Skip to main content

Posts

Showing posts from September 13, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

KIWANDA KIKUBWA CHA KUCHAKATA MCHANGA MZITO WA BAHARINI(HMS) BARANI AFRIKA KUJENGWA PANGANI,TANGA*

 ▪️Ni cha Kampuni ya Madini ya Shenghe ambacho ujenzi wake umeanza ▪️Madin ya mchanga mzito kutoka nchi mbalimbali Afrika kuchakatwa Pangani,Tanga ▪️Waziri Mavunde apongeza hatua ya kuifanya Tanzania kitovu cha uongezaji thamani madini Afrika ▪️Awataka wawekezaji kukamilisha ujenzi wa kiwanda mapema ▪️Rais Samia apongezwa kwa mazingira rafiki ya uwekezaji Chengdu,China Kampuni ya Shenghe Resources ya China imeanza ujenzi wa kiwanda kikubwa cha kuchakata madini madini ya mchanga mzito wa baharini (𝙃𝙚𝙖𝙫𝙮 𝙈𝙞𝙣𝙚𝙧𝙖𝙡 𝙎𝙖𝙣𝙙𝙨) katika eneo la Tajiri,Wilaya ya Pangani Mkoani Tanga ambapo kampuni hii inatekeleza mradi mkubwa wa uchimbaji wa madini tembo. Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Shenghe Ndg. Xie Bing wakati wa ziara ya Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde kutembelea na kujionea shughuli mbalimbali za uongezaji thamani madini zinazofanywa kampuni hiyo. Akizungumza katika ziara hiyo Ndg. Bing amesema kwa Bara la Afrika wana miradi ya madin...

PSPTB YATOA SIKU 30 KWA WATAALAMU WA UNUNUZI NA UGAVI KULIPA ADA YA MWAKA

 BODI ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) imewapa siku 30 wataalamu wote waliosajiliwa ambao wana madeni ya ada ya mwaka kuhakikisha wanalipa, ikionya kuwa watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo wanaweza kufutiwa usajili na kuchukuliwa hatua za kisheria. Agizo hilo limetolewa leo Septemba 14, 2026 na Mkurugenzi Mtendaji wa PSPTB, Godfred Mbanyi wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu ulipaji wa ada ya mwaka ya wanachama wa Bodi hiyo. Amesema ulipaji wa ada ya mwaka ni wajibu wa kisheria kwa kila mtaalamu aliyesajiliwa na PSPTB, kwa mujibu wa Sheria ya PSPTB, Sura ya 179 ya Sheria za Tanzania, pamoja na kanuni zinazosimamia taaluma hiyo. Mbanyi amesema kuwa mtaalamu anayeshindwa kulipa ada kwa kipindi cha miezi 24 mfululizo atachukuliwa kuwa amepoteza hadhi ya usajili na jina lake linaweza kuondolewa katika daftari rasmi la wataalamu waliosajiliwa na Bodi. Bodi pia imeonya kuwa mtu ambaye ataendelea kufanya kazi, kujitambulisha au kujihusisha na taaluma ya ununuzi na uga...

MWANAFA ANOGESHA 'AWESO CUP' PANGANI, AAHIDI SKAUTI KUSAKA VIPAJI

 * Ampongeza Aweso kwa kuandaa timu 80, ashangaa kuizidi Ligi Kuu. *Na Mashaka Mhando, Pangani NAIBU Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Hamis Mwinjuma maarufu 'MwanaFA', amekuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mashindano makubwa ya soka ya 'Aweso Cup' yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Sakura, wilayani Pangani. Akizindua mashindano hayo kwa kupiga penalti ya kifundi, MwanaFA alimmwagia sifa Mbunge wa Pangani ambaye pia ni Waziri wa Maji, Jumaa Aweso, kwa kuwekeza kwenye michezo na kufanikiwa kukusanya timu takribani 80 kutoka kata 14 za jimbo hilo. "Hongera Mheshimiwa, timu 80 siyo mchezo! Umeishinda hata Ligi Kuu yetu yenye timu 16 tu. Hili ulilolifanya si jambo dogo," alisema MwanaFA kwa mshangao. MwanaFA alibainisha kuwa Serikali imeweka mpango madhubuti wa kuhakikisha kila yanapofanyika mashindano ya mpira wa miguu, haijalishi yana udogo gani, inapeleka skauti kutoka Shirikisho la Soka Nchini (TFF) kusaka vipaji ili kuvilea kama inavyofanya kwa timu za...