Ni shangwe tupu mapokezi ya Dk.Nchimbi wilayani Itilima akiendelea na mikutano kuomba kura kuelekea uchaguzi mkuu
Wakazi wa Kata ya Langabilili,wilaya ya Itilima mkoani Simiyu leo Jumanne Septemba 2,2025 wamejitokeza kwa wingi kumpokea na kumkaribisha kwa shangwe Mgombea Mwenza wa Urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiendelea na ziara mkoani Simiyu. Dkt.Nchimbi amepokewa kwa shangwe na Wananchi wa Langabilili,ndani ya jimbo la Itilima, huku wakionesha shauku kubwa ya kutaka kumuona na kumsikiliza katika mkutano wake wa Kampeni. Dk.Nchimbi ambaye alitokea mkoani Mara na sasa ameingia mkoa wa Simiyu kuendelea na mikutano ya kampeni katika Mkoa huo,baada ya kutoka Busega,Bariadi Vijijini na sasa ameingia jimbo la Itilima kufanya mkutano mkubwa wa Kampeni Akiwahutubia wananchi katika stendi ya Mabasi ya Langabilili, Itilima mkoani Simiyu, katika muendelezo wa mikutano yake ya Kampeni,Balozi Dkt.Nchimbi ambae ni Mgombea Mwenza wa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, pia alimnadi mgombea ubunge wa jimbo la Itilima,Njalu Daudi Silanga sambamba na Wagombea Ubu...