Skip to main content

Posts

Showing posts from December 25, 2024

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Mkuu wa Mkoa Kagera atoa Zawadi ya Xmass kwa Watoto wa Mazingira Magumu

 Na Angela Sebastian ;Bukoba  MKUUU wa mkoa wa Kagera Hajat Fatma Mwassa ameunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan kwa kufanya tendo la uhuruma kwa watoto yatima,wanaoishi mazingira magumu na wenye uhitaji katika sikukuu ya Christmas. Hajat Mwassa amewaalika watoto zaidi ya 200 kutoka katika vituo vinne vya kulelea watoto yatima na wale wenye uhitaji vilivyoko Manispaa ya Bukoba ambapo amepika chakula na kisha kula nao mlo wa mchana lengo,likiwa ni kusherehekea sikukuu hiyo muhimu ili nao wajione kuwa wanayo haki ya kuungana na wengine wakati wa furaha. "Nimeamua kupika mwenyewe hapa Ikulu ndogo ya mkoa wa Kagera kisha kupakua,kula na kunywa na watoto hawa wenye uhitaji na yatima ili tufurahi wote katika sikukuu hii,maana tumezoea kubeba vyakula,nyama na vinywaji kupeleka vutuoni na kuacha lakini mimi nimeona tendo hilo la huruma nilitekeleze kwa njia hii"ameeleza Mwassa  Kwa upande wa mwenyekiti wa cha Mapinduzi (CCM) Wilay...

Zaidi ya watoto 50 wapokea Mahitaji ya Shule kutoka Taasisi ya Angeline

Taasisi ya The Angeline Foundation imekabidhi vifaa mbalimbali kwa ajili ya kuunga mkono juhudi mbalimbali anazozifanya Mhe Dkt.Angeline Mabula Mbunge wa Jimbo la Ilemela kwa kutoa vifaa na ufadhili Kwa watoto wanaoishi mazingira magumu pamoja na Yatima  Akipokea vifaa hivyo katika Bonanza la Krismass lililofanyika kwenye viwanja vya Furahisha Katibu wa Mbunge Ndugu Charles David ameshukuru taasisi ya The Angeline Foundation ambayo imekuwa ikifanya kazi kubwa sanaa kuunga mkono jitihada mbalimbali za Mhe Mbunge katika kuwatumikia wananchi.  Pamoja na hivi vifaa ambavyo siku ya leo tunavipokea n kuvitoa Kwa vijana hawa zaidi ya 50 ambao wanasoma Kwa ufadhili wa Mhe Dk Angeline Mabula Mbunge wa Jimbo la Ilemela leo tunapokea vifaa hivi Kristmass Bonanza ikiwa ni msimu wake wa nane tangu kuanzishwa Kwa taasisi hii imekuwa ikifanya kazi kubwa kutoa vifaa mashuleni , vifaa vya afya pamoja mahitaji mbalimbali . Akizungumza wakati wa kukabidhi vifaa hivyo Ndugu Ayubu Bariana mrat...