Skip to main content

Posts

Showing posts from July 20, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Katibu Tawala Mkoa wa Kagera Awaagiza Wakurugenzi Kuandaa Maadhimisho ya Juma la Elimu

Na.Angela Sebastian  KATIBU tawala wa mkoa wa Kagera  Steven Ndaki  amewaagiza wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya mkoani humo kuhakikisha wanaanda maadhimisho ya juma la elimu maalum katika Maeneo yao ili kuwezesha wananchi kupata uelewa kwa yanayofanywa na idara hiyo. Hayo yamebainishwa katika taarifa iliyosomwa na katibu tawala msaidi idara ya uchumi na biasharea Isaya Tendega  kwa niaba ya katibu tawala,wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili kwa maafisa elimu wa elimu maalum na wakuu wa shule zinazotoa elimu maalum mkoani humo yalifofanyika jana katika shule ya sekondari Omumwani . Amesema kuwa licha ya kwamba  mkoa utafanya maadhimisho ya juma hilo lakini pia kila Halmashauri lazima inatakiwa kufanya madhimisho katika maeneo yake lengo likiwa ni kuwezesha wananchi waudhulie na kupata elimu ya kutosha juu ya idara ya elimu maalum na watu wazima sambamba na majukumu yake na faida zake. “Tunatakiwa kuendelea kuadhimisha juma la elimu ya watu wazima kwa k...

Majaliwa: Wapiga Kura Wapya Zaidi ya Milioni 5 Kuandikishwa

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa kwa mujibu wa takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 jumla ya wapiga kura wapya 5,586,433 wataandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura. Amesema kuwa wapiga kura hao ni ambao watakuwa wametimiza umri wa miaka 18 katika kipindi cha kuanzia mwaka 2020 baada ya uchaguzi mkuu uliopita na ambao watatimiza umri huo ifikapo tarehe ya uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025. Amesema hayo leo (Jumamosi, Julai 20, 2024) alipozindua uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura, katika uwanja wa Kawawa, mkoani Kigoma. Uzinduzi huo unaashiria kuanza kwa uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura nchi nzima ambapo Mikoa inayoanza uboreshaji wa daftari hilo leo Julai 20, 2024 hadi  Julai 26, 2024 ni Kigoma, Katavi na Tabora kisha mikoa mingine kufuata. Ameongeza kuwa kwa mujibu wa taarifa za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, inakadiriwa kuwa wapiga kura 4,369,531 wataboresha taarifa zao. “Idadi hii si ndogo kwenye zoezi la uboreshaji wa daftari ...