Skip to main content

Posts

Showing posts from September 22, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rais Dkt. Samia Awasili Songea Kuanza Ziara ya Kikazi Mkoa wa Ruvuma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwasili katika uwanja wa Ndege wa Songea kwa ajili ya kuanza ziara ya kikazi Mkoani Ruvuma tarehe 23 Septemba, 2024.

Jeshi la polisi Mwanza lajipanga kudhibiti uvunjifu wa amani

  Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza leo tarehe 22 Septemba 2024, limefanya mazoezi ya utayari kuzunguka maeneo mbalimbali ya Mkoa huo. Mazoezi hayo yamefanyika kwa lengo la kujiweka tayari kukabiliana na viashiria na vitendo vya uvunjifu wa amani hususan maandamano haramu yaliyoitishwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema). Akizungumza wakati wa maonyesho hayo ya utayari Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza Naibu Kamishna wa Polisi Wilbrod Mutafungwa amesema Jeshi la Polisi  limejipanga kikamilifu kukomesha vitendo hivyo na kuimarisha doria maeneo yote ya Mkoa huo Chanzo:Dawati la Habari Polisi Mwanza

Viongozi wa Kimila Nchini Wampongeza Rais Dkt. Samia

  Na Elizabeth Cornely VIONGOZI wa Kimila kutoka mikoa mbalimbali nchini, wamemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuanzisha Tamasha la Utamaduni la Kitaifa pamoja na kuongeza thamani ya viongozi wa mila iliyoonekana kushuka kwa miaka mingi. Wamesema hatua hiyo ya kuthamini, kufufua misingi na kuenzi tamaduni zilizokuwa zimeanza kuwekwa kando itasaidia kwa kiwango kikubwa kulinda maadili na tamaduni za Kitanzania. Wakizungumza kwa nyakati tofauti mkoani Ruvuma linakofanyika kongamano hilo la tatu la utamaduni la kitaifa, viongozi hao wa kimila wamesema kwa miaka mingi mila na tamaduni za Kitanzania zilionekana kutokuthaminiwa lakini Rais Samia ametambua umuhimu wake na kufufua. “Tunamshukuru Chifu Hangaya (Rais Samia), yeye kama kiongozi namba moja wa Machifu wote Tanzania, ameona umuhimu wa kuenzi mila na tamaduni zetu ambazo zilikuwa zimeachwa kupewa kipaumbele sana, kwa kifupi ni kwamba amezifufua na kuupa thamani kubwa utamaduni wa Mtanzania, na kwa kuwa yeye ndiye msimamizi m...

Waziri Mkuu Ashiriki Mkutano wa Summit of Future

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Septemba 22, 2024 akishiriki katika ufunguzi wa Mkutano wa ngazi ya juu wa Wakuu wa Nchi na Serikali ‘Summit of the Future’ uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Umoja wa Mataifa New York nchini Marekani. Mkutano huo unawaleta pamoja  viongozi wa nchi na Serikali duniani ili kujadili masuala mbalimbali ya maendeleo na namna wanaweza kuboresha hali ya sasa na kuzilinda siku zijazo. Mheshimiwa Majaliwa yupo nchini Marekani kumwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano Mkutano wa 79 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UNGA79)

Polisi Simiyu yaimarisha hali ya usalama

Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu Septemba 22, 2024 limefanya doria katika mitaa mbalimbali ya Mji wa Bariadi Mkoani humo kwa lengo la kuimarisha usalama wa raia na mali zao.

Usalama waimarishwa kanda maalum ya Tarime Rorya

Jeshi la Polisi Mkoa wa kipolisi Tarime Rorya leo 22.09.2024 limefanya zoezi la kujaribu vitendea kazi vyake vyote vya kulinda raia na mali zao  ili kujiweka tayari kwa lolote litakalojitokeza. Vitendea kazi hivyo ikiwemo magari ya doria ya kawaida na magari ya maji washa, kikosi cha mbwa na farasi na kikosi vya Usalama barabarani  na kikosi cha  kuzuia ghasia vilionekana katika doria  mitaa mbali mbali ya Mji wa Tarime ,Sirari na Rorya ili kuwaondoa hofu raia wema  wanaofuata sheria na taratibu za nchi na kuwahakikishia kuwa ulinzi na usalama wao umeimarika. Aidha, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tarime Rorya SACP Mark Njera amefanya ukaguzi wa vitendea kazi hivyo pamoja na ukakamavu wa askari kuhakikisha wepesi wao katika kukabiliana na uhalifu na wahalifu na kupongeza uimara wao uluotokana na mazoezi ya Utayari ya mara kwa mara.

Benki ya dunia yaipa kongole Misungwi kwa utekelezaji Mzuri wa miradi ya Boost na Sequip

Benki ya Dunia nchini imeeleza kuridhishwa na ubora wa miradi ya elimu iliyotekelezwa na Serikali wilayani misungwi Mkoani Mwanza kupitia ufadhili wa Benki hiyo. Mwakilishi wa  Benki ya Dunia  nchini Dkt.Safari Aquiline amebainisha hayo wakati wa ukaguzi wa miradi ya ujenzi wa shule ya awali na msingi Shilabela pamoja na shule ya sekondari Mwambola zilizoko wilayani humo.   Dkt.Aquiline amesema kuwa ujenzi wa shule hizo uliotekelezwa kupitia mradi wa kuboresha mazingira ya Ujifunzaji na Ufundishaji kwenye shule za awali na Msingi nchini(BOOST) pamoja na mradi wa kuboresha elimu ya Sekondari nchini (SEQUIP) umefanyika kwa viwango vya ubora na thamani ya shilingi billioni 1.124 zilizotumika  inaonekana.   “Nashukuru sana maana ukienda mahali ukakuta Mmama anashika hatamu unafurahi,umeupiga mwingi sana,umeupiga mwingi kwa kusaidiana na mkurugenzi.What you did is the real outcome of what we want to be reflect”alisema Dkt.Aquiline na kuongeza kuwa   “Baada ...