Skip to main content

Posts

Showing posts from April 11, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Fedha Zilizokusanywa Bunge Marathoni Zinatumika ipasavyo-Majaliwa

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amewahakikishia Watanzania fedha zilizokusanywa katika mbio za hisani za Bunge zitakwenda kutumika kama ilivyokusudiwa. Ameyasema hayo leo (Jumamosi, Aprili 12, 2025) katika mbio za hisani za Bunge zilizolenga kuchangisha fedha za ujenzi wa Shule ya Sekondari Bunge Wavulana. Ujenzi wa shule hiyo shule hiyo itakayokuwa na uwezo wa kusajili wanafunzi wasiopungua 300 hadi 350 kwa mwaka utagharimu zaidi ya shilingi bilioni tatu. Shule hiyo ya kidato cha tano na sita itajengwa katika eneo la Kikombo, Jijini Dodoma karibu kidogo na shule ya wasichana iliyojengwa na wabunge wanawake 2020. “Ninawapongeza sana Wabunge wenzangu kwa kuweka alama na kugusa maisha ya Watanzania na watoto wetu wa kiume watakaopata fursa ya kusoma katika shule hiyo.” Amesema ujenzi wa shule hiyo ni mpango wa Bunge wa kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia suluhu Hassan katika kukuza na kuendeleza sekta ya elimu. Shule hiyo ya bweni itakuwa maabara nne za biolojia, kemia, fiziki...

"Rto" Mara Ahimiza Umakini Kwa Madereva Ajali ya Tata Ikinusuru Kifo Musoma Vijijini

Na Shomari Binda-Musoma  ABIRIA waliokuwa wakisafiri na bus la Spider aina ya Tata lenye namba za usajili T 703 DDS kutoka Musoma mjini kuelekea Musoma Vijijini wamenusulika vifo baada ya bus hilo kupinduka jana jioni. Bus hilo liliacha njia na kupinduka katika Kijiji cha Murunyigo Kata ya Ifulifu ambapo mashuhuda walioshuhudia ajali hiyo wamedai dereva wa gari hilo alikuwa mwendo kasi. Wakizungumza na GMTV eneo la ajali hiyo mashuhuda hao wamesema mwendo usiokuwa wa kistarabu ndio uliopelekea gari hilo kupinduka. Juma Katundu mmoja wa walioshuhudia ajali hiyo amesema madereva wa njia hiyo wamekuwa wakiendesha mwendo kasi na kuomba jeshi la polisi kupitia kitengo cha usalama barabarani kuongeza nguvu kw3nye njia hiyo. " Madereva njia hii ya Majita wanaendesha kwa kasi sana huku wakiwa wanafukuzana kuwahi abilia hii ni hatari sana. " Hili ni bus la pili kwa siku za hivi karibuni kupinduka lakini tunaehukuru Mungu hakuna vifo vilivyotokea eneo la ajali hatujui wakati wakipewa h...

China nayo yajibu Rais Trump kwa kuongeza ushuru

 CHINA Ijumaa ilimjibu Rais Donald Trump kwa kuongeza ushuru kwa bidhaa inazoagiza kutoka Amerika kwa asilimia 125, huku ubabe wa kibiashara kati ya nchi hizo ukiendelea kutikisa ulimwengu kibiashara. Rais Trump alikuwa amepandisha ushuru kwa bidhaa ambazo Amerika inaagiza kutoka China hadi asilimia 145 wiki hii. China na Amerika zimekuwa na ubabe wa kibishara tangu Trump aingie mamlakani Januari, na kusababisha thamani za sarafu mbalimbali duniani kushuka. “Hatua ya Amerika inakiuka kanuni za kibiashara ulimwenguni. Huu ni udikteta wa kibiashara,” ilisema Wizara ya Masuala ya Kigeni ya China. Kiongozi huyo wa Amerika wiki hii aliweka ushuru kwa mataifa mbalimbali lakini baadaye akaghairi nia na kuzisitisha kwa muda wa siku 90. Hata hivyo, ushuru ambao uliwekewa bidhaa za China haukuondolewa. “Hatua ya Amerika kuweka ushuru wa juu, inakiuka kanuni za kibiashara za ulimwenguni. Huu ni udikteta wa kibiashara,” ikasema wizara ya masuala ya kigeni ya China. Rais Xi Jinping naye alisema...

Mataifa Yanayoendelea Yatamuweza Trump?

Na Obunde Michael TAIFA la Sudan Kusini limepigishwa magoti na Amerika hivi majuzi! Limesalimu, likampisha Marekani ili lisivunjwe mbavu bure.  Ukiona cha mwenzio kikinyolewa, chako tia maji. Busara hizo za wahenga zinaweza kutumiwa na mataifa yanayoendelea, hasa wakati huu wa misukosuko mikuu ya uhamiaji na vita vya kiuchumi. Marekani na Sudan Kusini zilikosana pale Sudan Kusini ilipokataa kumpokea mtu aliyefukuzwa na serikali ya Rais Donald Trump kwa kuwa mhamiaji asiyekuwa na kibali cha kuishi Amerika. Sudan Kusini ilimkataa mtu aliyeitwa Bw Nimeri Garang alipofika kwenye Uwanja wa Ndege wa Juba kwa kuwa, baada ya kumhoji, ilithibitishwa jina lake halisi ni Bw Makula Kintu, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Idara ya Uhamiaji ya Sudan Kusini ilisema Bw Kintu mwenyewe alisema aliondolewa Marekani bila hiari yake, tena akalazimishwa kwenda Juba. Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Bw Marco Rubio, alichemka kwa hasira na kulipa kisasi mara moja! Alitoa amri iliyowazuia...

Hakuna Maendeleo Yanayowezekana Bila Amani na Mshikamano wa Kitaifa - Dkt. Biteko

📌 Asisitiza uwekezaji katika elimu inayozingatia sayansi, teknolojia na ubunifu 📌 Awasihi Watanzania kuziishi falsafa za Mwl. Nyerere 📌 Chuo cha Mwl. Nyerere cha adhimisha miaka 103 ya kuzaliwa kwa Mwl. Nyerere Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewaasa Watanzania kuendeleza fikra za Mwl. Nyerere kwa kuwekeza katika sekta za elimu, kilimo, viwanda, teknolojia na biashara ndogo ndogo zinazotegemewa na wananchi wengi ili kukuza uchumi jumuishi.  Aidha, Serikali na sekta binafsi zinapaswa kushirikiana ili kuhakikisha uwekezaji unaleta tija kwa wananchi wa kawaida. Dkt. Biteko amesema hayo leo Aprili 11, 2025 jijini Dar es salaam wakati aliposhiriki katika Kongamano la Kumbukizi ya Kuzaliwa Kwa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere. Amesema Kongamano hilo lenye mada inayosema Maono ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika Elimu, Uwekezaji na Ujenzi wa ...

Utekelezaji wa Ilani Jimbo la Tarime Vijijini Wampa Waitara Uhakika wa Kurejea Bungeni

Na Shomari Binda-Musoma  UTEKELEZAJI wa ilani ya uchaguzi ya mwaka 2020/2025 kwenye Jimbo la Tarime Vijijini umempa uhakika mbunge wa jimbo hilo Mwita Waitara kurejea bungeni kwenye uchaguzi wa 2025. Kauli hiyo ameitoa leo aprili 11 bungeni jijini Dodoma wakati akichangia Bajeti Kuu ya Serikali kwenye Kikao cha 4 cha Mkutano wa 19 wa Bunge la 12. Akianza kutoa mchango wake ameishukuru serikali ya awamu ya 6 chini ya Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kupeleka fedha nyingi kwenye jimbo hilo kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ikiwemo ya elimu. Mbunge huyo amesema tangu mwaka 2021 majengo ya madarasa 376,yenye thamani ya zaidi ya bilioni 7 yamejengwa na shule mpya 19  zimejengwa,madawati,viti pamoja na meza. Amesema ujenzi wa madarasa na shule hizo imewezesha wanafunzi kupata elimu ya uhakika na hakuna mzazi aliyechangishwa fedha. Waitara amesema licha ya sekta ya elimu ndani ya jimbo la Tarime Vijijini wakandarasi wapo kazini kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ya maji,af...

Vyama Vya Siasa Vitakavyoshiriki Uchaguzi Mkuu Kujulikana Kesho Aprili 12

Na. Mwandishi Wetu Dodoma Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, vyama vya siasa na Serikali kesho tarehe 12 Aprili, 2025 wanatarajiwa kusaini Kanuni za Maadili ya Uchaguzi yatakayotumika kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Akizungumza kwenye mahojiano maalum na vyombo vya habari mkoani Dodoma leo tarehe 11 Aprili, 2025 Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndugu. Kailima Ramadhan amesema chama cha siasa ambacho hakitasaini maadili hayo hakitaruhusiwa kushiriki kwenye uchaguzi huo. Ndugu. Kailima amesema maadili hayo yameandaliwa kwa mujibu wa kifungu cha 162 (1), (2) na (3) cha Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani Na. 1 ya Mwaka 2024 ambacho kinaitaka Tume baada ya kushauriana na vyama vyote vya siasa na Serikali, kuandaa na kuchapisha katika Gazeti la Serikali Kanuni za Maadili ya Uchaguzi zitakazoainisha maadili ya vyama vya siasa, Serikali na Tume wakati wa kampeni za uchaguzi na uchaguzi na utaratibu wa utekelezaji wake. Amesema ki...

Balozi Nchimbi Akutana na Mwenyekiti wa Wabunge wa Ccm, Spika wa Bunge

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), ambaye ni Waziri Mkuu wa Tanzania, na Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mwansasu (Mb), Spika wa Bunge la Tanzania, pia Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), wakizungumza jambo wakati wakiagana baada ya kikao cha mashauriano kilichofanyika leo Ijumaa, tarehe 11 Aprili 2025, ofisini kwa Balozi Nchimbi, Makao Makuu ya CCM, jijini Dodoma. Pichani kushoto ni Ndugu John Mongella, Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara).

Rais Mstaafu Jakaya Kikwete Akabidhi Ujumbe wa Rais Samia Kwa Waziri Mkuu wa Ethiopia

 Rais Mstaafu wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete amewasilisha ujumbe Maalum wa Rais wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa Waziri Mkuu wa Ethiopia, Dkt. Abiy  Ahmed. Ujumbe huo umewasilishwa Ikuku jijini Addis Ababa April 11, 2025.   Mhe. Kikwete pia aliwasilisha Salamu za Rais Samia ambazo zilisisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiono wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Ethiopia  ambao uliimarika tokea  kipindi cha uanzishwaji wa Umoja wa Afrika.

Rais Samia Afanya Mazungumzo na Mmiliki wa Klabu ya Mpira Wa Miguu ya Manchester United

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mmiliki wa Klabu ya Mpira wa Miguu ya Manchester United ya Uingereza Sir Jim Ratcliffe, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Aprili, 2025. Katika mazungumzo yao Rais Dkt. Samia amemshukuru Sir Jim Ratcliffe kupitia Taasisi yake ya Six Rivers ambayo ina shughulika na masuala ya Uhifadhi, kwa namna inavyofanya vizuri katika kudhibiti muingiliano wa wanyamapori na binadamu kwa kushirikiana na Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) pamoja na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI).   Kupitia Taasisi yake ya Six Rivers, Sir Jim Ratcliffe amebainisha kuwa Taasisi hiyo imedhamiria kurejesha hadhi ya Hifadhi ya Taifa ya Selous na kuwa na Wanyama wakubwa katika Hifadhi hiyo. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi zawadi ya picha pamoja na Jezi ya Timu ya Taifa Tanzania (Taifa Stars) yenye Ujumbe wa, “Amaizing Tanzania” kw...