Na Angela Sebastian; Bukoba Mwenge wa Uhuru Kuzindua na Kukagua Miradi 54 ya Sh. Bilioni 23 Kagera Mwenge wa Uhuru mwaka huu unatarajiwa kuzindua, kufungua, kukagua na kuweka mawe ya msingi katika miradi 54 ya maendeleo yenye thamani ya Sh. bilioni 23 mkoani Kagera. Akizungumza na waandishi wa habari leo, Agosti 26, 2026, Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali Yahya Kido, amesema Mwenge huo utapokelewa wilayani Muleba ukitokea mkoani Geita tarehe Agosti 30, 2026, kabla ya kuanza kukimbizwa katika halmashauri nane za mkoa huo. Kwa mujibu wa Kanali Kido, Mwenge wa Uhuru utatembea umbali wa takribani kilomita 1,230 ndani ya Kagera, huku ukiifikia miradi 54 katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo,katika miradi hiyo, 25 itawekewa mawe ya msingi, mitano itafunguliwa, 11 itazinduliwa na 13 itakaguliwa ili kujiridhisha na utekelezaji wake pamoja na manufaa yake kwa wananchi. Miradi hiyo inahusisha sekta muhimu za maendeleo, ikiwemo maji, ...
Marato tv - Sauti ya Jamii