Skip to main content

Posts

Showing posts from October 7, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Naibu Rais wa kenya kujitetea kesho Jumanne mbele ya bunge la kitaifa

Naibu wa rais nchini Kenya Rigathi Gachagua amesema kwamba atawasili bungeni hapo kesho ili kujitetea. Naibu huyo ambaye anakabiliwa na mashtaka ya kumuondoa madarakani amesema kuwa atawasili mbele ya bunge pamoja na kundi lake la mawakili mwendo wa saa kumi na moja ili kujitetea. Akizungumza na waandishi habari nyumbani kwake huko Karen Jijini Nairobi, Kiongozi huyo amesema kwamba kabla ya yeye kuwasilisha hoja yake ya kujitetea atahitaji bunge kusikiliza maoni ya Wakenya waliomchagua. Kiongozi huyo alisema anatumai wabunge watamruhusu kujibu tuhuma zote bila kuingiliwa. Gachagua, amesema aliita kikao hicho na waandishi wa habari kutoa utetezi wake kwa Wakenya waliomchagua kabla ya kuwasili mbele ya wawakilishi hao. "Nafikiri ni haki wakati wabunge wataamua kwamba wanataka kumwondoa Naibu Rais afisini, watu waliomchagua Rigathi Gachagua kuwa Naibu Rais wasikie upande wake," akasema. Hoja ya kuondolewa mashtaka iliwasilishwa Septemba 26 na Mbunge wa Kibwezi Magharibi Mwengi M...

Heri ya kuzaliwa kwako Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete

*🎉HERI YA KUZALIWA KWAKO DKT. JAKAYA KIKWETE*  Heri ya siku ya kumbukizi ya kuzaliwa kwako Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kipindi cha mwaka 2005 hadi 2015. Rais Mstaafu Jakaya Kikwete alizaliwa mwezi Oktoba 07, 1950 huko Msoga, Chalinze mkoani Pwani.  GMTV  inakutakia afya njema na Maisha marefu Baba HBD  Rafiki JK

Ivona Bajumuzi Awashauri Wanawake Wajasiliamali Kagera Kusaidiana

  Na Angela Sebastian- Bukoba MWENYEKITI wa chama cha wanawake wajasiriamali mkoani Kagera (TWCC)  mwalimu Ivona Bajumuzi amewashauriwa wanawake wajasiriamali kutafuta namna ya kuwakwamua wenzao kwa kuwapa elimu ambao bado wanashindwa kuondokana na utegemezi kwa wenza wao ili waweze kujiongezea kipato kupitia ujasiriamali. Bajumuzi ametoa ushauri huo wakati akiongea na baadhi ya wanawake wajasiriamali wa Manispaa ya Bukoba waliopata mafunzo ya ujasiriamali yaliyoandaliwa na kampuni ya Stain Group na kufanyika katika ukumbi wa mtakatifu Theresa Bukoba mjini. "Kwasasa hakuna haja ya wanawake kuendelea kuwa tegemezi kwa wenza wao au mtu yoyote hivyo wale ambao tayari wameshapiga hatua za kibiashara wawasaidie wengine kuwapa mbinu za kufanya ujasiriamali kwa kuwapa mawazo,umuhimu na faida za kufanya ujasiriamali ili nao waweze kujikwamua na wimbi la umaskini "alisema Bajumuzi.  Amesema wanawake wengi wanashindwa kufanya ujasiriamali na kisimama wenyewe kutokana na changamoto ...

Uvccm Mara waratibu matembezi ya butiama hadi mwanza kumuenzi mwl Nyerere

   Na Shomari Binda-Musoma VIJANA zaidi ya 1000 wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi ( UVCCM) mkoa wa Mara watafanya matembezi ya  kilometa 143 kutoka Butiama hadi Mwanza kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Akizungumza na GMTV leo oktoba 7 Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM ( UVCCM) mkoa wa Mara Irene Moleli amesema vijana wanaendelea vizuri na kambi iliyopo chuo cha ufundi Veta wilayani Butiama na wapo tayari kwa matembezi hayo. Amesema matembezi hayo yatakayoanza jumatano ya oktoba 9 yana lengo maalum ya kumbukumbu ya miaka 25 ya kifo cha Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Irene amesema Baba wa Taifa amelifanyia Taifa mambo mengi mazuri hivyo kama vijana lazima wamuenzi kwa hayo aliyoyafanya. Amesema moja ya mambo ambayo vijana hao wanafundishwa kwenye kambi hiyo ya mkoa ni uzalendo ambao Mwalimu Nyerere alikuwa akihusisitiza enzi ya uhai wake. Katibu huyo wa vijana mkoa wa Mara amesema vijana waliopo kambini wapo n...

Mkuuwa mkoa wa njombe akabidhiwa tuzo ya afua za lishe na waziri mkuu Mhe.Kassim Majaliwa

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, amepokea tuzo maalum kutoka kwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, kwa mchango wake mkubwa katika utekelezaji wa afua za lishe kwenye sekta mtambuka. Tuzo hiyo ilikabidhiwa hivi karibuni wakati wa hafla ya kufunga Mkutano Mkuu wa Kumi wa Wadau wa Lishe uliofanyika kwenye ukumbi wa Malaika Beach Resort, Jijini Mwanza. Tuzo hii ni ishara ya kutambua juhudi za Mhe. Mtaka na Mkoa wa Njombe katika kuboresha hali ya lishe miongoni mwa wananchi. Akizungumza Ofisini kwake, Mhe. Anthony Mtaka alieleza kufurahia kutambuliwa kwa mchango wa Mkoa wa Njombe kwenye sekta ya Lishe. "Tuzo hii ni uthibitisho kwamba jitihada zetu za kupambana na udumavu na kuboresha afya na lishe katika Mkoa wetu zinaonekana. Hatuishii hapa, Njombe itaendelea kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha tunatokomeza udumavu kupitia mipango madhubuti ya lishe," alisema Mhe. Mtaka alipokuwa akiongea na Afisa Habari Msaidizi, Bw. Chrispin Ka...

Majaliwa:Rais Dkt.Samia ana matumaini makubwa na Taifa stars

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameitembelea Timu ya Taifa ya Tanzania ya Mpira wa Miguu (Taifa Stars) inayofanya mazoezi kwenye uwanja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) jijini Dar es Salaam na kusema kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassaan anamatumaini makubwa kuwa timu hiyo itafanya vizuri kwenye michezo yote miwili. Mheshimiwa Majaliwa ameyasema hayo leo (Jumatatu, Oktoba 07, 2024) alipozungumza  na wachezaji, benchi la ufundi pamoja na viongozi wakiwa katika maandalizi ya michezo miwili ya kufuzu michuano ya AFCON 2025 dhidi ya Congo itakayochezwa Oktoba 10 na 15, 2024.   “Kila mmoja aone ana jukumu kubwa, kwako wewe mwenyewe na kwa nchi yako, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia anawatakia kila la kheri na alichofanya ametoa usafiri wa uhakika wa ndege itakayowapeleka nchini Congo kwa ajili ya mchezo wa Oktoba 10, 2024, hili ni jambo kubwa.” Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa kwa jitihada za Rais Dkt. Samia amefanikiwa kushawishi mashirikisho ya mpira wa miguu ya Afrika na FIFA...