Skip to main content

Posts

Showing posts from May 3, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Rais Samia Amedhamiria Kuisogeza Serikali Kwa Wananchi-Mchengerwa

Na John Mapepele Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imedhamiria kwa dhati kuisogeza Serikali karibu zaidi na wananchi wake hasa wale walio na kipato cha chini katika maeneo ya vijijini na mijini ili kuwaletea maendeleo. Akizungumza kwenye Kongamano la Uchumi la Arusha leo Mei 3, 2025 jijini Arusha akiwa miongoni mwa watoa mada, Mhe. Mchengerwa amefafanua kwamba lengo kuu ni kuwakomboa wananchi kutoka katika mnyororo wa ukosefu wa taarifa, huduma na fursa, kwa kuwajengea uelewa, uwezo na maarifa ya msingi, sambamba na kuwawekea miundombinu inayowawezesha kushiriki kikamilifu katika kupanga na kutekeleza mipango yao ya maendeleo. “Tupo katika zama ambazo maendeleo hayategemei tena maamuzi ya viongozi wa kitaifa peke yao, bali yanategemea uwezo wa maeneo yetu ya mikoa na halmashauri zetu kuongoza kwa dira, maarifa na maamuzi ya kimkakati”...

Majaliwa: Wana - Luangwa hatuna deni na Mhe.Rais Dkt.Samia

  _▪️Asema ni kutokana na maendeleo yaliyopatikana kipindi cha uongozi wake_▪️ MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama Chama cha Mapinduzi, Waziri Mkuu na Mbunge wa Jimbo la Ruangwa, Kassim Majaliwa amesema kuwa Wilaya hiyo haina deni na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutokana na kazi kubwa ya kimaendeleo iliyofanyika katika sekta mbalimbali. Ameyasema hayo leo (Jumamosi, Mei 03, 2025) wakati akizungumza katika kikao kilichojumuisha wajumbe wa Mabaraza ya Jumuia za Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Ruangwa kilichofanyika katika Bwalo Shule ya Awali na Msingi ya Wonder Kids. Waziri Mkuu amesema kuwa katika kipindi cha kuanzia mwaka 2010 hadi sasa ujenzi wa vituo vya afya umeongezeka kutoka vituo 2 hadi 12 hali inayowezesha kusogeza huduma za afya karibu na wananchi. “Tulikuwa na zahanati 22 lakini sasa zimefikia 35, na jitihada bado zinaendelea.” Aidha, Waziri Mkuu amesema kuwa kwa kutambua umuhimu wa sekta ya elimu, Wilaya hiyo imewezesha kujenga shule za sekondari 30 kutoka shule...

Kiwanda Cha Nguzo za Zege Tabora Kuzalisha Ajira, Kukuza Uchumi wa Nchi

  📌 Dkt. Biteko aweka Jiwe la Msingi Ujenzi Kiwanda cha Nguzo za Zege 📌 Awataka wananchi Tabora kutogawanyika wakati Uchaguzi Mkuu 📌 Asema maono ya Rais Samia ni viongozi kuwasaidia wananchi Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa Kiwanda cha Kutengeneza Nguzo za Zege cha TCPM kutakidhi mahitaji ya Mkoa wa Tabora na maeneo mengine ya jirani na kukuza uchumi wa nchi. Kiwanda hicho kitakachokuwa na uwezo wa kuzalisha nguzo 120 kwa siku inadhihirisha kasi ya matumizi na uhitaji wa nguzo hizo za kisasa. Pia, makadirio yanaonesha kuwa, mahitaji yanaongezeka na hivyo kuongeza fursa kwa TCPM kulichangamkia soko hilo. Dkt. Biteko amesema hayo leo Aprili 3, 2025 mkoani Tabora mara baada ya kuweka jiwe  la msingi la ujenzi wa Kiwanda cha Kutengeneza Nguzo za Zege cha TCPM. “Niwapongeze uongozi wa Kampuni ya TCPM na wadau wengine kwa jitihada zenu za kusimamia ujenzi wa K...

Waziri Mavunde azindua mradi wa kihistoria wa vijana Nyamongo - Tarime

  ▪️Agawa Leseni za madini awamu ya kwanza kwa Vijana 2000 ▪️Ni utekelezaji wa Maagizo ya Mh. Rais Dkt. Samia ▪️Aupongeza mgodi wa Barrick North Mara kwa kutoa Leseni kwa Vijana wa Vijiji 13  ▪️Benki ya Dunia (WB) na Baraza la Dhahabu Duniani (WGC) waonesha dhamira kusaidia mradi *📍Tarime,Mara* Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde  amezindua mradi wa uchimbaji Madini ya dhahabu kwa vijana, wanawake na wenye ulemavu kwa kutoa leseni za uchimbaji mdogo wa madini ikiwa ni utekelezaji wa Programu ya Mining For a Brighter Tomorrow (MBT). Amezindua mradi huo leo Mei 03, 2025 katika viwanja vya shule ya sekondari Ingwe vilivyopo katika eneo la Nyamongo wilayani Tarime  Mkoa wa Mara ambapo ametoa leseni 48 za uchimbaji mdogo wa madini kwa wanufaika zaidi ya 2000 vijana, wanawake na wenye nahitaji maalumu. Akizungumza katika hafla hiyo amesema, Wizara ya Madini imekamilisha maandalizi ya Programu ya MBT ambayo itatekelezwa katika kipindi cha miaka mitano kuanzia mwaka 2025 ...