Skip to main content

Posts

Showing posts from January 19, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Ghana na Tanzania Zaendelea Kuimarisha Ushirikiano wa “local Content” Katika Sekta ya Madini

Accra, Ghana Nchi za Ghana na Tanzania zinaendelea kuimarisha ushirikiano wa kitaasisi katika utekelezaji wa sera za Ushirikishwaji wa Wazawa katika Sekta ya Madini (Local Content), kwa lengo la kuongeza ushiriki wa wananchi wa ndani katika minyororo ya thamani ya madini, kuimarisha uwezo wa taasisi za ndani na kuhakikisha manufaa ya kiuchumi yanabaki ndani ya nchi. Hayo yamebainishwa katika ziara rasmi ya kubadilishana uzoefu kati ya wawakilishi wa Tume ya Madini ya Tanzania na Tume ya Madini ya Ghana, iliyolenga kujifunza na kushirikishana mbinu bora, sera na mifumo ya utekelezaji wa Local Content katika sekta ya madini. Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini, Dkt. Theresia C. Numbi, amesema kuwa sera ya Local Content si takwa la kisheria pekee, bali ni nyenzo muhimu ya kuchochea maendeleo ya taifa, ujenzi wa viwanda na uwezeshaji wa kiuchumi kwa wananchi. “Ningependa kusisitiza kuwa Maudhui ya Ndani katika sekta ...

Waziri wa Ulinzi Akutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama

waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Mheshimiwa Dkt Rhimo Nyansaho (mb), tarehe 19 January,2026 amekutana na kamati ya kudumu ya bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mambo ya nje, ulinzi na usalama maarufu ikijulikana kama NUU katika ofisi za Bunge jijini Dodoma kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Kikao hicho kati ya waziri wa ulinzi na JKT na kamati ya kudumu ya bunge inayoongozwa na mwenyekiti wake, Mheshimiwa Najma Murtaza Giza na makamu mwenyekiti wake Mheshimiwa Pascal Inyasi Chinyele ilihusisha kamati hiyo ya Bunge kupewa taarifa ya majukumu na muundo wa wizara ya ulinzi na JKT inayoongozwa na Mhe.Dkt.Rhimo Nyansaho aliyeteuliwa Tarehe 17 Novemba 2025 na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga Taifa.

Waziri wa Ulinzi Akutana na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama

waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Mheshimiwa Dkt Rhimo Nyansaho (mb), tarehe 19 January,2026 amekutana na kamati ya kudumu ya bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania ya mambo ya nje, ulinzi na usalama maarufu ikijulikana kama NUU katika ofisi za Bunge jijini Dodoma kwa ajili ya kuwasilisha taarifa ya wizara ya ulinzi na jeshi la kujenga Taifa Kikao hicho kati ya waziri wa ulinzi na JKT na kamati ya kudumu ya bunge inayoongozwa na mwenyekiti wake, Mheshimiwa Najma Murtaza Giza na makamu mwenyekiti wake Mheshimiwa Pascal Inyasi Chinyele ilihusisha kamati hiyo ya Bunge kupewa taarifa ya majukumu na muundo wa wizara ya ulinzi na JKT inayoongozwa na Mhe.Dkt.Rhimo Nyansaho aliyeteuliwa Tarehe 17 Novemba 2025 na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga Taifa.

Prof. Shemdoe Aelekeza Ujenzi Wa Maegesho ya Magari Pembezoni Mwa Mradi wa Stendi ya Mabasi Kihonda

Na OWM - TAMISEMI Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ameitaka Manispaa ya Morogoro kuona uwezekano wa kujenga sehemu maegesho ya magari pembezoni mwa Mradi wa Stendi ya Mabasi Madogo ya Kihonda inayojengwa kupitia mradi wa TACTIC, ili maegesho hayo yawe ni chanzo kipya cha mapato ya manispaa hiyo. Prof. Shemdoe ametoa wito huo kwa uongozi wa Manispaa ya Morogoro, mara baada ya baada ya kumaliza ukaguzi wa ujenzi wa mradi wa Stendi ya Mabasi Madogo Kihonda, stendi ambayo inajengwa karibu na Stesheni ya SGR ya Jakaya Kikwete Morogoro. “Kuna watu wanatoka mbali wanakuja Stesheni ya Jakaya Kikwete ili waende Dar es Salaam na kurudi jioni lakini wakifika hapo stesheni wanakuta maegesho ya magari yamejaa, hivyo manispaa jengeni maegesho ya magari ambayo yatawaingizia kipato,” ameelekeza Prof. Shemdoe. Prof. Shemdoe aitaka Manispaa hiyo ya Morogoro kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ili kurahisisha...