutio Bora cha Utalii Barani Afrika (Africa's leading Tourist Attraction) Ngorongoro, Mlima unaoongoza Afrika - Mlima Kilimanjaro....

Viongozi wa CCM katika picha Zanzibar

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar, ambaye pia ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, akiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, na Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais  Mstaafu wa Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein, walipokutana Ikulu Zanzibar leo Jumatatu, tarehe 14 Aprili 2025. Mwingine pichani ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dkt. Mohamed Said Mohamed Dimwa.

Wanawake Wachangia 35% ya Pato la Taifa

  📌 Dkt. Biteko afungua Mkutano wa TAWiFA 📌 Dkt. Biteko awataka wanawake kuwekeza katika teknolojia kufikisha huduma vijijini 📌 Uwekezaji kwa wanawake si hisani ni kimkakati kwa maendeleo ya Taifa Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Wanawake nchini Tanzania wametajwa kuwa na mchango mkubwa katika Pato la Taifa ambapo takwimu zinaonesha kuwa asilimia 35 ya uchumi wa Tanzania unatokana na juhudi za wanawake ambao wanachangia asilimia 70 ya nguvu kazi ya kilimo ni wanawake hasa katika mazao ya chakula. Mchango wa mwingine wa wanawake unajidhihirisha katika biashara, viwandani na katika huduma za kifedha kupitia utafiti uliofanywa na Chama cha Mabenki Tanzania (TBA) mwa ka 2022 umeonesha wanawake ni 47% ya wafanyakazi wote wa sekta ya fedha. Pia wanashika 10% ya nafasi za kufanya maamuzi. Vile vile, 18% wakiwa wajumbe katika bodi za wakurugenzi sawa na wastani wa wanawake wawili katika kila bodi. Hayo yamebainishwa leo Aprili 14, 2025 jijini Dodoma na Naibu Waziri Mkuu n...