Skip to main content

Posts

Showing posts from January 26, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Miaka 65 ya Maisha ya Rais Samia, Safari yake Ya Kusisimua Kutoka Karani Masijala Hadi Mkuu wa Nchi

Na Bwanku M Bwanku. Leo Januari 27, 2025 Taifa letu linasherehekea miaka 65 toka kuzaliwa kwa Rais wa sasa wa Awamu ya 6 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, anayehudumu kwa mara ya kwanza kwenye nyadhifa ya juu kabisa nchini toka achukue mikoba hiyo Machi 19, 2021 baada ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Awamu ya 5 Hayati John Pombe Magufuli. Kwa wasiyemfahamu sana, Rais Samia, ndiye Mwanamke wa kwanza katika historia ya Tanzania kushika nafasi ya Urais wa Tanzania baada ya pia kuwa Mwanamke wa kwanza kushika nafasi ya Makamu wa Rais mwaka 2015 hadi 2021, nafasi kuu za juu kabisa katika Taifa letu. Rais Samia Suluhu Hassan alizaliwa Januari 27, 1960 katika Kijiji cha Kizimkazi kilichopo Jimbo la Makunduchi, Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja Visiwani Zanzibar, kabla ya kuanza masomo yake ya Msingi katika shule mbalimbali ikiwemo Shule ya Msingi Chwaka kuanzia mwaka 1966 hadi 1968, kisha Ziwani mwaka 1970 na baadae Shule ya Msingi Mahonda mwaka 1972. Baadae...

CCM Mkoa wa Mara yamtakia Heri ya Kuzaliwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan

Na Shomari Binda-Musoma  CHAMA cha Mapinduzi ( CCM)mkoa wa Mara kinaungana na watanzania kumtakia heri ya kuzaliwa Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan Salam hizo zimetolewa na Katibu wa CCM mkoa wa Mara Ibrahim Mjanakher alipokuwa akizungumza na GMTV ofisini kwake. Amesema katika siku ya leo januari 27 inaposherehekewa siku ya kuzaliwa ya Dkt.Samia CCM mkoa wa Mara na wananchi hawana budi kumpongeza kwa mazuri aliyoyafanya kwenye mkoa. Amesema kwa kipindi kifupi mkoa umepokea zaidi ya tilioni 1 kwaajili ya miradi mbalimbali ya maendeleo. Mjanakher amesema ukifika mkoa wa Mara utaona mabadiliko makubwa zikiwemo shule nzuri zilizojengwa,hospitali,miradi ya maji,barabara na mingineyo. Amesema kutokana na mazuri hayo wana kila sababu ya kumpongeza na kumtakia heri katika siku yake ya kuzaliwa. " Tunamuombea maisha marefu Mama Samia na kumtakia majukumu mema anapokuwa anawahudumia watanzania hapa nchini. " Ukifika...

Biteko afungua Mkutano wa Nishati wa nchi za Afrika

  Matukio katika picha wakati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akifungua Mkutano wa Nishati wa Nchi za Afrika (Africa Energy Summit) katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere(JNICC) jijini Dar es Salaam, leo tarehe 27 Januari 2025.  Ministers and sector leaders from across Africa gather today (day 1) at the Julius Nyerere International Convention Centre in Dar es Salaam, Tanzania, for Ministerial & Partnerships Day at the Mission 300 Africa Energy Summit. Held on January 27, 2025, the summit—hosted by Tanzania, the African Union, the African Development Bank, and the World Bank—aims to accelerate electricity access for 300 million people by 2030. Mission 300 Africa Energy Summit: Ministerial & Partnerships Day.