Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limeadhimisha miaka 62 tangu kuanzishwa kwake Septemba 1, 1964, huku maadhimisho hayo yakifanyika sambamba na kufungwa kwa Wiki ya Sita ya Ushirikiano wa Kijeshi na Kiraia ya Majeshi ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Akizungumza katika hafla hiyo iliyofanyika Viwanja vya Gofu vya Lugalo jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Jacob John Mkunda, amesema historia ya JWTZ imejengwa kupitia utekelezaji wa majukumu ya kulinda taifa pamoja na kushiriki katika shughuli zinazogusa maisha ya wananchi. Jenerali Mkunda amesema JWTZ limeendelea kuimarisha uwezo wa askari wake ili kukabiliana na majukumu mbalimbali ya kitaifa, huku misingi ya uzalendo, weledi na uwajibikaji ikiendelea kuwa sehemu ya utendaji wa jeshi hilo. Kwa mujibu wa Jenerali Mkunda, maadhimisho hayo yamekuja wakati ambapo nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki zinaendelea kutafuta njia za kuongeza ushirikiano wa majeshi yao, si katika masuala ya kijeshi...
Marato tv - Sauti ya Jamii