Skip to main content

Posts

Showing posts from March 30, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Hakuna Taifa Lisilokopa Duniani, Uchumi wa Dunia Umejengeka Kwa Mikopo. Kukopesheka ni Ishara ya Uchumi Imara

 _Deni la Tanzania ni himilivu na lina afya kiuchumi ukilinganisha na Mataifa mengi ya Afrika na ulimwenguni._  Na Bwanku M Bwanku. Kwa siku za hivi karibuni kwenye Taifa letu kumezuka mjadala kuhusu nchi kukopa ama kutokukopa. Je kuna haja ya kukopa au kutokukopa au lipi ni lipi? Kama mwananchi nami ningependa kutoa mchango wangu kwa faida ya wote kuhusu huu mjadala. Je ni muhimu kukopa? Hatuwezi kuleta maendeleo yetu wenyewe bila kukopa? Na maeneo mengine kama hayo yanayozunguka kwenye mjadala huu.  Kwa Mujibu wa Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) iliyosomwa Wiki iliyopita Alhamisi Machi 27, 2025 Deni la Taifa hadi kufikia muda huu ni Trilioni 97. Deni hili linahusisha mikopo kutoka kwenye Taasisi mbalimbali za ndani na nje ya nchi n.k ambazo fedha zote hizo zikikopwa zinaelekezwa kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo ndani ya Taifa.  Kwanza, ni muhumu ikafahamika kwamba hakuna nchi yoyote duniani inayofanya shughuli za kiuchumi kuteke...

Waislamu Mkoa Wa Tanga Watakiwa Kufanya Yaliyomema Wakati Wote

 Na MASHAKA MHANDO, Tanga  WAISLAMU nchini wametakiwa kuendeleza matendo mema ya mwezi mtukufu wa Ramadhani kwa kuyaishi hata baada mfungo huo kumalizika. Akizungumza katika Swala ya Eid el Fitr katika msikiti wa Chumbageni Jijini Tanga, Sheikh Mussa Zubeir alisema Watanzania hasa wa dini ya Kiislamu waendelee kufanya mema hata baada ya kumaliza kwa Ramadhani. Alisema waumini wa dini hiyo kama waliweza kujizuia na mambo yasiyo mpendeza mungu katika kipindi chote Cha mfungo huo hawana budi kuendeleza matendo hayo hata baada ya mfungo kwisha. Naye Sheikh Aziz Yunus wa msikiti wa Majengo mjini Muheza maarufu msikiti wa Mwalimu Ali, alisema kuwa Watanzania waendelee kulinda amani kama ambavyo wamemaliza funga zao kwa amani. Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Hamisi Mwinjuma maarufu MwanaFA, alipopewa nafasi ya kuzungumza katika msikiti huo aliwataka Watanzania kuendeleza Umoja na mshikamano na kuyaishi yale mema walivyokuwa wakiyafanya wakati wa Ramadhani. Alisema W...

Mbunge Mwanyika Atoa Mahitaji ya Sikukuu ya Eid

Machi 30, 2025 Mbunge wa Njombe mjini mhe. DEO MWANYIKA (MB) ametoa mahitaji ya sikukuu ya Idd El Fitri inayotarajiwa kufanyika Machi 31, 2025 kwa wazee na wahitaji katika misikiti yote ya Njombe mjini. Akiongea wakati wa kukabidhi mahitaji hayo Mhe Mwanyika amewapongeza waislamu wote kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani ambao unakwenda kuhitimishwa kwa sikukuu ya Eid Machi 31,  2025. Naye Sheikh wa Mkoa wa Njombe amemshukuru Mhe. Mbunge kwa majitoleo yake kwa waislamu wakati wa mfungo wa mwezi  mtukufu wa Ramadhani, kwani amekuwa akichangia mahitaji ya mfungo kila mwaka. Waislamu wanamtakia heri na baraka katika majukumu yake aliyokabidhiwa ya kuwatumikia wananjombe na watanzania kwa ujumla.

Rais Samia Ashiriki Katika Swala ya Eid Jijini Dar es Salaam

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan  akijumika na waisalamu wengine  kusali swala ya Eid katika kukamilisha ibada ya Mfungo wa Ramadhan katika Msikiti wa Mohamed VI uliopo katika Makao Makuu ya Baraza Kuu la Waislamu Tanzania  (BAKWATA) Kinondoni Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuswali Swala ya Eid El Fitr tarehe 31 Machi, 2025.

Wasira Awasambaratisha Zitto Kabwe na Chadema huku Akishangiliwa

Na Mwandishi Wetu MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, Stephen Wasira amemjibu Kiongozi Mstaafu wa ACT-Wazalendo Zitto Kabwe kuwa CCM haibishani na CHADEMA kwa kuwa iliwaambia wazungumze wakajibu hawako tayari kupotezewa muda. Pia, Wasira ametumia nafasi hiyo kuwaambia CHADEMA wajitokeze hadharani wawaambie wanataka nini na kama wanashindwa kuiambia CCM basi waiambie Tume. Akizungumza Leo machi 30 2025 katika mkutano wa hadhara mbele ya maelfu ya wananchi wa Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu, Wasira alitumia nafasi hiyo kumjibu Zitto Kabwe ambaye akiwa Lindi alisema Wasira anajua historia hivyo kwa nini anabishana na CHADEMA badala ya kuzungumza. “Mimi niliwaambia tuzungumze Tundu Lissu akasema tutawapotezea muda, sasa mtu ana muda wake na hataki upotee wewe umlazimishe kupoteza muda wake wa nini? Kwa hiyo sisi tunawaambia wakiwa na jambo linazungumzika na linawezekana waje tuzungumze. “Hawataki kuzungumza sasa wanasema hayo mabadiliko wanayoyataka wao ambayo mimi siyajui...

Nimeridhishwa na Maandalizi Kuelekea Kuwashwa Kwa Mwenge Wa Uhuru - Majaliwa

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema ameridhishwa na hatua za maandalizi kuelekea  sherehe za kuwashwa kwa Mwenge wa Uhuru ambao utazunguka katika Mikoa 31 na Halmashauri 195 nchini. Amesema hayo leo Jumapili (Machi 30, 2025) baada ya kukagua maandalizi hayo katika uwanja wa uwanja wa Shirika la Elimu Kibaha Mkoani Pwani. Mgeni rasmi katika sherehe hizo zitakazofanyika Aprili 02, 2025 atakuwa ni Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango Akizungumza baada ya kukagua maandalizi hayo Mheshimiwa Majaliwa ametoa wito kwa waratibu wote wa Sherehe hizo kuhakikisha wanakamilisha haraka maeneo machache yaliyobaki. "Nimeridhishwa na maandalizi yaliyofanyika, mmefanya kazi kubwa hadi kufikia hatua hii, tuhakikishe sehemu ndogo zilizobaki tunazikamilisha kwa wakati." Naye Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Ridhiwani Kikwete amesema maandalizi hayo yamefikia asilimia 96 na maeneo machache yaliyobaki yatakamilishwa ndani ya muda mfupi. Awali, akitoa salamu ...

Balozi Mwapachu azikwa Kijiji kwake Tanga

📍Serikali yasema itaenzi kazi zake NAIBU Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Hamisi Mwinjuma maarufu MwanaFA, ameshiriki mazishi ya aliyekuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) Balozi Juma Mwapachu aliyezikwa leo Machi 30 Kijijini kwao Pande Jijini Tanga. Katika mazishi hayo yaliyoongozwa na Jaji Mstafu wa Mahakama Kuu Jaji Osman Chande, MwanaFA alisema kuwa serikali imempoteza mtumishi bora hivyo itahuisha yale yote mema aliyoyaacha wakati wa utumishi wake. Alisema marehemu wakati wa uhai wake alikuwa mchapakazi aliyefanya kazi kwa maslahi Mapana ya nchi yake, uzalendo lakini pia alikuwa mwaminifu aliyeongoza wenzake vizuri. "Kiukweli tumepoteza mtu muhimu, mtu makini mchapa kazi aliyejali nchi yake na aliyeongoza wenzake katika njia sahihi, alisema. MwanaFA ambaye ni mbunge wa Muheza alisema kwa niaba ya serikali wataenzi yote aliyoasisi marehemu katika ngazi mbalimbali za utumishi alizopitia ikiwemo nafasi aliyostafu nayo ya Katibu Mkuu wa EAC. Jajj Mst...

Kambarage Wasira Aongoza Harambee ya Kanisa Bunda Na Kuchangisha Milioni 10

Na Shomari Binda-Bunda MKURUGENZI wa kampuni ya Audacia Investment Ltd na mdau wa Maendeleo wilaya ya Bunda mkoani Mara Bw Kambarage Wassira amefanikisha kupatikana kwa shilingi milioni kumi za kusaidia Maendeleo ya kanisa la Waadventista Wasabato Nyasura juu mjini Bunda. Bw Kambarage Wasira ambaye pia ni kada wa CCM aliwakilishwa katika harambee hiyo kama mgeni rasmi  na Safari Lubulila ambapo alichangia shilingi milioni moja Taslimu. Akizungumza kwenye harambee hiyo Kambarage amesema viongozi wa dini kupitia nyumba za ibada wanasaidia kujenga maadili kwenye jamii hivyo ni muhimu kujenga na kuziimarisha. Amesema ili taifa liweze kusonga mbele kwenye maendeleo jamii wakiwemo vijana wanapaswa kuwa na maadili mema na viongozi wa dini wamekuwa msaada kwa serikali eneo hilo. Kambarage ambaye amekuwa mstari wa mbele kuchangia masuala ya jamij mara kwa mara kwenye kwenye matukio tofauti ametoa wito kwa kila mmoja kuchangia kwenye mambo ya dini. " Niko hapa kumuwakilisha  ndugu yetu ...