Skip to main content

Posts

Showing posts from December 15, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Kuweni Baraka,Sio Kitunguu Kuwatoa Machozi Wengine-Dkt. Biteko

*📌 Amwakilisha Rais Samia hafla ya kutabaruku kanisa SDA- Magomeni* *📌 Ataka watu kutengenezeana furaha badala ya kuumizana* *📌 Ahimiza Mshikamano wa Taifa ili kuleta maendeleo* *Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka Watanzania kujenga misingi ya kusaidiana kuheshimiana na kuvumiliana ili kufanikisha malengo wanayojiwekea kimaendeleo. Dkt. Biteko ametoa rai hiyo leo Desemba 15, 2024 Jijini Dar es Salaam alipomwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa mgeni maalum katika Hafla ya Kutabaruku Jengo la Kanisa la Waasventista Wasabato, Magomeni. Amewahimiza waumini na Watanzania kwa ujumla kuboresha huduma za jamii na kuwekeza katika mipango itakayowezesha kukidhi mahitaji na kupata Taifa endelevu. “ Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan siku zote amekuwa akisisitiza maridhiano, uhimilivu, mabadiliko na kuimarisha amani yetu il...

Dkt. Biteko ashiriki Hafla ya Uwekaji Wakfu Kanisa SDA-Magomeni

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa  Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameshiriki hafla ya uwekaji Wakfu Jengo la Kanisa la Waadventista  wa Sabato Magomeni inayofanyika leo Disemba 15, 2024 jijini Dar es Salaam. Dkt. Biteko amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambapo Kanisa hilo limewekwa Wakfu na Mchungaji Joel Okindo, Msaidizi wa Mwenyekiti wa Divisheni ya Afrika Mashariki na Kati (ECD).

Mtanzania na Raia wa Kigeni Wakutwa na Shehena ya Nyaya za Tanesco

  Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Rujifi limewakamata Watu wawili ambapo mtu mmoja akiwa na asili ya Kiasia na mwingine akiwa ni Mtanzania kwa tuhuma za kukutwa na shehena ya nyaya za shaba mali zilizoibwa katika Miundombinu ya Umeme - TANESCO na Shirika la Reli Tanzania (TRC).  Kupitia taarifa iliyotolewa na Jeshi la polisi imeeleza kuwa Watuhumiwa hao walikutwa na copper block 426 zenye uzito wa kilogramu 7,728 na Cooper Wire zenye uzito wa kilogramu 2628.5 ambazo ni  mali za TANESCO zilizoibwa pamoja na Waya za Copper za TRC zenye uzito wa kilogramu 430. Chanzo cha kukamatwa kwa Watuhumiwa hao ni baada ya kukamatwa gari aina ya Fuso lililokuwa likisafirisha Nyaya hizo kutoka kiwanda chao kwenda kuzificha kutokana na masako mkali wa jeshi la Polisi unaoendelea Mkoani humo. Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Rujifi limetoa wito kwa Wananchi wote kuendelea kutoa ushirikiano katika kubaini, kuzuia na kuwakamata wale ambao hawataki kufuata njia halali za kujipatia kipa...

Mwauwasa kujenga visima viwili na kuboresha mtandao wa maji Ngudu

  MRADI MPYA KUIMARISHA HUDUMA YA MAJI NGUDU  *DC KWIMBA AIPONGEZA WIZARA YA MAJI*  Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mwanza (MWAUWASA) imeanza utekelezaji wa mradi wa ufufuaji Visima Viwili na Uboreshaji wa Mtandao wa Maji kwa KM 4.5 unaolenga kunufaisha wakazi wa mji wa Ngudu Wilayani Kwimba kwa kuimarisha upatikanaji wa huduma ya maji. Akizungumza wakati wa zoezi la mapokezi ya Shehena ya kwanza ya bomba yenye urefu wa KM 1.5, Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija ameshukuru Serikali kupitia Wizara ya Maji kwa kutekeleza ahadi kwa wakati na kusimamia nia ya Mhe. Raisi ya kumtua mama ndoo ya maji kichwani. "Tumekuwa na changamoto ya uchakavu wa bomba kuu linalosafirisha maji kutoka chanzo cha Ihelele na kuhudumia Mji huu na Wizara kupitia Mhe. Waziri Jumaa Aweso aliahidi kutafuta mbadala wa haraka kwa mpango wa muda mfupi, tunaona leo mmetekeleza na kazi imeanza, nawapongeza kwa kubuni mradi huu na nawasisitiza MWAUWASA mfanye kazi hii kwa bidii ili...