_• Waanza ujenzi wa Zahanati kuondoa kero kwa wananchi_ _• Wasaidia upatikanaji wa urahisi wa kokoto katika marekebisho ya ujenzi wa barabara ya Iringa, Dodoma_ MGODI wa Mawe wa Ndolela Quarry uliopo kijiji cha Ndolela jimbo la Isimani mkoani Iringa umeanza ujenzi wa Zahanati kwa kushirikiana na wananchi ambayo itaondoa adha ya wananchi hao kutembea umbali mrefu kufuata huduma za afya. Akizungumza katika mahojiano maalum, Mwenyekiti Mtendaji wa Kijiji cha Ndolela, Majuto Dumicus amesema Zahanati hiyo ikikamilika itaweza kuhudumia Kaya 377 zilizopo katika eneo hilo. Amesema, ujenzi wa Zahanati hiyo ni kutimiza takwa la kisheria na Kanuni za Wajibu wa Wamiliki wa Leseni za Madini Kwa Jamii. Kwa upande wa Meneja Msaidizi wa Mgodi wa Mawe wa Ndolela (Ndolela Quarry) Hilter Ranjiti amesema tangu kuanzishwa kwa mgodi huo mwaka 2022 umekuwa na manufaa kwa wananchi kwa kutoa ajira pia kutekeleza takwa la kisheria kwa kuchangi...