Skip to main content

Posts

Showing posts from December 4, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Tawa Yakabidhi Bweni la Wasichana Shule ya Sekondari Mchengerwa, Rufiji

📍 Mradi wagharimu zaidi ya TZS Milioni 252 Na Beatus Maganja, Rufiji, Pwani.  Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) imekabidhi rasmi bweni jipya la wasichana katika Shule ya Sekondari Mchengerwa iliyopo Kata ya Ngarambe wilayani Rufiji mkoani Pwani ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuboresha mazingira ya elimu, hasa kwa mtoto wa kike. Bweni hilo ambalo ujenzi wake umegharimu zaidi ya shilingi milioni 252, limejengwa kwa ushirikiano kati ya TAWA na Shirika la Uhifadhi wa Wanyamapori  (Frankfurt Zoological Society – FZS) chini ya ufadhili wa Serikali ya Ujerumani kupitia Benki ya Maendeleo ya watu wa Ujerumani (KfW), limekabidhiwa likiwa na jumla ya vitanda 40 aina ya "double decker", magodoro 80, huduma ya maji safi, pamoja na umeme unaohudumia wanafunzi wapatao 80. Mbali na bweni hilo, TAWA pia imekabidhi darasa moja la kisasa likiwa na meza 45 na viti 45 vya wanafunzi pamoja na viti vinne na meza mbili za walimu katika shule ya Sekond...

Spika wa Bunge la Tanzania azungumzia na baadhi ya Mabalozi wa umoja wa Ulaya

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Azzan Zungu, amekutana na kufanya mazungumzo na baadhi ya Mabalozi wa Nchi Wanachama wa Umoja wa Ulaya wakiongozwa na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU), Mhe. Christine Grau walipomtembelea leo tarehe 4 Desemba, 2025 katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam. Pamoja na mambo mengine, walizungumza kuhusu kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Nchi Wanachama wa Umoja wa Ulaya, ikiwa ni pamoja na kuimarisha diplomasia ya kibunge (Parliamentary Diplomacy). Kikao hicho kimehudhuria na Mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini Tanzania ambao ni Balozi wa Finland, Balozi wa Hispania, Balozi wa Italia, Balozi wa Ubelgiji na Balozi wa Ujerumani.

Vijana watakiwa kulinda amani kupitia msomera historical,Marathon

*Na MASHAKA MHANDO, Tanga* WAKIMBIAJI wapatao 200, wengi wao wakiwa ni vijana, wanatarajiwa *kufukuza upepo* katika uzinduzi wa msimu wa kwanza wa 'Msomera Historical Marathon' utakaofanyika Desemba 13 mwaka huu katika Kijiji cha Msomera, wilayani Handeni, Mkoa wa Tanga. Mbio hizo zimeanzishwa na Kampuni ya Mawasiliano na Uendelezaji Utamaduni nchini (yenye makao makuu Butiama, Mara) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Handeni.  **Kuunga Mkono Uamuzi wa Uhamaji** Mratibu wa shindano hilo, Mashaka Mgeta, alisema mbio hizo zinakwenda kuwakutanisha vijana na wanariadha wakubwa kutoka maeneo mbalimbali nchini ili kuunga mkono dhamira ya wananchi waliokuwa wakiishi wilayani Ngorongoro, Arusha, kuhamia kwa hiari katika Kijiji cha Msomera na kufanya makazi yao ya kudumu. Mgeta, ambaye kitaaluma ni Mwandishi wa Habari na anahudumu Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga kama Ofisa Habari wa Mkoa, alisema kitendo cha kuacha eneo la Ngorongoro kuendelea kuhifadhiwa na kuendeleza utalii...

WANANCHI BABATI WAIPA KONGOLE REA

📌 *Mitungi ya gesi 3,255 kusambazwa  na kuuzwa kwa bei ya ruzuku* 📌 *Mtungi mmoja kuuzwa kwa bei ya ruzuku TZS 17,500*. 📍 *Babati* Kongole hizo zimetolewa leo, tarehe 04 Disemba, 2025 na wananchi wa kata ya Ayalagaya Wilaya ya Babati mkoani manyara wakati wa usambazaji na uuzaji wa mitungi ya gesi kwa bei ya ruzuku katani hapo. Uuzaji wa majiko hayo umeongozwa na  diwani wa kata ya Ayalagaya Mheshimiwa Sabil John , mwakilishi wa mkuu wa wilaya ya Babati, mtendaji kata ya Ayalagaya , Afisa kutoka REA na mwakilishi wa kampuni Manjis Logistics Limited.  "Kinachofanyika leo ni kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia  katika kutunza mazingira na afya za wananchi" amesema Mhe. Sabil. Mhe. Sabil amesema, Lengo la mradi huu unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ni kuendeleza juhudi za utunzaji wa mazingira na Afya za wananchi kwa kuhakikisha wananchi wanapata elimu  na hamasa ya kutosha...

Chuo Kikuu Kairuki chaelezea upasuaji kwa kutumia roboti

Na Mwandishi Wetu VYUO vya afya nchini vimetakiwa kuongeza udahili wa wanafunzi wanaosomea fani ya tiba ili kuziba pengo kubwa lililopo la watumishi wa sekta hiyo kwenye maeneo mbalimbali nchini. Hayo yalisemwa leo  jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu cha Kairuki, Dk Donald Mmari, kwenye mahafali ya chuo hicho yaliyofanyika kwenye kampasi yake Boko jijini Dar es Salaam Kwenye mahafali hayo,  jumla ya wahitimu 426 walitunukiwa vyeti, Shahada, Stashahada na Shahada za Uzamili. Alisema tangu kuanzishwa kwake Chuo cha Kairuki kimetoa mchango mkubwa sana kwa kutoa watumishi wa afya kwenye maeneo mbalimbali wakiwemo madaktari bingwa wa wanawake, watoto na wa upasuaji. Alisema pamoja na mchango mkubwa wa chuo hicho bado kuna upungufu mkubwa wa watumishi wa sekta ya afya hivyo kuna umuhimu wa vyuo kutoa wahitimu wengi. Alisema idadi ya madaktari wanaohitajika katika kila wananchi 100,000 bado ni pungufu kulinganisha na viwango vilivyowekwa na  Shirika la Af...

Vita,Vurugu Havijawahi Saidia Nchi yoyote-Simbachawene

Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,George Simbachawene amewataka wanaharakati na vijana kutafuta njia sahihi ya kudai haki na sio kutumia njia ambazo zinahatarisha usalama wa nchi ambao baaadhi ya nchi amani ilipotea na kupelekea kuzalisha wakimbizi ambao wameenea sehemu mbalimbali duniani ambapo pia amewahakikishia wananchi wa Tanzania amani na usalama kuelekea mwisho wa mwaka. Ametoa kauli hiyo wakati wa Mkutano wa Pili unaohusisha Pande Tatu ikiwemo Serikali ya Tanzania, Jamhuri ya Demokrasia ya Congo na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani UNHCR ambapo pia walitumia mkutano huo kusaini nyaraka zinazoelezea Mpango wa Urejeshwaji wa Wakimbizi Elfu Themanini na Sita na Mia Mbili Hamsini na Sita kutoka nchi ya Congo. ‘Nchi yetu iko na amani na tunakokwenda katika Sikukuu za Mwisho wa Mwaka niwatakie Watanzania wenzangu sikukuu njema na wasiwe na hofu na tunapozungumza mambo haya ya kuwaambia wenzetu warudi kwao na sisi huku hatuna nafasi ya kuwahifadhi b...

Dk Migiro: Tunao wajibu kwa Tanzania ilipo salama

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk. Asha Rose Migiro amesema Watanzania wote kwa pamoja, wanaowajibu wa kuhakikisha taifa linakuwa salama kwa misingi na mazingira mazuri ya kusonga mbele. Akizungumza leo Alhamis tarehe 4 Desemba 2025, jijini Dodoma wakati akifungua Kongamano la Jukwaa la Wanawake ambao wamekutana na mazungumzo kati ya Tanzania, wakitumia kauli mbiu inayosema “Mama ni Amani.” "Tumekutana kama kina mama na kauli mbiu yetu inatuambia mama ni amani. Anapokuwepo mama kuna amani kwa namna mbalimbali. Nitumie nafasi hii kuleta salamu kwenu kutoka kwa Rais Dk.Samia Suluhu Hassan. “Anajua kina mama tunakutana leo, anajua kina baba wataungana nasi leo, anajua vijana wake pamoja na taifa hili zinaonesha vijana ni sehemu kubwa sana ya Taifa letu. “Kwa hiyo Rais Samia anatoa salamu za pekee kwenu na amefurahi kusikia vijana kuungana mama zenu, baba zenu na walezi wenu katika mada hii muhimu ya mama ni amani,” amesema Balozi Dkt. Migiro. Balozi Migiro alisema pia kuwa ...

Dkt.Mwigulu afunga semina elekezi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Desemba 04, 2025 amefunga semina elekezi kwa Mawaziri na Naibu Mawaziri iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam. Semina hiyo ambayo ilifunguliwa na Makamu wa Rais, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ilikuwa na lengo la kuwajengea uelewa wa pamoja kuhusu majukumu, taratibu, maadili na matarajio ya Serikali kwa Wananchi na Taifa kwa ujumla.  Akizungumza katika semina iliyoandaliwa kwa ajili ya Baraza la Mawaziri, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa maarifa waliyoyapata yatasaidia kuwaongoza katika kusimamia Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi, Rasilimali za Umma, Dira 2050, Mipango ya Maendeleo na kuimarisha utoaji huduma kwa wananchi.