Na Angela Sebastian ;Bukoba Mgombea Ubunge wa jimbo la Bukoba mjini kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhandisi Johnston Mutasingwa amewashukuru wananchi wa jimbo hilo, kwa ushirikiano na mapokezi makubwa waliompatia tangu kuanza kwa kampeni za kunadi Ilani ya chama hicho na kuomba ridhaa. Adha amewashauri wajitokeze kwa wingi kesho kutekeleza haki yao ya kidemokrasia kwa kupiga kura na kuchagua viongozi wa CCM kuanzia ngazi ya Taifa hadi kata ili waweze kushirikiana kuwaletea maendeleo. Mutasingwa ameeleza hayo leo wakati akihitimisha kampeni zake katika viwanja vya Shule ya Msingi Kashai ndani ya Manispaa ya Bukoba ambapo amesema kesho ni siku muhimu kwa Taifa letu hivyo, akawaomba wananchi kumuamini na kumtuma kwa kumpigia kura za kutosha Rais Dk.Samia Suluhu Hassan,yeye kwa nafasi ya ubunge na madiwani kwasababu ndiyo chaguo sahii la kutatua kero zao. "Nawaomba mjitokezeni kwa wingi kesho mpige kura kwa amani, utulivu na mchague viongozi wa CCM tutumeni kwas...
Marato tv - Sauti ya Jamii