Skip to main content

Posts

Showing posts from June 23, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

DPP KENYA;WANAFUNZI SITA KUKABILIWA NA MASHTAKA 16 YA MAUAJI

  Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) nchini Kenya imeidhinisha kufunguliwa kwa mashtaka dhidi ya wanafunzi Sita wanaotuhumiwa kuhusika na tukio la moto lililotokea katika shule ya Utumishi Girls Academy, Kaunti ya Nakuru, tarehe 28 Mei 2026. Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Ofisi ya DPP tarehe 23 Juni 2026, faili la uchunguzi wa awali lililowasilishwa na Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) limefanyiwa tathmini ya kina na kubaini kuwepo kwa ushahidi wa kutosha wa kuendelea na hatua za kisheria dhidi ya watuhumiwa. DPP amesema kuwa wanafunzi wanaohusishwa na tukio hilo watakabiliwa na mashtaka 16 ya mauaji, yakitokana na vifo vya wanafunzi 16 vilivyoripotiwa kufuatia ajali hiyo ya moto iliyotikisa taifa la Kenya. Katika taarifa hiyo, DPP ameonesha wasiwasi mkubwa kuhusu ongezeko la matukio ya uchomaji moto na vitendo vingine vya uhalifu vinavyoripotiwa katika taasisi za elimu nchini humo. Aidha, amesisitiza kuwa watu wote watakaobainika kuhusika na makosa...

MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA YACHANGIA VIFO VINGI NCHINI-MCHENGERWA

 Waziri wa Afya, Mhe Mohammed Mchengerwa amesema kuwa magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza yamesababisha vifo kwa watoto wachanga kuanzia umri wa mwaka 1 hadi 5 zaidi ya elfu 12 kila mwaka huku ugonjwa wa kansa ukikatisha maisha ya watanzania zaidi ya elfu 43 kila mwaka. Hayo amebainisha leo Juni 23, 2026 jijini Dar es Salaam katika Mkutano Mkuu wa Tatu wa Kimataifa wa Kimkakati wa Kikanda wa PEN-Plus (ICPPA 2026), unaowakutanisha viongozi, watunga sera, wataalamu wa afya, watafiti, washirika wa maendeleo na wadau mbalimbali kutoka nchi za Afrika na sehemu nyingine za dunia ambapo amesema magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza huchukua zaidi ya asilimia 20 kila mwaka katika mfuko wa bima wa NHIF. Aidha, Waziri Mchengerwa amesema kuwa serikali imejipanga katika kujikinga na magonjwa hayo yasiyokuwa ya kuambukiza huku akimpongeza Rais Samia kwa kufanikisha kupeleka vifaa tiba mbalimbali katika vituo vya afya ili kusaidia kuwafikishia huduma bora ya afya wananchi. Kwa upande wake mkur...

DG TASAC: KUKAMILIKA KWA MV LIEMBA KUTAIMARISHA BIASHARA, USAFIRI NA UCHUMI KIGOMA

 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC), Bw. Mohamed Salum, amesema kukamilika kwa ukarabati wa meli ya MV Liemba kutaimarisha huduma za usafiri wa majini, kuchochea biashara na kuharakisha maendeleo ya uchumi wa Mkoa wa Kigoma na ukanda mzima wa Ziwa Tanganyika. Bw. Salum amesema hayo leo, tarehe 23 Juni, 2026 alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ukarabati wa meli hiyo katika Bandari ya Kigoma, ikiwa ni sehemu ya shughuli za Maadhimisho ya 16 ya Siku ya Mabaharia Duniani yanayoendelea mkoani humo. Amesema wananchi wanaoishi katika maeneo yanayozunguka Ziwa Tanganyika wanategemea kwa kiwango kikubwa usafiri wa majini kwa shughuli za biashara, usafirishaji wa bidhaa na huduma za kijamii, hivyo kukamilika kwa MV Liemba kutaboresha huduma hizo na kuongeza ufanisi wa usafiri salama na wa uhakika. "MV Liemba ni meli yenye umuhimu mkubwa kwa wananchi wa ukanda wa Ziwa Tanganyika. Kukamilika kwake kutaimarisha usafiri salama, kurahisisha biashara, kuunganisha ...

KATAMBI ATOA WITO KWA JAMII KULINDA MAADILI, ASEMA SHERIA ZITACHUKUA HATUA DHIDI YA UHALIFU WA KIMAADILI

 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi ametoa wito kwa Watanzania kushiriki kikamilifu katika kulinda maadili, uzalendo na utamaduni wa taifa, akisisitiza kuwa Serikali haitasita kuchukua hatua kali dhidi ya makosa yanayohusiana na mmomonyoko wa maadili katika jamii. Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Jun 23,2026 Jijini Dodoma kuhusu ongezeko la matukio yanayohusiana na maadili mitandaoni na katika jamii, Katambi amesema kuwa Sheria ya Kanuni ya Adhabu ina vifungu vinavyohusiana na makosa dhidi ya maadili ya jamii na kwamba Serikali inaendelea kuzitekeleza kikamilifu. Amesema baadhi ya makosa hayo ni pamoja na vitendo vya kuingilia maumbile kinyume cha sheria, ubakaji, ulawiti, ukahaba pamoja na makosa mengine ya ukatili wa kijinsia na uvunjifu wa amani, akibainisha kuwa vyote vinaainishwa kisheria na vinachukuliwa hatua. Katambi amesisitiza kuwa ongezeko la maudhui yasiyofaa katika mitandao ya kijamii ni changamoto inayohitaji ushirikiano wa jamii, wazazi, taasisi...

MAYEYE:UPINZANI SI KUPINGA KILA KITU, BAJETI INAMENGI YA KUWANUFAISHA WANANCHI

 Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kupitia chama Cha ACT WAZALENDO  kiza Mayeye, amesema uamuzi wake wa kuipigia kura ya "Ndiyo" Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka wa fedha 2026/2027 umetokana na kutanguliza maslahi ya wananchi, akisisitiza kuwa jukumu la mbunge wa upinzani si kupinga kila jambo linaloletwa na Serikali, bali kuchambua, kushauri na kukosoa pale inapohitajika. Akizungumza leo  Jun 23,2026 katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma baada ya Bunge kupitisha bajeti hiyo, Mayeye amesema si mara yake ya kwanza kuunga mkono bajeti, akieleza kuwa hata alipokuwa mbunge katika Bunge la mwaka 2015 hadi 2020 aliwahi kufanya hivyo kwa kuzingatia maslahi ya wananchi aliokuwa anawawakilisha. "Kwa sababu mimi ni mpinzani, haimaanishi lazima nipinge kila kitu. Kazi yangu kama mbunge ni kuwatetea wananchi, kuishauri Serikali, kuielekeza na pale panapohitajika kuikosoa kwa lengo la kuboresha huduma na maendeleo," amesema. Mayeye amesema katika mjadala wa bajeti alitoa mapen...

SIMAI:WATU WAZIMA WAMEELEWA NILICHOSEMA KUHUSU YUDA

 Mbunge wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mohamed Simai Said, amesema Watanzania wameelewa vyema kauli yake kuhusu Yuda aliyotoa bungeni, akisisitiza kuwa suala hilo ni la zamani na sasa anataka kuangazia utekelezaji wa bajeti na maendeleo ya taifa. Akizungumza na waandishi wa habari leo Jun 23,2026 Bungeni Jijini Dodoma Simai amesema ni kawaida kwa wabunge kutofautiana na kukubaliana katika mijadala ya bunge, lakini mwisho wa siku wote hufanya kazi kwa lengo la kuwatumikia wananchi. Amesema anaamini Watanzania ni watu wazima na wameitafsiri kwa usahihi kauli yake kuhusu Yuda, hivyo hakuna sababu ya kuendelea kujadili suala hilo. "Ninaamini Watanzania ni watu wazima na wameelewa nilichosema kuhusu Yuda. Jambo hilo lilishapita, na kama nilivyofundishwa shuleni, historia ni somo linalohusu mambo yaliyopita," amesema. Simai aliongeza kuwa kwa sasa kipaumbele chake ni kusimamia utekelezaji wa bajeti, kumshauri Rais na Serikali, pamoja na kushiriki katika kuwaletea wananchi maend...