Dodoma | Januari 22, 2026 Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde, amesema Serikali haitasita kuwachukulia hatua kali Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa ambao ofisi zao zitabainika kuhusika au kusababisha migogoro katika shughuli za uchimbaji wa madini, akisisitiza ulazima wa kuzingatia kikamilifu Sheria na Kanuni za Madini katika utekelezaji wa majukumu yao. Mhe. Mavunde ametoa kauli hiyo leo jijini Dodoma wakati wa ufunguzi kikao cha Menejimenti cha Tume ya Madini kilichowakutanisha Wakurugenzi, Mameneja na Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa, kilicholenga kufanya tathmini ya utekelezaji wa majukumu ya Tume kwa kipindi cha robo ya pili ya mwaka, pamoja na kuweka mikakati ya kukabiliana na changamoto zinazojitokeza katika Sekta ya Madini. Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Naibu Waziri wa Madini, Mhe. Dkt. Steven Kiruswa; Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo; Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Dkt. Janet Lekashingo; Kamishna wa Tume ya Madini, Mhandisi Theonestina Mwasha, pamoja n...
Marato tv - Sauti ya Jamii