JWTZ na Jeshi la India kushirikiana na mataifa tisa ya Afrika kukabiliana na matishio bahari ya hindi
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mh dkt Stergomena Lawrence Tax amezindua zoezi la Pamoja la ulinzi wa Bahari maarufu kama ‘AIKEYME’ lenye lengo la kukabiliana na matishio mbalimbali ya uhalifu baharini katika ukanda wa Bahari ya hindi. Akizungumza wakati wa kuzindua zoezi hilo aprili 13 mwaka 2025 katika bandari ya Dar es saam, baada ya kupokea meli vita moja kutoka nchini India ambayo imekuja maalum kwa ajili ya zoezi hilo linalohusisha nchi nyingine tisa za afrika, Mh, Stergomena Tax,amesema kuwa kumekuwa na matishio mbalimbali ya kiusalama baharini kama vile usafirishaji haramu wa madawa za kulevya,ugaidi,usafirishaji haramu wa bianadamu na uvuvi haramu. Kwa sababu hiyo amesema kwa kushirikiana kwa Pamoja katika mazoezi hayo kutasaidia kuleta tija katika kushughulikia maswala hayo Pamoja na kuongeza ushirikiano na ujuzi katika ya nchi na nchi. Waziri huyo wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa,amesema kuwa uwepo wa mazoezi hayo ni moja ya matokeo ya jitiha...