Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (DPP) nchini Kenya imeidhinisha kufunguliwa kwa mashtaka dhidi ya wanafunzi Sita wanaotuhumiwa kuhusika na tukio la moto lililotokea katika shule ya Utumishi Girls Academy, Kaunti ya Nakuru, tarehe 28 Mei 2026. Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Ofisi ya DPP tarehe 23 Juni 2026, faili la uchunguzi wa awali lililowasilishwa na Idara ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) limefanyiwa tathmini ya kina na kubaini kuwepo kwa ushahidi wa kutosha wa kuendelea na hatua za kisheria dhidi ya watuhumiwa. DPP amesema kuwa wanafunzi wanaohusishwa na tukio hilo watakabiliwa na mashtaka 16 ya mauaji, yakitokana na vifo vya wanafunzi 16 vilivyoripotiwa kufuatia ajali hiyo ya moto iliyotikisa taifa la Kenya. Katika taarifa hiyo, DPP ameonesha wasiwasi mkubwa kuhusu ongezeko la matukio ya uchomaji moto na vitendo vingine vya uhalifu vinavyoripotiwa katika taasisi za elimu nchini humo. Aidha, amesisitiza kuwa watu wote watakaobainika kuhusika na makosa...
Marato tv - Sauti ya Jamii