📌Mamia wajitokeza 📌Waipongeza Serikali kwa mkakati huo Wananchi Wilayani Karatu Mkoani Arusha wamejitokeza kwa wingi kujipatia majiko ya gesi ya kilo sita (LPG) yanayotolewa na Serikali kwa kushirikiana na Kampuni ya Lake Gas kwa bei ya ruzuku ya 50%. Wakizungumza kwa nyakati tofauti Desemba 7, 2024 wananchi hao wameipongeza Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuja na mkakati huo ambao wamesema utawasaidia kupunguza gharama walizokuwa wakitumia kununua mkaa. Mkazi wa Kata ya Qurus, Neema Alfred amesema mkakati huo wa Serikali wa kusambaza majiko kwa bei ya ruzuku unakwenda kuwapunguzia adha ya kutembea mwendo mrefu kusaka kuni. "Kijijini kwetu kuni hazipatikani ni hadi tutembee umbali mrefu; kwahiyo kupata haya majiko ya gesi na kwa bei nafuu ni neema kwetu," amesema Neema. Elizabeth Fikalala kutoka Kiiiji cha Bashay alisema kijijini hapo upatikanaji wa kuni ama mkaa ni mgumu na kwamba wanalazimika kutumia gharama kubwa kunua mkaa hivyo ujio wa mradi huo n...
Marato tv - Sauti ya Jamii