Skip to main content

Posts

Showing posts from December 19, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Dkt. Mwigulu Akagua Ujenzi Wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 20, 2025 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Lindi pamoja na kusalimia baadhi ya wananchi wanaopata huduma katika hospitali hiyo.

Waziri Mkuu Akagua Mradi Unaojengwa Kwa Ushirikiano na Mradi wa Lng na Tpdc, Lindi

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 20, 2025 amekagua maendeleo ya mradi wa shule mpya ya msingi ya Likong’o inayojengwa kwa ushirikiano na Mradi wa LNG na TPDC. Shule hiyo iliyopo katika kijiji cha Likong’o itagharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.2 pale itakapokamilika, ambapo kati ya fedha hizo, Serikali imechangia asilimia 26.6, kampuni ya Shell imechangia asilimia 36.6 na kampuni ya Equinor imechangia asilimia 36.6. Akizungumza na wakazi wa eneo hilo, Dkt. Mwigulu ametoa wito kwa wakazi wa eneo hilo na  Tanzania kwa ujumla kuwapeleka watoto wao shuleni kwani Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweka mazingira wezeshe katika sekta ya elimu yanayowafanya watoto wa kitanzania kupata elimu bora. “Rais Dkt. Samia aliahidi ajira za walimu katika siku 100, sasa usaili umefanyika na walimu 7000 wataajiriwa na itakapofika Januari 10, 2026 walimu hawa wataripoti katika vituo vya kazi watakavyopangiwa” Naye, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI Reuben Kwagilwa amesema kuwa Rais...

Mbunge Agness Marwa Aendelea Kumwaga Misaada Musoma Mjini

 MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Mara mh Agnes Mathew Marwa amekabidhi mchango wa saruji na mchanga kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa ofisi ya mtendaji wa kata ya Bweri katika halmashauri ya Manisipaa ya Musoma mkoani Mara. Mchango huo umekabidhiwa na diwani wa viti maalum katika halmashauri ya Manispaa ya Musoma Mh Sister Yohana kwa niaba ya mbunge Agness Marwa katika kikao cha kwanza cha maendeleo cha kata ya Bweri chini ya uenyekiti wa diwani wa kata hiyo Paul Katikiro. Akizungumza wakati wa kukabidhi mifuko mitano ya saruji na mchanga kwa ujenzi wa ofisi hiyo hiyo inayotumiwa pia na diwani wa kata ya Bweri,Mh Sister Yohana,amesema mbunge Agness kama kada wa CCM, ametoa mchango huo ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono kazi kubwa inafanywa na watendaji wa serikali pia itamwezesha diwani kupata sehemu nzuri ya kufanyia kazi katika kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabioi wananchi wa kata yake Amesema kama mbunge wa viti maalum mkoa wa Mara anayetokana na CCM, ataendelea kusaidia ujen...

Mbunge Agness Marwa achangia ujenzi ofisi ya CCM kata ya Bweri Musoma mjini

MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Mara mh Agnes Mathew Marwa amekabidhi mchongo wa saruji na mchanga kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya chama cha Mapinduzi kata ya Bweri katika halmashauri ya Manispaa ya Musoma mkoani Mara. Mchango huo umekabidhiwa na diwani wa viti maalum katika halmashauri ya Manispaa ya Musoma Mh Sister Yohana kwa niaba ya mbunge Agness Marwa katika kikao cha kwanza cha maendeleo cĥa kata ya Bweri chini ya uenyekiti wa diwani wa kata hiyo Paul Katikiro. Akuzungumza wakati wa kukabidhi mifuko ya saruji na mchanga kwa ujenzi wa ofisi hiyo ya CCM kata ya Bweri,Mh Sister Yohana, amesema mbunge Agness kama kada wa CCM, ametoa mchango huo katika sehemu ya kuunganisha kazi kubwa inafanywa na viongozi wa CCM katika kuisimamia Serikali yake. Amesema kama mbunge wa viti maalum mkoa wa Mara anayetokana na CCM, ataendelea kusaidia ujenzi wa ofisi za chama na miradi mingine ya Maendeleo katika kuunga mkono juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt Samia S...

Dkt. Kijaji: Tanapa, Tawa Nendeni na Kasi ya Rais Samia Kuchechemua Utalii

Na Sixmund Begashe, Iringa WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji, amezitaka taasisi za uhifadhi nchini, Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), kuongeza kasi ya kuhamasisha utalii wa ndani ili Watanzania waweze kunufaika moja kwa moja na matokeo chanya ya uhifadhi wa rasilimali za utalii. Dkt. Kijaji ametoa wito huo wakati wa kikao chake na menejimenti ya Wizara ya Maliasili na Utalii, pamoja na viongozi wakuu wa TANAPA na TAWA, kilicholenga kutathmini utekelezaji wa mikakati ya kukuza sekta ya utalii nchini. Amesema kasi ya kuchechemua utalii na kuimarisha uhifadhi endelevu Kusini mwa Tanzania, inayotekelezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo, inapaswa kuungwa mkono kwa nguvu zote na taasisi zote zilizo chini ya Wizara hiyo. Amebainisha kuwa Tanzania imejaliwa kuwa na utajiri mkubwa wa vivutio vya asili, hususan katika ukanda wa kusi...

Naibu Waziri aipongeza CBE kwa maboresho ya miundombinu

Na Mwandishi Wetu NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Patrobas Katambi, ameipongeza menejimenti ya Chuo cha Elimu ya Biashara CBE kwa uongozi mzuri na maendeleo yaliyopatikana ndani ya kipindi cha muda mfupi. Naibu Waziri Katambi aliyasema hayo jana jijini Dar es salaam, alipotembelea chuo hicho ikiwa mwendelezo wa ziara zake za  kujitambulisha kwenye taasisi mbalimbali zilizo chini  ya wizara hiyo. “Marais wote waliopita waliona umuhimu wa kuendeleza chuo hiki nawapongeza nyinyi kwa mpango mkubwa wa upanuzi wa chuo na katika utoaji wa huduma kwa watanzania. Mmeweza kwenda Dodoma, Mwanza, Mbeya na sasa Kilimanjaro ni hatua kubwa sana kuwafikia kokote waliko badala ya wote kulazimika kuja Dar es Salaam wanasoma huko huko waliko,” alisema. Alisema CBE imefanikiwa kuongeza madarasa, maeneo ya wazi ya kupumzikia, kupanua maeneo ya madarasa majengo ya utawala na maeneo ya bweni. “Nimeona jengo kubwa la metrolojia litakalogharimu shilingi bilioni 26 ambalo limefikia zaidi ya asilim...

Wastaafu Elfu 50 Kupatiwa Vitambulisho vya Kielektroniki

Na. Mwandishi Wetu-Dodoma DODOMA:Wastaafu wanaolipwa na Serikali wapatao 609 katika Wilaya ya Dodoma Mjini, wamepatiwa vitambulisho vya kielektroniki katika zoezi la kugawa vitambulisho hivyo linalotekelezwa na Wizara ya Fedha ambapo inalenga kuwafikia wastaafu wapatao elfu 50 nchini. Hayo yalibainishwa na Mhasibu Mkuu wa Serikali Msaidizi- Huduma za Mfuko Mkuu, Wizara ya Fedha Perfectus Killenza, alipokuwa akitoa taarifa ya maendeleo ya zoezi la kutoa vitambulisho vya kielektoniki kwa wastaafu kutoka Wilaya ya Dodoma Mjini, linaloendelea katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square jijini Dodoma. Killenza alisema kuwa vitambulisho vya kielektroniki ni salama, imara na vinaondoa changamoto zilizokuwepo awali za vitambulisho vya karatasi ambavyo vilikuwa vikiharibika kwa urahisi na kufanya taarifa zisomeke kwa shida. “Vitambulisho hivi vipya vitarahisisha upatikanaji wa huduma kwa wastaafu wetu kwa kuwa taarifa zao zitasomeka kwa urahisi kwa njia ya kielektroniki, sambamba na kuonge...

Dkt.Mwigulu akagua maendeleo ya ujenzi wa Madaraja Lindi

_Asisitiza Rais Dkt. Samia amedhamiria kushughulika kwa vitendo na umasikini wa watanzania_ WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 19, 2025 amekagua maendeleo ya ujenzi wa Madaraja na Ukarabati wa barabara kuu ya Marendego-Nangurukuru-Lindi-Mingoyo Akizungumza baada ya ukaguzi huo, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amewaambia wakazi wa Somanga mkoani Lindi kuwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatekeleza miradi ya kimkakati ili kushughulika kwa vitendo na umasikini wa Watanzania Amesema kuwa Rais Dkt. Samia alisimamia ukamilishaji wa Bwawa la Kuzalisha Umeme la Julius Nyerere ili kuhakikisha kila mtanzania ananufaika na huduma ya nishati ya umeme.  “Tumeshuhudia Rais Dkt. Samia namna anavyotekeleza miradi kwenye sekta mbalimbali ikiwemo uvuvi, maji, kilimo, afya, elimu na hata uwezeshaji wananchi kiuchumi