Skip to main content

Posts

Showing posts from December 13, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Kurudi Kwa Minada ya Madini Mirerani Kutasaidia Kuongeza Thamani ya Madini-Wadau wa Madini

🔹️ *_Biashara kufanyika kidijitali kupitia Soko la Bidhaa Tanzania-TMX_* 🔹️ *_Waziri Mavunde kuwa Mgeni Rasmi Hafla ya Mnada_* 🔹️ *Wanawake wahamasishwa kuchangamkia fursa za biashara katika mnyororo wa madini_* 📍 *Mirerani- Manyara* Wafanyabiashara wa Madini nchini Tanzania wameelezea matumaini yao makubwa kuhusu hatua ya kurejeshwa kwa Minada ya Madini katika eneo Mirerani, Mkoa wa Manyara na kueleza kuwa kurejea kwa minada hiyo kutasaidia kuleta mchango mkubwa katika kuongeza thamani ya madini, hususan Tanzanite, ambayo ni madini adimu yanayopatikana nchini Tanzania pekee. Hayo yameelezwa kwa nyakati tofauti na baadhi ya wafanyabiashara wakati wakizungumza na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Madini leo Desemba 13, 2024 kuelekea Siku ya Mnada wa Madini ya Vito Mirerani 2024 inayotarajiwa kufanyika Desemba 14, 2024. Wafanyabiashara hao wameitaka Serikali kuendelea kushirikiana na wadau ili kuhakikisha kuwa minada inafanyika mara kwa mara, kwa uwazi, na kwa misingi ya h...

Matukio ya picha za usiku wa waandishi wa habari na wadau Mwanza

 

Profesa Kahyarara afungua Kongamano la Wahitimu NIT

Na Mwandishi Wetu, Dar Katibu Mkuu wa wizara ya Uchukuzi Prof Godius Kahyarara amesema serikali inampango wa kutambua bunifu mbali mbali zinazofanywa na wanafunzi wa vyuo vikuu kikiwemo Chuo cha Taifa Cha Usafirishaaji na kuangalia namna ya kuzitumia kwa manufaa ya Taifa. Ameyasema hayo leo jijini dar es salaam katika kongamano la 11 la wahitimu wa chuo cha Taifa cha usafarishaji NIT sambamba na kutoa zawadi kwa wahitimu waliofanya vizuri katika matokeo yao. "Katika sekta ya usafirishaji tumeona ubunifu wa vifaa unaofanywa na wanafunzi na tumeviangalia kwa kuona namna gani vinaweza kusaidia katika sekta ya usafirishaji" amesema kahyarara Ameongeza kuwa serikali imejipanga vizuri katika sekta ya usafirishaji na vitu vingi vimeongezeka ukiachana na mwanzo ilivyokuwa. "Niwasahi vijana wanaomaliza vyuo vikuu kujipangana na kutambua kuwa kuna mda wakukomaa kabla ya kuingia kwenye soko la ajira na wasikate tamaa kwamba leo umemaliza shule na kesho ukupata ajira, kuna muda wa k...

Tamasha la Bibi Titi Linafanya Kazi Nzuri ya Kuenzi Kazi za Serikali-Mhe. Mongella

Na John Jayros Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Mhe. John Mongella amesema Tamasha la Bibi Titi  Mohamed siyo tu  Tamasha  linalotumika kumuenzi hayati  bibi Titi  bali ni Tamasha linalotumika kuenzi kazi kubwa inayofanywa na Serikali ya CCM inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan. Mhe. Mongella  ameyasema haya leo Desemba 13, 2024 wakati akifungua rasmi  tamasha la mwaka huu la Bibi Titi IKwiriri Wilayani Rufiji  huku akimpongeza Mbunge wa Jimbo hilo Mhe. Mohamed Mchengerwa  kwa kazi  kubwa na nzuri anayoifanya  ya kuwaletea  maendeleo  wananchi wa jimbo  hilo. “Ndugu wananchi wa jimbo la Rufiji, Sisi kama Chama  tunaliona jimbo hili ni miongoni mwa  majimbo salama  ambayo  yamefanya kazi nzuri kwa wananchi wake, hivyo mtambue  kuwa  mna  mbunge  bora”.Amefafanua  Mhe  Mongella Ametoa  rai kwa  viongozi  wa CCM ko...