Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Kazi Maalum), Prof. Palamagamba Kabudi, amewahimiza Watanzania wanaoishi nje ya nchi (Diaspora) kuendelea kuwekeza nchini na kushiriki kikamilifu katika juhudi za maendeleo ya taifa. Amesema Watanzania walioko ughaibuni wana nafasi kubwa ya kuchangia ukuaji wa uchumi wa nchi kupitia mitaji, utaalamu na uzoefu walioupata nje ya nchi. Prof. Kabudi ameyasema hayo wakati wa mkutano na Watanzania wanaoishi jijini London, Uingereza, ambapo aliwasilisha salamu za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na ujumbe wa serikali kwa Watanzania waishio ughaibuni. Amesema serikali inaendelea na juhudi za kurekebisha, kujenga upya na kufanya maboresho katika sekta mbalimbali. Aidha, Profesa Kabudi amewataka Watanzania wanaoishi nje ya nchi kununua hisa katika miradi ya maendeleo inayotekelezwa nchini, kushiriki katika uwekezaji wa pamoja na kutumia utaalamu wao kwa kushirikiana na wataalamu waliopo Tanzania kusaidia maendeleo ya sekta m...
Marato tv - Sauti ya Jamii