Wananchi waupokea kwa furaha Mpango wa kitaifa wa matumizi bora ya Ardhi unaotekelezwa katika Vijiji 8 vya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mkoani Mwanza . Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, na Maendeleo ya Makazi pamoja na Timu ya Wawezeshaji wa masuala ya Ardhi kutoka Tume ya Taifa ya Mipango na Matumizi bora ya Ardhi mapema wiki hii imetambulisha mpango huo wa matumzi bora Ardhi katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi utakaotekelezwa katika Vijiji 8 kati ya Vijiji 115 vya Wilaya hiyo kwa kutenga maeneo rasmi kisheria kwa matumizi ya huduma za kijamii sambamba na kutoa hati za kimila. Akizungumza katika Mikutano ya Hadhara na Viongozi wa Serikali za Vijiji katika Kijiji cha Gulumungu na Lukanga Afisa wa Tume ya Mipango ya matumizi ya Ardhi Bw. Bwahama Bagenyi ameeleza kwamba Serikali inaendelea kuboresha na kuweka mipango ya upimaji wa maeneo ya Vijiji kwa ushirikiano na Wananchi pamoja na Viongozi, waweze kutenga maeneo yao kwa ajili makazi, Kilimo, malisho, Makaburi, taasisi ...
Marato tv - Sauti ya Jamii