Waziri Gwajima apongeza Mchango wa Shirika la Kivulini katika Mapambano dhidi ya Ukatili wa Kijinsia
Serikali imepongeza Mchango wa shirika la kutetea haki za wanawake na watoto la Kivulini katika kuinua uchumi wa kaya na kupunguza vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto,mimba pamoja na ndoa za utotoni. Pongezi hizo zimetolewa na Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Dkt.Dororthy Gwajima wakati wa ziara yake katika ofisi za shirika hilo zilizoko nyamhongolo Jijini Mwanza. Akizungumza na Menejimenti na wafanyakazi wa shirika la Kivulini,Dkt.Gwajima ameahidi kuwa serikali itaendelea kuunga mkono shirika hilo ikiwemo kuhakikisha linapata ufadhili zaidi ili kuongeza ufanisi kwenye shughuli za kupambana na ukatili wa kijinsia pamoja na kuinua uchumi wa kaya. ‘’Kivulini wanafanya kazi kubwa ambayo haijasimuliwa vizuri make sio watu wa kupiga kelele,Niseme natambua kwa ukubwa kazi mnayofanya,ushirikiano wenu,Tuna Jukumu moja tu la Kuisemea Kivulini ili isikike na iendelee kupata ufadhili kwa sababu kazi zake ziko kwenye Jamii huko na ni kati ya mashirik...