Skip to main content

Posts

Showing posts from December 7, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Karatu Wachangamkia Majiko ya Ruzuku

📌Mamia wajitokeza 📌Waipongeza Serikali kwa mkakati huo Wananchi Wilayani Karatu Mkoani Arusha wamejitokeza kwa wingi kujipatia majiko ya gesi ya kilo sita (LPG) yanayotolewa na Serikali kwa kushirikiana na Kampuni ya Lake Gas kwa bei ya ruzuku ya 50%. Wakizungumza kwa nyakati tofauti Desemba 7, 2024 wananchi hao wameipongeza Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kuja na mkakati huo ambao wamesema utawasaidia kupunguza gharama walizokuwa wakitumia kununua mkaa. Mkazi wa Kata ya Qurus, Neema Alfred amesema mkakati huo wa Serikali wa kusambaza majiko kwa bei ya ruzuku unakwenda kuwapunguzia adha ya kutembea mwendo mrefu kusaka kuni. "Kijijini kwetu kuni hazipatikani ni hadi tutembee umbali mrefu; kwahiyo kupata haya majiko ya gesi na kwa bei nafuu ni neema kwetu," amesema Neema. Elizabeth Fikalala kutoka Kiiiji cha Bashay alisema kijijini hapo upatikanaji wa kuni ama mkaa ni mgumu na kwamba wanalazimika kutumia gharama kubwa kunua mkaa hivyo ujio wa mradi huo n...

Jinsi Mashine za Kusaga za Solar Zilivyo Suluhisho Mbadala wa Mashine za Mafuta Katika Gharama za Uendeshaji na Uhifadhi wa Mazingira

Na Emmanuel  Chibasa Mashine za kusaga ni vifaa vinavyotumika kusaga na kukoboa nafaka Kwa ajili ya kupata chakula kutoka Katika mazao mbalimbali kama vile mahindi, mihogo, ulezi, mtama, mpunga pamoja na bidhaa nyingine za kilimo. Kuna aina tofauti za mashine za kusaga nafaka ambazo pia zinatumia vyanzo tofauti vya uzalishaji wa umeme, ambazo ni mashine zinazotumia umeme wa gridi, mashine zinazotumia mafuta ya dizel pamoja na mashine zinazotumia nishati ya umeme jua yani Solar. Katika maeneo ya vijijini bado kuna baadhi ya maeneo ambayo hayajafikiwa na umeme wa gridi, wananchi  wanatumia mashine za kusaga zinazotumia mafuta  zinaendeshwa kwa kutumia injini inayotumia mafuta ya diseli kama chanzo cha nguvu kuendesha mfumo wa magurudumu na gia zinazowezesha nafaka kukobolewa na kusagwa. Katika makala yetu leo, George Marato Tv Tunaangazia huduma za kusaga nafaka kwa mashine zinazotumia mafuta ya disel kwa kuangalia changamoto za gharama za uendeshaji na uhifadhi wa mazingir...

Uvccm Mkoa Kagera Yazindua na Kukabidhi Nyumba ya Mama Asimwe-Tuliahidi na Tumetekeleza

📍Izigo_Muleba  🗓️Trh. 07/12/2024 Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kagera Comrade Faris Buruhani,ameongoza  uzinduzi na makabidhiano ya  nyumba ya Mama Asimwe sambamba na  chumba kimoja cha biashara. Tukio hilo limefanyika leo tarehe 07/12/2024 katika kata ya Izigo, wilaya ya Muleba. Makabidhiano hayo yamekuja baada ya  ukamilishaji wa ahadi ya Umoja wa Vijana wa CCM mkoa wa Kagera kwa Mama Asimwe, ya kumboreshea mazingira yake ya kuishi kwa kumjengea nyumba ya kuishi na chumba kimoja cha biashara.  Ni miezi 6 sasa imepita tangu tukio la ajabu na la kikatili la Mauaji ya Mtoto asiye na hatia Asimwe Novat, aliyekuwa na ulemavu wa ngozi (Albino) litokee na kuacha simanzi kubwa kwa mwana dada Judith Richard (Mama Asimwe) na jamii nzima ya watanzania.   

Rais Mwinyi:Zanzibar Kuna Fursa za Uwekezaji

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amezikaribisha nchi za Umoja wa Ulaya, hususan sekta binafsi kuja Zanzibar kubaini fursa za uwekezaji ziliopo kwani kuna maeneo mengi hayajafikiwa hasa kwa sekta ya Uchumi wa Buluu kupitia Utalii, Bandari, Mafuta na gesi pamoja na sekta ya usafirishaji wa majini.  Rais Dk. Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 7 Disemba 2024, Ikulu Zanzibar alipozungumza na Ujumbe kutoka Kamisheni ya Umoja wa Ulaya ukiongozwa na Bi. Rita Laraujinha Mkurugenzi Mwendeshaji wa masuala ya nje, Kanda ya Afrika waliomtembelea. Aidha Rais Dk.Mwinyi amesema Zanzibar inadhamiria kuwa na umeme wa uhakika kutokana na kutanuka kwa shughuli za uchumi, miradi mikubwa ya maendeleo, ongezeko la hoteli za kitalii na kasi ya uwekezaji inayokuwa kila siku. Rais Dk. Mwinyi ameeleza kwa muda mrefu Zanzibar imekua ikipokea megawatt 100 za umeme kutoka Tanzania Bara kupitia waya za chini ya bahari ambao kwa sasa hautoshelezi, hivyo kuna kila sababu y...

Waziri Aweso anadi Miradi ya Maji Korea

Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa H. Aweso (Mb) ametembelea na kufanya mazungumzo na Benki ya EXIM ya Korea ambayo imefadhili utekelezaji wa miradi ya Majitaka nchini Tanzania yenye jumla ya Dola za Kimarekani Milioni 248.3 (Mkoa wa Dar es Salaam 90 $US milioni, Dodoma 70 $US million; na Iringa 88.3 $US million).  Katika mazungumzo hayo, Makamu wa Rais wa Benki hiyo amesema kupitia EDCF na Mifuko mingine Serikali ya Korea itaendelea kuisapoti Serikali ya Tanzania kupitia Sekta ya Maji katika uwekezaji zaidi wa utekelezaji wa Miradi ya Maji. Utelezaji wa miradi hiyo utaimarisha huduma za Usafi  wa Mazingira, kuondoa na kutibu majitaka. Vilevile, Tanzania imepata msaada wa Dola za Kimarekani milioni 8 ambazo zitajenga mfumo wa kusimamia huduma za maji yaani Smart Water Management System (SWMS) katika Mamlaka ya Maji Iringa kutoka Korea Environmental Industry and Technology Institute (KEITI).  Pia, Kupitia mfumo huo, IRUWASA itakuwa Mamlaka ya Maji ya kwanza Nchi kutumia mfumo huo ...

Serikali Mkoani Mara yamshukuru Rais Dkt. Samia Ujio wa Madaktari Bingwa na Bobezi Kuhudumia Wananchi

Na Shomari Binda-Musoma SERIKALI mkoani Mara imemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa ujio wa madaktari bingwa na bobezi na kuweza kuwahudumia wananchi. Shukrani hizo zimetolewa na Katibu Tawala wa mkoa wa Mara Gerald Kusaya kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambi wakati wa kufunga kambi ya siku 5 ya madaktari hao. Akizungumza kwenye hafla ya shukrani kwa madaktari waliokuwa wameweka kambi kwenye hospital ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Kusaya amesema wananchi 2,244 wamefanikiwa kuonwa na kutibiwa. Amesema kati ya hao 74 wamefanyiwa upasuaji na 46 wamepewa rufaa ya kwenda hospital ya rufaa ya kanda Bugando kwa matibabu zaidi. Katibu Tawala huyo amesema kambi hiyo imefanikiwa kukusanya shilingi milioni 186 na kutoa shukrani kwa madaktari hao kutokana na kazi kubwa waliyoifanya. " Tunawashukuru sana madaktari kwa kazi kubwa na nzuri mliyoifanya kwa kuja na kufanikiwa kuwatibu wananchi hapa Mara. "Tunamshukuru pia Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kut...

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Katibu Msaidizi Ofisi ya Kimataifa ya Madawa ya Kulevya na Masuala ya Utekelezaji wa Sheria Maggie

 Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Katibu Msaidizi Ofisi ya Kimataifa ya Madawa ya Kulevya na Masuala ya Utekelezaji wa Sheria Maggie Nardi kwa ajili ya kuangalia namna bora ya kuimarisha ushirikiano katika masuala ya Usaidizi wa Kisheria na uhalifu ili kusaidia katika kupambana na uhalifu wa kupangwa wa kimataifa katika kanda. Akizungumza katika kikao hicho kilichofanyika Jijini Dar es salaam Disemba 06,2024 Mhe Sagini amesema kuwa Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kudhibiti wimbi la usafirishaji haramu wa Binadamu ikiwemo kutunga sheria ya kuzuia usafirishaji haramu wa binadamu, Kuanzishwa kwa Kikosi Kazi cha Ulinzi wa Watoto wa Usafirishaji Haramu wa Binadamu mwaka 2022 na hatua nyingi zaidi ikiwemo kuzinduliwa kwa Mwongozo wa Ulinzi na Utunzaji wa Mashahidi mnamo Mei 2023.  Sagini ameongeza kuwa mbali ya kuwepo kwa muendelezo wa mafunzo kwa waendesha mashtaka na wapelelezi bado nguvu kubwa inah...

Halmashauri ya Wilaya Misungwi yaweka Mikakati ya Kuongeza Ufanisi Kwenye Utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo

Wakuu wa vituo vya kutolea huduma za afya na Elimu, watendaji wa kata na wakuu wa idara Halmashauri ya Wilaya Misungwi Mkoani Mwanza wamenufaika na mafunzo yanayolenga kuongeza ufanisi kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2024/2025. Akizungumza wakati wa Mafunzo hayo,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Wilaya ya Misungwi Bw. Addo Missama ameeleza kuwa bila ya maadili mema na uwazi katika utendaji wa shughuli za Kiserikali ni vigumu kufikia malengo ya maendeleo endelevu.  Missama amesema kuwa ili kufikia malengo hayo,kila mmoja katika Serikali anapaswa kuwajibika katika kuhakikisha kuwa rasilimali za umma zinatumika kwa njia inayofaa na kwa manufaa ya wananchi wote. Naye Kamanda wa Takukuru Wilaya ya Misungwi Bi. Elly Makala amesema kuwa kuelekea maadhimisho ya sikukuu ya Maadili tarehe 10/12/2024 kuna umuhimu wa kuimarisha maadili katika utendaji wa majukumu ya kiserikali na jamii ikiwa ni pamoja na kuzingatia kanuni za maadili katika kazi zao ili kujenga ima...