Skip to main content

Posts

Showing posts from July 9, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

KAMISHNA WA UHIFADHI TANAPA AANZA KAZI KWA MAAGIZO SITA YA WAZIRI KIJAJI

 Na. Calvin Katera - Arusha. Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Ashatu Kijaji (Mb) ametoa maagizo sita kwa Kamishna wa Uhifadhi TANAPA Massana Mwishawa leo Julai 09, 2026, jijini Arusha alipokuwa akiongoza zoezi la uapisho kwa aliyekuwa Naibu Kamishna wa Uhifadhi baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan Julai 02, 2026 kuchukua nafasi ya Kamishna wa Uhifadhi (Mstaafu) CPA Musa Nassoro Kuji aliyemaliza muda wake. Akizungumza katika hafla ya uapisho huo Waziri Kijaji amemwelekeza Kamishna Mwishawa kusimamia miundombinu ya hifadhi, kuvutia wawekezaji, kubuni bidhaa mpya za utalii, kusimamia mapato, kuimarisha uhusiano na jamii zinazozunguka maeneo ya hifadhi bila kusahau nidhamu, uadilifu, weledi, ustawi wa watumishi na kusimamia maslahi yao kwa wakati. Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini TANAPA, Mkuu wa Majeshi (Mst.) Jenerali George Waitara alieleza kuwa Bodi itaendelea kutoa ushirikiano wa dhati na ushauri wakati wote ili kufanik...

CP KAVIRONDO ASISITIZA UBUNIFU NA UBORA KATIKA MIRADI YA UJENZI YA JESHI LA MAGEREZA

 Na. Ssgt Mawazo Mtondo - DODOMA. Kamishna wa Huduma za Urekebu Jeshi la Magereza, CP Amina Kavirondo, Julai 8, 2026, alifanya ziara ya kukagua maendeleo ya miradi mbalimbali ya ujenzi inayotekelezwa na Jeshi la Magereza Jiji la Dodoma. Katika ziara hiyo, CP Kavirondo alikagua eneo linalotarajiwa kujengwa Ofisi za Makao Makuu ya Jeshi la Magereza lililopo NCC Ntyuka lenye ukubwa wa hekari 7.3, eneo la ujenzi wa nyumba ya Mkuu wa Jeshi la Magereza lililopo Itega lenye ukubwa wa hekari 4 na eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za Makamishna lililopo Msalato.  Aidha, alikagua mradi wa ukarabati wa Gereza Maalum lililopo eneo la Isanga, mradi wa ujenzi wa Gereza Jipya linaloendelea kujengwa katika eneo la Msalato, ujenzi wa jukwaa la uwanja wa gwaride pamoja na jengo la kubadilishia nguo katika viwanja vya michezo vilivyopo eneo la Makao Makuu ya Jeshi la Magereza Msalato Jijini Dodoma. Akiwa katika ukaguzi wa ujenzi wa Gereza Jipya la Msalato, CP Kavirondo alisisitiza...

RC MTAMBI:ASIKILIZA KERO ZA WANANCHI WA SUGUTI NA KUZITATUA

 Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Kanali Evans Alfred Mtambi, ameendelea kusisitiza utatuzi wa kero za wananchi kwa vitendo baada ya kufanya mkutano wa hadhara na wakazi wa Kijiji cha Suguti, Kata ya Suguti, Halmashauri ya Wilaya ya Musoma, ambapo alisikiliza changamoto mbalimbali na kutoa maelekezo ya utekelezaji wa haraka. Akizungumza katika mkutano huo uliofanyika Julai 9, 2026, Mhe. Mtambi aliliagiza Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara kuanza taratibu za kuanzisha kituo kidogo cha polisi katika eneo la Suguti, kufuatia ombi la wananchi waliobainisha kuwa uwepo wa kituo hicho utasaidia kuimarisha ulinzi na usalama wa wakazi pamoja na mali zao. "Wananchi wanahitaji huduma za usalama karibu yao. Jeshi la Polisi lifanye taratibu za kuanzisha kituo kidogo cha polisi katika eneo hili ili kuongeza ufanisi wa ulinzi na usalama," amesema Mhe. Mtambi. Katika hatua nyingine, Mkuu huyo wa Mkoa aliunda kamati maalumu ya kuchunguza malalamiko ya uchafuzi wa mazingira katika Kitongoji cha Karusenyi,...

CCM AND ACT-WAZALENDO SIGN UNITY DEAL AS SAMIA, MWINYI PRAISE POLITICAL ACCORD

By Prosper Makene   Zanzibar, July 09, 2026– The Ruling Party, Chama Cha Mapinduzi (CCM) and ACT-Wazalendo have signed a unity agreement, paving the way for the implementation of a Government of National Unity in Zanzibar. The agreement was signed today at the State House Grounds in Zanzibar, following the Joint Statement of the Political Accord between the two parties.  The President of Zanzibar and Chairman of the Revolutionary Council, Dr. Hussein Ali Mwinyi said the deal demonstrates the commitment of political leaders to prioritize national interests. He noted that it will strengthen peace, unity, solidarity and development in Zanzibar. President Dr. Mwinyi stressed that the Government will continue to work with all stakeholders to ensure the process upholds stability, good governance and sustainable development. The President of the United Republic of Tanzania, Dr. Samia Suluhu Hassan, also commended the accord. She said it opens a new chapter in strengthening unity...

MWENYEKITI WA SERIKALI AFUNGWA MIAKA MITATU KWA KUWEZESHA RAIA WA BURUNDI KUWA MTANZANIA

  Na Angela Sebastian ;Kagera   Mahakama ya Wilaya ya Karagwe imemtia hatiani Mwenyekiti wa Kitongoji cha Chagati, Robson Andrea Nganshinga, kwa kosa la rushwa baada ya kubainika kuwa alitoa barua ya utambulisho iliyomwonyesha mtu aliyedaiwa kuwa raia wa Burundi kuwa ni Mtanzania ili apate ajira katika Kiwanda cha Kukoboa Kahawa (KDCU). Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Mwandamizi (SRM), Charles Ngonyani, katika shauri la rushwa namba 15343/2026. Akizungumza leo mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Kagera, Ismail Bukuku, amesema mshtakiwa alishtakiwa kwa kosa la rushwa kinyume na kifungu cha 15(1)(b) na (2) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCA), Sura ya 329, Toleo la Mwaka 2023. Bukuku alisema uchunguzi ulionyesha kuwa Nganshinga aliidhinisha barua ya kumtambua Fabuan John, anayefahamika pia kwa jina la Dusabimana Fabiice, kuwa ni mkazi na raia wa Tanzania, huku akijua kuwa alikuwa raia wa Burundi. Amesema lengo la barua hiyo lilikuwa kumwezesha mtu huyo kupata aji...

RAIS DKT. MWINYI: TAMKO LA PAMOJA CCM NA ACT-WAZALENDO LAFUNGUA NJIA YA UTEKELEZAJI WA SERIKALI YA UMOJA WA KITAIFA

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema Tamko la Pamoja kati ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ACT-Wazalendo linafungua njia ya utekelezaji wa uundaji wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa na kuimarisha amani, umoja, mshikamano na maendeleo ya Zanzibar. Rais Dkt.Mwinyi ameyasema hayo baada ya kushuhudia utiaji wa saini wa ajenda zilizokubaliwa kwa pande zote mbili kwa ajili ya kufanyiwa kazi kufuatia Tamko la Pamoja la Muafaka wa Kisiasa Zanzibar baina ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na ACT-Wazalendo katika Viwanja vya Ikulu Zanzibar leo tarehe 09 Julai, 2026. Aidha, Rais Dkt. Mwinyi amesema maridhiano hayo yanaonesha dhamira ya viongozi kuweka mbele maslahi ya taifa, huku akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wote kuhakikisha mchakato huo unadumisha utulivu, utawala bora na maendeleo endelevu. Halikadhalika, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepongeza hatua hiyo akieleza kuwa mar...

KAGERA YAONGEZA ULINZI YA EBOLA,SHULE ZAAGIZWA KUPIMA JOTO LA WANAFUNZI WANAOREJEA KUTOKA LIKIZO

Na Angela Sebastian, Bukoba Afisa Afya wa Mkoa wa Kagera, Yassin Mwinori, amewataka wakuu wa shule na walimu wakuu wa shule zote mkoani humo kuhakikisha wanafunzi wote wanaorejea shuleni kutoka likizo wanapimwa joto la mwili mara wanapowasili, ikiwa ni sehemu ya hatua za awali za kuzuia kuingia na kusambaa kwa ugonjwa wa Ebola. Mwinori ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akitoa elimu ya afya kwa wananchi katika maeneo mbalimbali yenye mikusanyiko ikiwemo zahanati, vituo vya afya na maeneo ya mipakani Amesema licha ya ugonjwa wa Ebola kuripotiwa katika baadhi ya nchi jirani, Mkoa wa Kagera bado uko salama na hakuna kisa chochote kilichothibitishwa hadi sasa. Amesisitiza kuwa kutokana na mwingiliano mkubwa wa watu kati ya Tanzania na Uganda, hususan wanafunzi wanaovuka mpaka kwenda kusoma pande zote mbili, ni muhimu kwa shule kuchukua tahadhari za ziada ili kuzuia uwezekano wa maambukizi. "Kwa sasa shule zimefunguliwa kuna watoto wa Tanzania wanaosoma Uganda na wa Uganda wanaosoma Tanza...