Skip to main content

Posts

Showing posts from July 19, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

CP. KAVIRONDO ASHIRIKI MKUTANO WA 28 WA KAMATI YA MAWAZIRI WA SADC KUHUSU SIASA, ULINZI NA USALAMA

 Na. Ssgt. Mawazo Mtondo - DODOMA Kamishna wa Huduma za Urekebu wa Jeshi la Magereza, CP Amina Kavirondo, akimuwakilisha Mkuu wa Jeshi la Magereza, CGP Jeremiah Yoram Katungu, alishiriki katika ujumbe wa Tanzania uliohudhuria Mkutano wa 28 wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), uliohitimishwa Julai 18, 2026, mjini Salima, Malawi. Ushiriki wa Kamishna wa Huduma za Urekebu katika mkutano huo unaonesha mchango wa Jeshi la Magereza katika masuala ya usalama wa Taifa na ushirikiano wa kikanda, sambamba na dhamira ya Tanzania ya kuimarisha amani, ulinzi na usalama ndani ya nchi na katika ukanda wa SADC. Tanzania, ikiwa ni miongoni mwa nchi waasisi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), ilishiriki kikamilifu katika Mkutano huo ambao ulianza kwa vikao vya ngazi ya Makatibu Wakuu vilivyofanyika Julai 13 na 14, 2026, na kufuatiwa na vikao vya ngazi ya Mawaziri vilivyofanyika Julai 16 na 17, 2026. Katika ngazi ya...

PROFESA TIBAIJUKA AIPONGEZA ST ANNE MARIE KWA MIAKA 25 ILIYOSHEHENI MAFANIKIO

 Na Mwandishi Wetu Waziri wa zamani wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka amewataka wakaguzi wa shule kutenda haki kwa shule binafsi na kuziona kama mshirika wa maendeleo badala ya mshindani. Kadhalika, Profesa Tibaijuka ameipongeza shule ya St Anne Marie Academy kwa kuendelea kusomesha bure wanafunzi wanaofiwa na wazazi wao ikiwa shule pekee ya binafsi inayofanya hivyo kwa sasa nchini. Alitoa pongezi hizo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya miaka 25 ya kuanzishwa kwa shule hiyo Julai 18 mwaka 2001. Aliwataka wakaguzi wa elimu nchini kuacha kuziwekea vikwazo shule binafsi kwa kuziona kama washindani kwenye sekta ya elimu na badala yake wanatakiwa kuwaona kama washirika muhimu kwenye kutoa huduma hiyo. ”Unakuta wanawawekea wenye shule binafsi viwango vya kusadikika tofauti kabisa na shule za umma, sisemi kwama muwawekee viwango hafifu, hapana mimi nataka uwiano wa haki baina ya shule za umma na shule binafsi,” alisema Alisema sh...

DC ITUNDA AWATUNUKU VYETI WAHITIMU 70 KAPS MBEYA, AWAPA NENO ZITO KUJIAJIRI

 Na Mwandishi Wetu, Mbeya MKUU wa Wilaya ya Mbeya, Mhe. Solomon Itunda, amewatunuku vyeti wahitimu 70 wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii (KAPS) na kuwataka kutumia elimu waliyoipata kuwa chachu ya mabadiliko chanya na kutengeneza fursa za kujiajiri badala ya kusubiri ajira za kuajiriwa. Hafla hiyo ya mahafali imefanyika Julai 17, 2026, katika viwanja vya chuo hicho kilichopo mtaa wa Forest, Jijini Mbeya, ambapo wahitimu hao walihitimisha masomo yao na kutunukiwa Astashahada (Certificate) ya Maendeleo ya Jamii. Akizungumza wakati wa hafla hiyo akiwa kama Mgeni Rasmi, Mhe. Itunda aliwapongeza wahitimu hao kwa juhudi, nidhamu na uvumilivu waliouonesha katika kipindi chote cha masomo yao, na kuwakumbusha kuwa maendeleo ya Taifa yanategemea nguvu kazi yenye maarifa na uzalendo. "Mnapaswa kwenda kuwa chachu ya maendeleo katika maeneo yenu kwa kuzingatia misingi ya kazi na utu. Tumieni elimu mliyoipata hapa kujiajiri na kuajiri wengine, huku mkizingatia maadili ya kazi, uzalendo na uwajibika...