▪️Jiji kujenga sakafu kupunguza nguvu ▪️Mbunge Mavunde awachangia 10m kutunisha mfuko wa Soko ▪️Awataka Mgambo wa Jiji kuacha kutumia mabavu ▪️Aahidi kuwaunganisha na Taasisi za fedha kwa ajili ya mitaji ▪️DC Shekimweri aahidi kusimamia utatuzi wa kero sokoni 𝐃𝐨𝐝𝐨𝐦𝐚 Wafanyabiashara wadogo wa Soko la Machinga Complex Jijini Dodoma wameishukuru serikali ya awamu ya sita chini ya Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa namna ilivyowahamisha kutoka barabarani na kuwajengea soko maalum maarufu kama Machinga Complex. Akizungumza katika mkutano mkuu wa soko Kaimu Mwenyekiti wa Machinga Complex Ndg. Lucas Kingamkono ameishukuru serikali kwa uwepo wa soko la Machinga ambalo limerahisisha ufanyaji wa biashara kwa wafanyabiashara hao wadogo ambao awali walikuwa maeneo ambayo hayakuwa rasmi na hivyo kufanya biashara kwa mashaka. Akizungumza katika mkutano huo,Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini *lMh. Anthony Mavunde ameupongeza uongozi wa soko Kwa kuandaa mkutano wa kusikiliza kero za wafanyabiash...
Marato tv - Sauti ya Jamii