…..Ni kwa kutumia kipimo cha Checkfor UTI Test Na Mwandishi Wetu Tanzania imeendelea kupiga hatua katika sekta ya afya ambapo kipimo kipya cha UTI kinachomwezesha mtu kujipima akiwa nyumbani na kugundua kuwa amepata maambukizi ya ugonjwa huo kimeanza kutumika hapa nchini. Kipimo hicho kinachojulikana kama Checkfor UTI Test kimekuwa nyenzo muhimu kwani maambukizi ya njia ya mkojo, yanayojulikana zaidi kama UTI, ni miongoni mwa changamoto za kiafya zinazowakumba watu wengi katika jamii. Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na daktari Dk Eshton Nkala wakati akizungumzia kipimo hicho kipya cha aina yake kuanza kutumika nchini. Alisema mara nyingi, maambukizi haya huanza kwa dalili ambazo zinaweza kuonekana kuwa ndogo, ikiwemo kukojoa mara kwa mara, maumivu au muwasho wakati wa kukojoa, maumivu ya chini ya tumbo, mkojo kubadilika rangi au kuwa na harufu isiyo ya kawaida. Alisema changamoto kubwa katika udhibiti wa UTI ni kuchelewa kutambua dalili na kuchelewa kufika katika vituo v...
Marato tv - Sauti ya Jamii