Skip to main content

Posts

Showing posts from November 5, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Uwekezaji mkubwa sekta ya madini mapato yaongezeka

• Ajira zamwagwa kwa Watanzania • Minada ya Madini kurejeshwa • Mauzo yapaa Na Vicky Kimaro,  Tume ya Madini. “Serikali imefanya uwekezaji mkubwa katika Sekta ya Madini, tumenunua mitambo mikubwa, mitano imeshafika nchini, kumi ipo njiani inakuja, mitambo hii itawarahisishia wachimbaji wadogo kupata taarifa  za uchimbaji na kuwaepusha na hasara,” kauli ya  Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, aliyoitoa Oktoba 21, 2024 ambapo aliongeza, “Mitambo hii ikifika itagawanywa pote, ila nimemtaka Waziri  (Mheshimiwa Anthony Mavunde)  atenge mitambo miwili kwa ajili  ya vijana na mmoja kwa ajili ya wanawake. Kauli hiyo ya Rais Samia ni muendelezo wa dhamira yake ya dhati ya kuhakikisha Sekta ya Madini inaendelea kuongeza mchango wake katika ukuaji wa uchumi wa nchi.  Mpango wa Serikali ni kuhakikisha kuwa sekta hii inachangia asilimia 10 au zaidi katika Pato la Taifa ifikapo 2025.  Ukuaji wa Sekta ya Madini umeongezeka kutoka asilimia 9.4 Mwaka 2021 hadi ku...

Zaidi ya billioni 11 kusambaza umeme kwenye vitongoji 90 vya mkoa shinyanga

*📌Kunufaisha Kaya 2,970 katika Vitongoji 90 ndani ya Wilaya Tatu* *📌RC Macha asema Umeme ni kipaumbele cha Rais Samia* Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa Shilingi Bilioni 11.18 wa kusambaza umeme katika vitongoji 90 utakaonufaisha Kaya 2,970 Mkoani Shinyanga. Msimamizi wa Miradi ya REA Kanda ya Magharibi, Mhandisi Robert Dulle amebainisha hayo Novemba 05, 2024 Mkoani Shinyanga mbele ya Mkuu wa Mkoa huo, Mhe. Anamringi Macha wakati wa kumtambulisha Mkandarasi aliyeshinda zabuni ya kutekeleza mradi huo Kampuni ya wazawa ya Derm Group (T) Limited ya Jijini Dar es Salaam. “Tunamshukuru Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kiasi cha shilingi 11,184,759,397.2 kitumike kusambaza umeme katika vitongoji 90 Mkoani hapa, leo hii tumefika hapa kumtambulisha Mkandarasi na tayari maandalizi ya awali ya kutekeleza mradi yameanza,” alisema Mhandisi Dulle. Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Anamringi Macha aliipongeza REA kwa kutekeleza majukumu y...