Skip to main content

Posts

Showing posts from January 31, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Askari Wapya JWTZ wahitimu mafunzo

  Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Jacob John Mkunda amefunga rasmi Mafunzo ya Askari wapya katika hafla iliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Mafunzo ya Awali ya Kijeshi (RTS) Kihangaiko Msata Mkoani Pwani leo tarehe 31 Januari 2025. Jenerali Mkunda amewataka askari wapya kukiishi na kuzingatia kiapo cha utii wakati wote watakapokuwa wakitekeleza majukumu yao sehemu mbalimbali watakayopangiwa, huku akisisitiza kuchukuliwa hatua kwa askari watakaokwenda kinyume na kiapo chao. Askari wapya wameaswa kutotenda mambo ambayo ni kinyume na taratibu za kijeshi ikiwemo kutojihusisha na siasa, matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii, matumizi ya madawa ya kulevya, michezo ya kamari na kuepuka madeni yasiyo na tija. Mkuu wa Majeshi amewataka Askari hao kutunza Afya zao na kuzingatia lishe bora wakati wote wanapotekeleza majukumu yao. Aidha, wasijihusisha na uhalifu wa aina yoyote kwani watakuwa wamekwenda kinyume na sheria na taratibu za kijeshi hivyo watachukuliwa hatua za kinidhamu. Je...

Waziri Mkuu Aipongeza Benki ya Azania Kwa Jinsi Inavyoshiriki Mambo ya Kijamii

  DODOMA Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Lameck Nchemba leo Januari 31, 2026 ameshiriki kwenye Azania Bank Bunge Bonanza 2026 linalofanyika katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya John Merlin jijini Dodoma ambapo ametumia nafasi hiyo kuwashukuru Azania Bank kwa kuendelea kuzamini Bonanza hilo. Amesema Bonanza hilo limefana sana kutokana Azania Bank kulipamba na mwitikio wake ni mkubwa. Akizungumza Mara baada ya kumaliza Matembezi, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu ametoa rai kwa watanzania kuweka ratiba ya kufanya Mazoezi kwajili ya Afya zao pamoja na kuleta umoja wa Kitaifa. "Nitoe Rai Kwa watanzania kuweka ratiba ya kufanya Mazoezi kwajili ya Afya zao na kuleta umoja Kwa Kitaifa, na kufanya Mazoezi ni jambo jema la Afya, hivyo Kila mmoja atenge Muda wake Afanye mazoezi ili kuondokana na Magonjwa yasiyo ya kuambukiza". Amesisitiza Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Azania Dkt. Esther Mang'enya amesema pamoja na Kuwezesha uchumi lakini pia Azania ...

Mkuu wa Wlaya ya Kyerwa Atoa Onyo Kali Kwa Watendaji wa Kata na Vijiji

  Mkuu wa Wilaya ya Kyerwa Zaitun Msofe amewataka watendaji wa kata na vijiji kuakikisha wale wote wanaoandikishwa kwenye daftari la wakazi wawe ni Raia wa Tanzania pekee huku akisema kuwa atakayeandikisha mtu asiye raia wa Tanzania kwa maslai yake binafsi hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.  Msofe amesema kuwa Serikali imeanzisha zoezi hilo ili kuwatambua wenyeji na wageni wanaishi katika Wilaya hiyo kwa utaratibu maalumu ikiwa na lengo la kulinda usalama wa Wilaya hiyo na wananchi wake. Msofe ametoa agizo hilo katika kikao cha baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo ambacho kimejadili taarifa ya utekelezaji ya miradi ya maendeleo kwa robo ya pili ya mwaka wa fedha 2025/2026 ambapo,amesema uandikishaji huo ni nguzo muhimu ya kuimarisha ulinzi na usalama wa Wilaya hiyo na nchi kwa sababu Wilaya hiyo iko mpakani. Wakati huohuo baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo wametoa wiki moja kwa wazazi wote ambao hawajapeleka watoto wao waliochaguliwa kuanza kidato ch...

Rais Samia Aibuka Kinara Tuzo za Uhifadhi na Utalii

● Atunukiwa Tuzo Maalum ya Kiongozi Mwenye Maono ● Watalii wa kimataifa wafikia zaidi ya milioni 2.09 mwaka 2025 RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ameibuka kinara wa Tuzo za Kitaifa za Uhifadhi na Utalii (Serengeti Awards) kutokana na uongozi wake bora na wa kimkakati katika kukuza sekta ya Maliasili na Utalii kupitia jitihada zake za kutangaza vivutio vya Tanzania kimataifa. Katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Kitaifa za Uhifadhi na Utalii (Serengeti Awards) iliyofanyika leo Januari 31, 2026 katika Ukumbi wa Mount Meru Hotel jijini Arusha, Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alitunukiwa Tuzo Maalum ya Kiongozi Mwenye Maono (Visionary Leadership Award) kwa mchango wake mkubwa katika kukuza utalii na uhifadhi wa maliasili, hususan kupitia filamu za Tanzania The Royal Tour na Amazing Tanzania, pamoja na juhudi zake za kutafuta rasilimali fedha kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya utalii na kuimarisha uhifadhi. Tuzo hiyo ilipokelewa kwa niaba yake ...

Waziri Mkuu Atembelea Hifadhi ya Taifa ya Arusha

*Lengo ni kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia kuhamasisha utalii* WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Jumamosi, Januari 31, 2026 ametembelea Hifadhi ya Taifa ya Arusha ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuhamasisha utalii Waziri Mkuu amempongeza Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake za kuvitangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini. “Mheshimiwa Rais Dkt. Samia amekuwa mstari wa mbele katika kuviuza vivutio vyetu vya utalii duniani kote, sote ni mashahidi namna alivyoshiriki filamu za Tanzania The Royal Tour na The Amazing Tanzania ambazo zimechochea kuitangaza Tanzania na vivutio vyetu kimataifa.” “…Na ndiyo maana na mimi nimepata msukumo wa leo kuja hapa kujionea vivutio vyenu kama sehemu ya kumuunga mkono kwa jitihada zake hizo.” Akiwa katika hifadhi hiyo, Mheshimiwa Waziri Mkuu ameitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia taasisi zake za uhifadhi kuendelea kutunza mazingira ya hifadhi mbalimbali nchini ili ziwe ...

Siku Mia za Rais Samia , Mafanikio Makubwa Wizara ya Elimu,Sayansi na Tenolojia

 DODOMA  Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ndani ya siku 100 imetekeleza mpango mkakati wa kisayansi wa kujenga umahiri wa kusoma, kuandika na kuhesabu (KKK) kwa Watoto wa Elimu ya awali na darasa la kwanza hadi la pili ili kukabiliana na changamoto ya uwepo wa wanafunzi wanaohitimu Elimu ya msingi wakiwa hawajui kusoma. Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 31Januari, 2026, Waziri wa Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema Mpango mkakati huo unaotekelezwa ndani ya miaka mitano unalenga kuhakikisha Kila mtoto anamudu stadi za Msingi afikapo darasa la tatu kupitia njia za kisayansi shirikishi na bunifu. "Wataalamu wa elimu wameonesha wazi kuwa katika nchi yetu, ndani ya miaka minane ya mwanzo, watoto wetu huwa katika umri muafaka kabisa wa kujenga misingi ya mawasiliano na uelewa wa kusoma". Amesema "Tunapojua kwamba mtoto huanza Darasa la Kwanza akiwa na umri wa miaka sit...

Dkt. Mwigulu Kumuwakilisha Rais Dkt. Samia Kwenye Hafla ya Utoaji Tuzo za Uhifadhi na Utalii

WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 31, 2026 amewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) ambapo anatarajiwa kumwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika hafla ya Utoaji wa Tuzo za kitaifa za Uhifadhi na Utalii (The Serengeti Awards). Pia, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu atatembelea Hifadhi ya Taifa ya Arusha ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Mhe. Rais Dkt. Samia katika kukuza Utalii nchini.