Skip to main content

Posts

Showing posts from August 27, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Askari Polisi Moses Mwaulambo Atoa Elimu ya Kuzuia Uhalifu na Wahalifu Kupitia Polisi Jamii Cup 2024 Musoma

  Na Shomari Binda-Musoma VIJANA kutoka Wilaya ya Musoma Mkoani Mara, wametakiwa kuwa wa kwanza kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu ili jamii iweze kuishi salama na kushiriki shughuli za kiuchumi Ujumbe huo umetolewa  agosti 27 na Mkaguzi wa Polisi na askari Kata wa Kata ya Bweri Moses Mwaulambo, kwenye muendelezo wa mashindano ya Polisi Jamii Cup 2024 Wilaya ya Musoma Akizungumza na wachezaji wa timu ya Bweri na Mara Sport Mwaulambo, amesema mahala ambapo hakuna uhalifu shughuli za kiuchumi ikiwemo michezo ufanyika kwa ufanisi Amesema michezo kwa sasa ni sehemu kubwa ya uchumi na wachezaji wengi wanajipatia kipato hivyo ni vyema kushiriki michezo huku taarifa za uhalifu na wahalifu zikitolewa. Mwaulambo amesema wahalifu sio watu wazuri kwani wanaweza kufanya uhalifu wa wizi wa mali ambazo mwanamichezo amezitafuta hivyo ni vyema kumtolea taarifa. " Tuko hapa kwa ajili ya kushiriki michezo lakini tunapeana ujumbe wa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu kwenye maeneo yetu. ...

WATALII WA BRAZIL KUANZA KUMIMINIKA TANZANIA

  Nchi zinazoleta watalii kwa wingi na wameshangazwa zaidi na uzuri wa Tanzania na kushindwa kuwa katika nafasi ya kumi bora dunia kwenye sekta ya utalii. Mtazamo huo wa awali kabisa wa umetolewa na kundi la makampuni makubwa ya utalii na vyombo vya habari vya masuala ya safari waliofika nchini leo tayari kuitembelea na kuona uzuri wa Tanzania. Akizungumza na watendaji wa kampuni hizo takribani 12 kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam leo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi, amesema ujio wa makampuni hayo ambapo waandishi tu waliokuja nao watafikisha habari kwa Wabrazil takribani milioni 85, ni mwendelezo wa visheni ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyefanya filamu ya “Tanzania: The Royal Tour”kuitangaza zaidi nchi yetu. “Ujio wa wageni hawa ni utekelezaji wa visheni ya Mhe Dkt. Samia Rais wetu na utaona hapa kuna ushirikiano wa Wizara, Bodi ya Utalii na Ubalozi wetu wa Tanzania nchini Brazil katika kufanikisha hili,” alisema Dr. Abbasi. Naye B...

WALIOMCHINJA MELEMBE WA GGM NAO "WACHINJWA"

Mahakama Kuu Kanda ya Geita imewahukumu watuhumiwa watatu kunyongwa hadi kufa baada ya kuwatia hatiani kwa kosa la mauaji ya Milembe Suleiman (43), aliyekuwa mfanyakazi wa mgodi wa dhahabu Geita(GGML). Hukumu hiyo imetolewa na Jaji Mfawidhi Kelvin Mhina katika kesi namba 39 ya mwaka 2023, baada ya mahakama kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri bila kuacha shaka yoyote. Waliohukumiwa ni Dayfath Maunga (30), Safari Lubingo (54), na Genja Deus, ambao walitiwa hatiani kwa mauaji hayo yaliyotokea mnamo mwaka 2023. Hata hivyo, mshtakiwa wa nne katika kesi hiyo, Musa Lubingo, ameachiwa huru baada ya mahakama kutomtia hatiani. Katika hukumu yake, Jaji Mhina ameelezea kuwa mahakama imejiridhisha bila shaka kuwa washtakiwa watatu walihusika katika mauaji ya Milembe Suleiman, na hivyo wanastahili adhabu ya kifo kwa mujibu wa sheria za Tanzania. Ushahidi uliotolewa na upande wa Jamhuri ulionekana kuwa thabiti na wa kutosha kumtia hatiani kila mshtakiwa aliyepatikana na hatia. Ba...