Jumla ya Wakazi 600 wa Kitongoji cha Makundusini, Kijiji cha Singu Kata ya Kukirango Wilaya ya Butiama mkoani Mara wamenufaika na Mradi wa Maji uliofanikishwa na aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Butiama Mhe. Jumanne Abdallah Sagini kupitia Taasisi ya Direct Aid Society Tawi la Tanzania kutoka Kuwaït. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mradi wa Kisima cha Maji chenye uwezo za kuzalisha zaidi ya lita 20000 kwa siku, Mgeni Rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Wilaya ya Butiama Mhe. Thecla Mkuchika amepongeza juhudi zilizofanywa na Mbunge Mstaafu wa Jimbo hilo Mhe. Jumanne Sagini kwa kitendo cha kuunga mkono Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika sera ya kumtua ndoo mama kichwani pia amesema mradi huo utapelekea kuondokana na magonjwa yanayosababishwa na matumizi ya maji yasiyo safi na salama. Kwa upande wake Naibu Mkurugenzi wa Taasisi ya Direct Aid Society Tawi la Tanzania kutoka Kuwaït Bw. Abdelhamid Ismail amesema kuwa taasisi ilianza kutoa hudu...
Marato tv - Sauti ya Jamii