Skip to main content

Posts

Showing posts from September 6, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mahakama ya Hakimu Mkazi Yafunga Mwenendo wa Kesi ya Mauaji ya Mtoto Noela

Na Angela Sebastatian- Bukoba MAHAKAMA ya hakimu mkazi Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera imefunga rasmi mwenendo kabidhi kuhusu shauri namba 17740  linalowakabiri washitakiwa tisa akiwemo padri wa kanisa Katoliki pamoja na baba mzazi wa mtoto Noela Asimwe Novart (2.5) ambaye aliuawa na kisha kukatwa mikono yako na mwili kutelekezwa katika karavati. Waziri Magumbo mwendesha mashitaka wa mkoa wa Kagera kwa kushirikiana wa mawakili wenzake wanne wa serikali akiwemo Erick Mabagala  alisema kuwa kesi hiyo  ilifikishwa mbele ya hakimu Mkazi mfawidhi mahakama ya wilaya Bukoba Elipokea Yona kwa mara ya kwanza Juni 28 mwaka. Amesema Mei 30 mwaka huu mtoto Noela aliibwa na watu wasiojulikama ambao walifika nyumbani  kwao marehemu huyo na kumpola mikononi mwa mama yake kisha kutokomea kusikojulikana ambapo Juni 17mwaka huu mwili wa Noela ulipatikana ukiwa umetelekezwa katika karavati lililoko barabara ya Ruhanga ukiwa umekatwa mikono. Magumbo akisaidiana mawakili wanne wa Jamhuri ...

WAZIRI MKUU ASHIRIKI MBIO ZA HISANI ZA MAENDELEO BANK

  Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Septemba 07, 2024 ameshiriki katika mbio za hisani za Maendeleo Bank Marathon 2024 zilizoanzia na kuishia katika viwanja vya Greenpark garden Oysterbay jijini Dar es Salaam. Lengo la mbio hizo ni kukusanya zaidi ya shilingi milioni 200 kwa ajili ya kusaidia watoto wenye changamoto mbalimbali hapa nchini. Kauli mbiu ya mbio hizo ni “Hatua ya Faraja- Msimu wa Pili”.

Wanawake Wahimizwa Kujitokeza Kwenye Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Mpiga Kura Kuhakiki Taarifa Zao

Na Shomari Binda-Musoma WANAWAKE mkoa wa Mara wametakiwa kujitokeza kwenye zoezi la uboreshaji wa daftari la mpiga Kura kwa ajili kujiandikisha na kuboresha taarifa zao kwenye daftari la kudumu la wapiga kura. Kauli hiyo imetolewa Leo Septemba 6, 2024 na Mjumbe wa Baraza Kuu la Jumuiya ya Wanawake wa ( UWT) Taifa Rhobi Samwelly alipokuwa akizungumza na George Marato TV. Amesema siku zote wanawake wamekuwa mstari wa mbele kwenye masuala mbalimbali yakiwemo ya uchaguzi. Rhobi amesema katika zoezi hili la uboreshaji wa daftari kwa mkoa wa Mara lililoanza septemba 4 hadi 10 wanawake wote wenye sifa wanapaswa kujitokeza kushiriki zoezi hilo. Mjumbe huyo wa baraza la UWT Taifa amesema wanawake wasisubiri hadi siku ya mwisho bali wajitokeze sasa kujiandikisha na kuboresha taarifa. Amesema bila kujiandikisha na kuboresha taarifa huwezi kushiriki kikamilifu zoezi la uchaguzi pale litakapofika. " Zimebaki takribani siku chache kuhitimisha zoezi la uboreshaji daftari la wapiga kura kwenye mk...

Wananchi Nyatwali Wamuahidi Rc Mtambi Matumizi Sahihi ya Fedha za Fidia

Na Shomari Binda- Bunda WANANCHI wa  Kata ya Nyatwali wilayani Bunda  wamemuahidi mkuu wa mkoa wa Mara Kanali Evans Mtambj matumizi sahihi ya fedha za fidia kupisha shughuli za uhifadhi. Ahadi hiyo wameitoa kwenye Kata hiyo wakati wakipokea mfano wa hundi ya malipo hayo yanayotolewa na serikali kupitia Shirika la Hifadhi ya Taifa (TANAPA) Wamesema fedha watakazolipwa watazielekeza kwenye kupata makazi mapya na kuweka mazingira mazuri ya maisha kwenye maeneo watakayoamia Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Nzugumi Mayala amesema ushauri wa mkuu wa mkoa wataufanyia kazi baada ya kupata fedha hizo. Mkuu wa Mkoa  wa Mara Kanali Evans Mtambi amezindua ulipaji fidia kwa wananchi wanaohamishwa kutoka kata ya Nyatwali wilayani Bunda. Akizindua ulipaji wa fidia hizo katani hapo RC Mtambi amewataka wananchi wanaopata malipo hayo kuondoka katika eneo hilo na kutumia fedha hizo vizuri kwa maslahi ya familia zao. “Akili zenu zianze kufikiria jinsi mtakavyopata faida ku...

Wizara ya Katiba na Sheria Yazindua Rasmi Kituo Cha Huduma Kwa Mteja

  Na Elizabeth Zaya WIZARA ya Katiba na Sheria, imezindua rasmi Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Huduma za Kisheria ambacho kitakuwa kinapokea malalamiko, hoja maswali na tuhuma za rushwa kwa njia ya simu kutoka kwa wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya nchi na kutatuliwa moja kwa moja na wataalamu. Kituo hicho kimezinduliwa leo jijini Dodoma na Waziri wa Katiba na Sheria, Prof. Palamagamba Kabudi, hafla iliyoshirikisha viongozi  wadau mbalimbali pamoja na wananchi na kwamba kituo hicho ni sehemu ya Kampeni ya Kitaifa ya Huduma za Kisheria ya Mama Samia. Prof.Kabudi alisema Wizara ya Katiba na Sheria ni miongoni wiazara  vinara  zinazotekeleza kwa vitendo falsafa za Rais Samia Suluhu Hassan za 4R, ambazo ni maridhiano, ustahilmilivu, mabadiriko na kujenga upya. “Na kupitia kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia, imefanikiwa kupita katika mikoa saba na hivi karibuni itaanza kuendelea katika mikoa mingine iliyobaki,”alisema Prof.Kabudi. Amesema wizara imeanzisha kitu...

Rais Dkt. Samia Akutana na Watanzania Wanaoishi Nchini China

  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akutana na Watanzania wanaoishi nchini China (Diaspora) wakiwemo wafanyakazi, wanafunzi na wafanyabiashara,  Jijini Beijing tarehe 06 Septemba, 2024.

SERIKALI YAAGIZA UJENZI WA SKIMU YA MKOMBOZI UKAMILIKE IFIKAPO OKTOBA 30

Wakandarasi wanaotekeleza Mradi wa ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji ya Mkombozi iliyopo Mkoani Iringa wametakiwa kukamilisha ujenzi wa Skimu hiyo ifikapo mwishoni mwa mwezi ujao.  Agizo hilo limetolewana Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji(NIRC)Raymond Mndolwa wakati wa vikao kazi baina ya Uongozi wa Tume hiyo na Wakandarasi hao Mkoani Iringa. Mndolwa amewataka wakandarasi wa kampuni ya ndani ya Cimfix&engineering pamoja na Kampuni ya CRJE ya nchini China wanaotekeleza wa Mradi wa ujenzi wa Skimu ya Mkombozi kufanya kazi usiku na mchana ili kuwezesha mradi huo kukamilika kwa wakati na hatimaye kuwezesha uwekezaji mkubwa unaofanywa na serikali kunufaisha wakulima kuanzia Msimu Ujao wa Kilimo.  Katika vikao Kazi hivyo,Wakandarasi waliwasilisha mkakati wa kumaliza mradi kwa wakati ikiwemo kuhakikisha kazi zilizosalia zinakamilika oktoba 30 Mwaka huu.  Wajumbe walipitia mkakati huo na kutoa maoni na maazimio, huku mkandarasi akikubali kufanya marekebisho ya mpan...

TEKELEZENI KWA VITENDO FALSAFA YA 4R YA RAIS DKT. SAMIA-MAJALIWA

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka Maafisa waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na viongozi wa vyombo vya usalama wa Wizara hiyo kutekeleza kwa vitendo na kuiishi falsafa ya R nne (4R) ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kufikia malengo yaliyokusudiwa. Amesema kuwa ni muhimu kuifahamu vyema falsafa hiyo ya Rais Dkt. Samia na kuitekeleza kwa vitendo. “Nina imani kubwa kwamba uongozi wa juu wa Wizara umeielewa vizuri falsafa hiyo, na semina hii elekezi ni ushahidi tosha wa kuitekeleza kwa vitendo” Amesema hayo leo (Ijumaa, Septemba 06, 2024) wakati alipofungua Semina elekezi kwa viongozi waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi iliyofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Weruweru River Lodge, mkoani Kilimanjaro. “Falsafa hii inajikita katika masuala ya Maridhiano (Reconciliation), Ustahamilivu (Resilience), Mageuzi (Reforms), na Kujenga upya Taifa (Rebuilding). Hivyo, nitoe wito kwa washiriki ambao ni Maafisa Waandamizi wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama chini ya...

DARAJA LA MAGUFULI MBIONI KUKAMILIKA

  Ujenzi wa Daraja la JP MAGUFULI unaotekelezwa na serikali katika ziwa Victoria eneo la kigongo-Busisi Mkoani Mwanza kwa gharama ya zaidi ya shilingi billioni mia saba umefikia asilimia 90.5 Daraja hilo la kwanza kwa urefu katika nchi za afrika mashariki na kati litakuwa kiungo muhimu cha usafiri na usafirishaji baina ya mikoa ya kanda ya ziwa pamoja na mataifa Jirani ikiwemo UGANDA,BURUNDI,RWANDA na JAMHURI YA KIDEMOKRASIA YA CONGO. Meneja wa wakala wa Barabara nchini(Tanroads)Mkoa wa Mwanza Mhandisi AMBROSE PASCHAL amesema kuwa Daraja la JP MAGUFULI linajengwa kwa kutumia Teknolojia kisasa ya ujenzi wa madaraja marefu Juu ya Maji. Mhandisi PASCHAL amesema kuwa Daraja hilo litakuwa na uwezo wa kubeba Tani 120 za Mizigo na linatarajiwa kuanza kutoa huduma ifikapo mwishoni mwa mwaka huu. Daraja la JP MAGUFULI linajengwa na Mkandarasi wa kampuni ya CHINA CIVIL ENGINEERING CONSTRUCTION CORPORATION(CCECC)ya nchini china ambayo imeeleza kuvutiwa na mazingira mazuri ya kisiasa pamoja na...

ACT-WAZALENDO Yajipanga Kuikabili CCM Zanzibar

Mwenyekiti wa ACT- Wazalendo Taifa ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mheshimiwa Othman Masoud Othman, Leo Ijumaa Septemba 06, 2024, amefanya Mkutano Maalum na Waandishi wa Habari, hapo katika Ukumbi wa Golden Tulip Kiembesamaki, Mkoa wa Mjini-Magharibi Unguja. Mkutano huo umelenga Kutangaza Baraza Jipya Teule la Mawaziri Kivuli wa Chama hicho, kwa Upande wa Zanzibar. Uwepo wa Baraza hilo ni kwamujibu wa Miongozo ya Katiba ya Zanzibar, inayopendekeza kuwepo kwa 'Sauti ya Wananchi kupitia Upande wa Upinzani, pamoja na Matakwa ya ile ya ACT-Wazalendo, inayoelekeza kuundwa kwa Chombo hicho Wasemaji wa Sekta mbali mbali za Maendeleo ya Nchi, kupitia Kambi hiyo. Akitoa Hotuba yake kabla kutangaza Viongozi walioteuliwa Kuongoza katika Baraza hilo, Mheshimiwa Othman amesema uteuzi huo umezingatia taaluma, weledi katika eneo husika, maarifa na uzoefu, kwa  kuzingatia Sera za Sasa za Chama na Ahadi zake (The Brand Promises), pamoja na kuzitambua na kuzitatua changamoto za w...

TANAPA Kutumia Kampeni ya Twende Zetu Kileleni 2024 Kuhamasisha Utalii wa Ndani

SHIRIKA la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) kwa kushirikiana na makampuni ya waongoza watalii nchini imepanga kuwapeleka watanzania zaidi ya 500 katika kilele cha Mlima Kilimanjaro kusherehekea siku ya uhuru kupitia kampeni ya “Twenzetu Kileleni 2024” ikiwa ni msimu wa Nne wa Kampeni hiyo ikiwa na Kauli mbiu isemayo “Stawisha Uoto wa Asili Tanzania,Okoa Barafu ya Mlima Kilimanjaro kampeni ambayo imezunduliwa leo mpaka december 4, 2024. Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi na Maendeleo ya Biashara wa TANAPA, Jully Lyimo amewaeleza wanahabari katika mkutano na vyombo vya Habari uliofanyika katika ofisi za TANAPA jijini, Dar es Salaam leo kuwa lengo la kampeni hii ni kusherehekea miaka 63 ya Uhuru, tukio ambalo ni la kihistoria hufanyika kila mwaka ifikapo December  9. “Katika sura ya Utalii, TANAPA imekuwa ikitumia fursa hii ya maadhimisho ya siku ya uhuru kuhamasisha watanzania kupanda mlima Kilimanjaro na kutangaza vivutio vinavyopatikana katika hifadhi hii kupitia kampeni ya “Twenzetu ...

RAIS SAMIA AKUTANA NA WAWEKEZAJI WAKUBWA NCHINI CHINA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kuzungumza na Wawekezaji na Viongozi wa Makampuni mbalimbali ya China Academy of Space Corporation (CASC), China Electronics Corporation, Transsion Group, Weihua Group, China Railway Construction Corporation (CRCC) pamoja na Acme Consultant Engineers PTE Limited na CND jijini Beijing, China tarehe 06 Septemba, 2024.   Mhe. Rais yupo nchini China kwenye ziara ya kikazi ambapo alishiriki kwenye Mkutano wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC).