MASABALA MZEE MASHUHURI KAGERA ATUNUKIWA TUZO BAADA YA KUTOA ARDHI KWA AJILI YA BWENI LA WANAFUNZI-KIBETA
Na Angela Sebastian Mzee mashuhuri wa Mkoa wa Kagera, Joseph Masabala, amepewa hati ya shukrani na tuzo maalum baada ya kutoa sehemu ya ardhi yake kwa ajili ya ujenzi wa Bweni la wanafunzi katika Shule ya Sekondari Kibeta, Manispaa ya Bukoba, hatua inayotajwa kuwa mchango mkubwa katika kuboresha mazingira ya elimu kwa wanafunzi wa eneo hilo. Tuzo hiyo imetolewa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Michael Mwang’onda, wakati Mwenge wa Uhuru ulipotembelea na kuzindua miradi ya maendeleo katika Manispaa ya Bukoba. Mzee Masabala pamoja na mkewe, Lushaka Masabala, walipokea hati hiyo ya shukrani na tuzo kwa niaba ya familia yao. Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mwang’onda ameipongeza familia ya Mzee Masabala kwa uamuzi wao wa pamoja wa kutoa ardhi hiyo kwa ajili ya maendeleo ya elimu, akieleza kuwa hatua hiyo ni mfano wa uzalendo na kujitolea kwa jamii. Amesema ardhi hiyo haitakuwa tu sehemu ya ujenzi wa mabweni, bali itakuwa mkombozi wa elimu kwa kizazi cha sasa...