Na: Dk. Reubeni Lumbagala Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) ina jukumu la kutoa mikopo kwa waombaji ili waweze kutimiza malengo yao ya kupata elimu katika taasisi mbalimbali za elimu kama vyuo vya kati na vyuo vikuu. Pia, HESLB inawajibika kukusanya mikopo kutoa kwa wanufaika wake ili kuwezesha waombaji wengine waweze kupata mikopo ili nao waweze kupata elimu. Kwa zaidi ya miaka 20 sasa, serikali kupitia HESLB, imewezesha vijana wengi wa Kitanzania kutimiza malengo yao ya kielimu kwa kuwakopesha mikopo ya elimu. Wengi wa vijana hao ni wale wanaotoka familia zenye changamoto za kiuchumi ambazo pengine bila kuwezeshwa mikopo, wasingeweza kumudu kupata elimu kutokana na gharama kubwa za elimu zilivyo huko vyuoni. Hii ndiyo kusema, baadhi yao wasingeweza kutimiza ndoto zao za kusoma fani na taaluma mbalimbali kama wasingepata mkopo wa elimu. Kwa kuwa tayari fedha nyingi zimewekezwa kwa kukopesha vijana wengi, HESLB inayo kazi kubwa ya kukusanya mikopo hiyo kutoka kwa...
Marato tv - Sauti ya Jamii