Skip to main content

Posts

Showing posts from July 2, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

WATANZANIA SASA KUJIPIMA UTI WAKIWA NYUMBANI

 …..Ni kwa kutumia kipimo cha Checkfor UTI Test Na Mwandishi Wetu Tanzania imeendelea kupiga hatua katika sekta ya afya ambapo kipimo kipya cha UTI kinachomwezesha mtu kujipima akiwa nyumbani na kugundua kuwa amepata maambukizi ya ugonjwa huo kimeanza kutumika hapa nchini. Kipimo hicho kinachojulikana kama Checkfor UTI Test kimekuwa nyenzo muhimu kwani maambukizi ya njia ya mkojo, yanayojulikana zaidi kama UTI, ni miongoni mwa changamoto za kiafya zinazowakumba watu wengi katika jamii. Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na daktari Dk Eshton Nkala wakati akizungumzia kipimo hicho kipya cha aina yake kuanza kutumika nchini. Alisema mara nyingi, maambukizi haya huanza kwa dalili ambazo zinaweza kuonekana kuwa ndogo, ikiwemo kukojoa mara kwa mara, maumivu au muwasho wakati wa kukojoa, maumivu ya chini ya tumbo, mkojo kubadilika rangi au kuwa na harufu isiyo ya kawaida. Alisema changamoto kubwa katika udhibiti wa UTI ni kuchelewa kutambua dalili na kuchelewa kufika katika vituo v...

NEW IPU SECRETARY GENERAL TAKES OFFICE AS EXECUTIVE COMMITTEE CONCLUDES 300TH SESSION

By Prosper Makene The IPU Executive Committee held its 300th session in Geneva, Switzerland, on 29-30 June 2026, under IPU President Dr. Tulia Ackson. The constitutional meeting coincided with International Day of Parliamentarism, observed annually on 30 June to mark the founding of the IPU. Delegates reviewed preparations for the 153rd IPU Assembly scheduled for October in Arusha, Tanzania. They also discussed the upcoming election of a new President to replace Dr. Ackson. The session featured the formal handover of the Secretary General’s office. Mr. Martin Chungong passed the “keys” of leadership to Ambassador Anda Filip, elected in April in Istanbul. Her four-year term began on 1 July 2026. Ambassador Filip is the 10th Secretary General, the first woman, and the first from Eastern Europe to lead the IPU Secretariat. The Parliament of Tanzania congratulated Ambassador Filip and pledged continued cooperation with the IPU.

BALOZI FILIP AANZA KAZI RASMI

 Na Prosper Makene Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya IPU wamehitimisha kikao chao cha 300 jijini Geneva, Uswizi, tarehe 29-30 Juni 2026, chini ya uongozi wa Dkt. Tulia Ackson, Rais wa IPU. Kikao hicho cha Kikatiba kimeambatana na Maadhimisho ya Siku ya Mabunge Duniani, tarehe 30 Juni, ambayo ndiyo tarehe ya kuanzishwa kwa IPU.  Katika ajenda, Kamati ilijadili maandalizi ya Mkutano Mkuu wa 153 wa IPU utakaofanyika Oktoba jijini Arusha, Tanzania, pamoja na uchaguzi wa Rais mpya atakayemrithi Dkt. Ackson. Vilevile, kikao kilishuhudia makabidhiano ya Ofisi ya Katibu Mkuu. Bw. Martin Chungong alimkabidhi Balozi Anda Filip “funguo” ya uongozi, kufuatia uchaguzi wake Aprili jijini Istanbul. Balozi Filip alichukua wadhifa rasmi tarehe 1 Julai 2026.  Yeye ni Katibu Mkuu wa 10, Mwanamke wa kwanza, na Mtu wa kwanza kutoka Ulaya Mashariki kuongoza Sekretarieti ya IPU kwa kipindi cha miaka minne. Bunge la Tanzania linampongeza Balozi Filip na linaahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano n...

WAZIRI MKUU AKAGUA DARAJA LA NYATHOROGO, AIPONGEZA TARURA KWA MRADI WA SHILINGI MILIONI 729.2

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba, amekagua Daraja la Mto Nyathorogo lililopo Kijiji cha Nyathorogo, Kata ya Nyathorogo, wilayani Rorya mkoani Mara, linalounganisha wilaya za Rorya na Tarime katika ziara yake ya kikazi mkoani humo leo Julai 2, 2026. Akipokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Meneja wa TARURA Wilaya ya Rorya, Mhandisi Elifadhili Moses, amesema ujenzi wa daraja hilo umegharimu shilingi milioni 729.2, ambapo ulianza Agosti 1, 2025 na kukamilika Februari 28, 2026. Mhandisi Moses ameeleza kuwa daraja hilo limejengwa kwa teknolojia ya mawe, hatua iliyosaidia kupunguza gharama za ujenzi kwa zaidi ya asilimia 50 ikilinganishwa na usanifu wa awali. Ameongeza kuwa Serikali tayari imetenga fedha katika mwaka wa 2026/2027 kwa ajili ya ujenzi wa kingo za kulinda daraja hilo dhidi ya mmomonyoko wa maji. Kwa upande wake, Mbunge wa Jimbo la Rorya, Jafari Chege, amesema kukamilika kwa daraja hilo kumemaliza changamoto ya muda mrefu ya wananchi...

PRESIDENT CHAPO ARRIVES FOR A THREE-DAY WORKING VISIT

The President of the Republic of Mozambique, H.E. Daniel Francisco Chapo, has arrived in the United Republic of Tanzania to commence a three-day working visit from 2 to 4 July 2026. Upon his arrival at Julius Nyerere International Airport in Dar es Salaam, H.E. President Chapo was received by the Minister for Foreign Affairs and East African Cooperation, H.E. Ambassador Dr. Mahmoud Thabit Kombo (MP), who was accompanied by other senior Government officials. During his visit, H.E. President Chapo will hold official talks with his host, the President of the United Republic of Tanzania, H.E. Dr. Samia Suluhu Hassan, at the State House in Dar es Salaam. He will also officiate the opening of the 50th Dar es Salaam International Trade Fair (DITF), pay a courtesy call to Mama Maria Nyerere, and lay the foundation stone for the construction of the Embassy of the Republic of Mozambique in Dar es Salaam. It is noteworthy that this marks H.E. President Chapo's third visit to Tanzania since as...

RAIS WA MSUMBIJI AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI YA SIKU TATU

 Rais wa Jamhuri ya Msumbiji Mheshimiwa  Daniel Francisco Chapo amewasili nchini  kuanza ziara ya kikazi ya siku tatu, kuanzia Julai 2 -4 , 2026. Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Mheshimiwa Rais Daniel Francisco Chapo alipokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Dkt. Mahmoud Thabit Kombo (Mb) ambaye aliambatana na viongozi wengine waandamizi wa Serikali. Akiwa nchini, Mheshimiwa Rais Chapo atafanya mazungumzo rasmi na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu, jijini Dar es Salaam. Aidha, Mheshimiwa Rais Chapo atafungua rasmi Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam; atamtembelea Mama Maria Nyerere kwa lengo la kumsalimia na ataweka jiwe la msingi la ujenzi wa Ubalozi wa Msumbiji jijini Dar es Salaam. Itakumbukwa kuwa,  ziara hii ni ya tatu kwa Mheshimiwa Chapo kufanyika hapa nchini tangu alipoingia madarakani...

TANZANIA KUWA MWENYEJI WA MKUTANO MZITO WA COP12, NCHI 10 KUKUTANA DAR ES SALAAM KUJADILI UCHUMI WA BULUU

 Na MASHAKA MHANDO, Tanga SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakuwa mwenyeji wa Mkutano wa 12 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Nairobi (COP12) utakaofanyika kuanzia Oktoba 6 hadi 9 mwaka huu, jijini Dar es Salaam. Akizungumza na vyombo mbalimbali vya habari leo jijini Tanga, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Reuben Kwagilwa, amesema mkutano huo ni jukwaa muhimu kwa ustawi wa mazingira na uchumi wa taifa. Naibu Waziri huyo alizitaja nchi zitakazoshiriki kwenye mkutano huo kuwa ni pamoja na wenyeji Tanzania, Kenya, Somalia, Afrika Kusini, Msumbiji, Ufaransa, Comoro, Ushelisheli (Seychelles), Mauritius na Madagascar.  Alifafanua kuwa Tanzania ni miongoni mwa nchi wanachama wa Mkataba wa Nairobi ambao unahusu uhifadhi, usimamizi na uendelezaji wa mazingira ya bahari kwenye maeneo ya Ukanda wa Magharibi mwa Bahari ya Hindi. Kwa mujibu wa Naibu Waziri Kwagilwa, mkataba huo ulisainiwa Juni 21, 1985, na unatekelezwa chini ya usimamizi...