Skip to main content

Posts

Showing posts from March 25, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mradi wa Sequip Waendelea Kuboresha Elimu ya Sekondari Mtwara

Na OWM - TAMISEMI,Mtwara Mkoa wa Mtwara umeendelea kupiga hatua katika kuboresha Sekta ya Elimu kufuatia utekelezaji wa Mradi wa Kuimarisha Elimu ya Sekondari (SEQUIP), unaosimamiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, huku ukifadhiliwa na Benki ya Dunia. Akizungumza wakati wa ziara ya ufuatiliaji wa pamoja wa utekelezaji wa mradi huo, Mratibu wa Mradi wa SEQUIP kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Bw. Richard Makota, alisema shule za Mkoa wa Mtwara zimeonyesha mafanikio makubwa katika utekelezaji wa mradi. “Matokeo yanaonekana wazi, hasa katika ongezeko la ufaulu wa wanafunzi kwenye masomo ya sayansi na hisabati, pamoja na matumizi ya teknolojia ya kisasa katika ufundishaji,” alisema Bw. Makota. Alisema kupitia SEQUIP, maboresho makubwa yamefanyika ikiwemo ujenzi wa miundombinu mipya ya shule, upatikanaji wa vifaa vya kisasa vya TEHAMA kama mbao janja (smart boards) na kompyuta, pamoja na utoaji wa vifaa vya maabara na kemikal...

Kifo cha Lukuvi Chaahirisha Harambee Kubwa na Ufunguzi wa Kanisa Serengeti

 Taasisi ya Nyansaho foundation imehairisha hafla ya harambee ya kuchangia ujenzi wa shule mpya ya msingi na Zahanati katika kijiji cha Musati, ambayo ilitarajiwa kuongozwa na Jaji mkuu wa Tanzania mh George Masaju.  Hafla hiyo ambayo pia ingehudhuriwa na Waziri wa ujenzi mh Abdallah Ulega pamoja na mwenyekiti wa taasisi ya Nyansaho foundation mh Rhimo Nyansaho ilipangwa kufanyika machi 28 mwaka huu 2026 katika kijiji cha Musati Wilayani Serengeti mkoani Mara, sambamba na ufunguzi wa kanisa la Waadventista Wasabato Wasaba Musati Central katika eneo hilo.  Taarifa iliyotolewa na taasisi ya Nyansaho imesema kuahirishwa kwa Shughuli hizo kunatokana kifo cha aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Watu Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani, Marehemu William Vangimembe Lukuvi (Mb)  Taasisi ya Nyansaho foundation imesema itatangaza tarehe rasmi kwa AJILI ya kufanya zoezi hilo huku ikitoa pole kwa ndugu, Familia, Serikali na Watanzania...

AU Yamteua Jakaya Kikwete kuwa Mwakilishi wake Pembe ya Afrika

Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika, Mahmoud Ali Youssouf, ametangaza uteuzi wa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa zamani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuwa Mwakilishi Mkuu wa Pembe ya Afrika na Bahari ya Shamu. Katika jukumu lake Rais Kikwete ataunga mkono juhudi za Umoja wa Afrika kushughulikia mienendo tata ya kisiasa, amani na usalama katika kanda nzima. Mamlaka yake yatajumuisha kuendeleza diplomasia, kuwezesha mazungumzo ya kisiasa jumuishi, kukuza kujenga imani miongoni mwa wadau, na kuimarisha mifumo ya ushirikiano wa kikanda inayolenga kustawisha amani na utulivu endelevu. Aidha, Kikwete katika wadhifa wake atafanya kazi kwa uratibu wa karibu na washirika husika wa kikanda na kimataifa, ikiwa ni pamoja na Mamlaka ya Kiserikali ya Maendeleo (IGAD), Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Umoja wa Mataifa ya Kiarabu, Umoja wa Mataifa, na washirika wengine, kwa nia ya kuhakikisha uwiano, ulinganifu na ufanisi katika juhudi za pamoja za kukuza amani, utulivu na usalama. Kiongozi hu...

Mkalipa Azidi Kuimarisha Uhai wa Ccm Pangani

Na: Mwandishi Wetu, Pangani  Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilaya ya Pangani, Nasri Mkalipa, ameendelea na ziara ya Operesheni Samia ikiwa ni mwendelezo wa Jumuiya anayoingoza kuhakikisha uhai wa Chama unaendelea kuimarika zaidi katika Kata zote 14 za wilaya ya Pangani. Machi 25, 2026, Mkalipa amefanya ziara katika Kata za Kipumbwi na Mikinguni ambapo amekutana na wanachama wa CCM na wananchi hasa vijana ambao amewahimiza kuendelea kukitumikia Chama kwani Chama kipo pamoja nao bega kwa bega kuhakikisha changamoto zao zinapatiwa ufumbuzi. "Serikali ya Rais Dk. Samia Suluhu Hassan ipo kazini kuhakikisha changamoto za vijana zinapatiwa ufumbuzi, anatoa fedha nyingi kwa ajili ya vijana, ni wajibu wenu kama vijana kujiunga katika vikundi ili muweze kunufaika na fursa mbalimbali zinazotolewa na serikali," amesema Mkalipa. Aidha, Mkalipa amewahimiza vijana kudumisha amani na mshikamano kwani ndiyo nyenzo ya mafanikio. Kwa upande wa vijana, wameishukuru ser...

Tanzania na Benki ya Afdb Zadhamiria Kuimarisha Ushirikiano Katika Miradi ya Kimkakati

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb), amesema Ushirikiano kati ya Tanzania na Benki ya maendeleo ya Afrika  (AfDB), katika miradi ya kimkakati  unaendelea kuimarika jambo linawezesha nchi kukua kiuchumi. Ameyasema hayo Machi 25, 2026 alipokuwa anapokea nakala za hati za utambulisho za Mwakilishi Mkazi  mpya wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) nchini Tanzania Bi. Mary Manneko Monyau, katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam. Mhe. Kombo amesema miradi hiyo imejikita zaidi katika sekta za miundombinu, usafirishaji, na nishati ambazo ni uti wa mgongo wa mabadiliko ya kiuchumi nchini. Ameongeza kuwa kwa sasa Benki hiyo inafadhili miradi 27 ikiwemo  Barabara ya Mzunguko wa Nje ya Dodoma, Ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Msalato, Mradi wa Reli ya Kisasa (SGR)  na Mradi wa nyaya za umeme za chini ya bahari unaounganisha visiwa vya Zanzibar, Pemba, na Mafia. Aidha amempongeza  Bi. Monya...

Baadhi ya Mawaziri na Wabunge Wakiwa Nyumbani Kwa Marehemu William Lukuvi

 Baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wakiwa msibani nyumbani kwa aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Watu Wenye Ulemavu) na Mbunge wa Jimbo la Isimani, Marehemu William Vangimembe Lukuvi (Mb) Area D jijini Dodoma. Mhe. Lukuvi amefariki asubuhi ya leo tarehe 25 Machi, 2026 katika Hospitali ya Benjamini Mkapa alipokuwa akipatiwa matibabu.