Skip to main content

Posts

Showing posts from August 10, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

JWTZ Kuzindua Mashindano ya Kuhuisha Sanaa ya Muziki wa Dansi Wenye Asili ya Tanzania na Afrika

JESHI la ulinzi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) linakusudia kuzindua mashindano yanayolenga kuhuisha Sanaa, na muziki wa dansi wenye asili ya kitanzania na Africa. Uamuzi huo wa JWTZ umechukuliwa baada ya kubaini kuanza kusahaulika kwa Sanaa hiyo na kwamba  mashindano hayo yatawezesha watanzania kujivunia utamaduni wao, na kuleta mabadiliko makubwa ya kimaadili kwa Taifa. Mwenyekiti wa kamati iliyoundwa na Mkuu Wa Majeshi Jenerali Jacob John Mkunda, kwa ajili ya maandalizi ya mashindano hayo ya muziki wa dansi na ngoma za asili, Meja Jenerali Mbaraka Mkeremy ,ametangaza uamuzi huo leo Agosti 10-2024 wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa jeshi wa Msasani Club Jijini Dar es Salaam. Amesema baada ya kuzorota kwa Sanaa hiyo hapa nchini, jeshi la ulinzi wa wananchi kupitia kwa mkuu wake wa majeshi,aliunda kamati kwa kushirikisha wadau mbalimbali ambayo pamoja na mambo mengine imeandaa mashindano hayo ili kuhuisha Sanaa hiyo nchini. Meja jenearali Mkeremy,amesema kuto...

JWTZ Kuzindua Mashindano ya Kuhuisha Sanaa ya Muziki wa Dansi Wenye Asili ya Tanzania na Afrika

JESHI la ulinzi la wananchi wa Tanzania (JWTZ) linakusudia kuzindua Mashindano yanayolenga kuhuisha Sanaa na muziki wa dansi wenye asili ya kitanzania na Africa ambao umeanza kusahaulika nchini, hatua ambayo itawezesha watanzania kujivunia utamaduni wao, na kuleta mabadiliko makubwa ya kimaadili kwa taifa. Mwenyekiti wa kamati iliyoundwa na Mkuu Wa Majeshi Jenerali Jacob John Mkunda, kwa ajili ya maandalizi ya mashindano hayo ya muziki wa dansi na ngoma za asili, Meja Jenerali Mbaraka Mkeremy , amesema baada ya kuzorota kwa Sanaa hiyo hapa nchini, jeshi la ulinzi wa wananchi kupitia kwa mkuu wake wa majeshi, litazindua mashindano hayo August 19 mwaka huu, kwa kushirikisha Mziki wa Dansi na Vikundi vya Ngoma za asili kutoka maeneo mbalimbali hapa nchini. Meja Jenerali Mkeremy, amewaambia waandishi wa habari kuwa mashindano hayo ambayo pia ni sehemu ya shamrashamra za maadhimisho ya miaka 60 ya kuzaliwa kwa jeshi la ulinzi la wananchi Tanzania (JWTZ), na kwamba kamati imebaini baadhi ya ...

Takukuru Mara Kushirikiana na Waandishi wa Habari Kutoa Elimu ya Rushwa Kwenye Uchaguzi

Na Shomari Binda-Musoma WAANDISHI wa Habari wametajwa kuwa na nguvu kubwa kwenye mapambano dhidi ya Rushwa kuelekea uchaguzi serikali za mitaa na uchaguzi mkuu. Kauli hiyo imetolewa Agosti 9 na mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Mara Muhamed Shariff kwenye kikao kazi baina ya ya taasisi hiyo na Waandishi wa Habari. Amesema Kifungu cha 7(b)kikisomwa pamoja na kifungu cha 45 cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ( Sura ya 329) kinaitaka Takukuru ihamasishe ushiriki wa wadau katika kuondoa Rushwa nchini. Amesema Takukuru inatambua kwamba Waandishi na vyombo vya habari vinaaminika sana katika kuhakikisha taarifa au habari muhimu  sana kwa ustawi wa wananchi inawafikia Sharif amesema Waandishi na vyombo vya habari wanashughulikia uzalendo na uhai wa nchi kwa kutoa habari za kuelimisha ,kuburudisha na kuonyesha njia. " Waandishi na vyombo vya habari mna aminiwa sana na mnao ushawishi mkubwa kwa watanzania kwa hiyo utumieni ushawishi huo kuwaelekeza...

Man Kifimbo, 2T na Salma Queen Wanogesha Tamasha la Zanzibar Reggae Festival 2024

Na Andrew Chale, Zanzibar. WASANII wa muziki wa Rege Man Kifimbo (Tanzani), 2T Reggae Man (Rwanda), Salma Queen (Kenya) na msanii Nast Sterling (Jamaica) wameweza kukonga nyoyo wapenzi wa muziki huo kwenye msimu wa sita wa Zanzibar Reggae Festival 2024, katika viunga vya Ngome Kongwe, Mambo Club usiku wa Agosti 9,2024. Wasanii hao kwa nyakati tofauti wameshambulia jukwaa kwa nyimbo zao mbalimbali zenye ujumbe na kuburudisha. Awali Msanii Man Kifimbo alifungua pazia kwa mwaka huu na kupiga nyimbo zake kama; Nipe Tano, Nunu, Sema basi, Money Money Pesa, Usikate miti, Usinga na zingine nyingi huku msanii 2T aliwekukonga na nyimbo zake kama, Fasha, Champion Woman  na nyingine nyingi. Wasanii Salma Queen yeye aliburudisha na nyimbo kama Two face, People Rise, Mama Africa na nyingine nyingi huku Msanii Nat Sterling yeye akikonga na nyimbo kama Rasta shine na nyingine. Aidha, usiku wa leo Agosti 10, 2024, Msanii Mkongwe wa rege, Ras Gwandumi kutoka Tanzania Bara,Ras Coco (Zanzibar),Kushit...