MJUMBE wa Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) kutoka Mkoa wa Dodoma, Asia Abdallah, amewataka wanachama wa Umoja wa Leo Yetu Kesho Yetu kudumisha mshikamano, uaminifu na ushirikiano, huku akisisitiza kuepuka majungu, ubinafsi na migawanyiko inayoweza kudhoofisha maendeleo ya umoja huo. Akizungumza katika uzinduzi wa umoja huo uliofanyika jijini Dodoma, Asia Abdallah, ambaye pia aliwahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, amesema mafanikio ya umoja huo yanategemea zaidi mshikamano wa wanachama na utayari wa kufanya kazi kwa pamoja bila kuingiza tofauti za kisiasa, kikabila au kidini. Amebainisha kuwa taasisi za kifedha na mabenki zina nafasi kubwa ya kusaidia vikundi vya kijamii na kiuchumi kukua, lakini akasema mafanikio hayo hayawezi kupatikana iwapo kutakuwa na migogoro ya ndani. “Tunayo kazi ya pamoja na taasisi za kifedha ili kuviinua vikundi hivi. Nasihi muwe kitu kimoja, epukeni majungu, ubinafsi na migawanyiko. Umoja wa kweli unaosimama bila maslahi bina...
Marato tv - Sauti ya Jamii