Skip to main content

Posts

Showing posts from April 28, 2025

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Majaliwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari Duniani

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Aprili 29, 2025 ni mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya uhuru wa vyombo vya habari, inayofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Grand Melia jijini Arusha  Maadhimisho hayo yanalenga kubadilishana mawazo na kufanya majadiliano kuhusu fursa na changamoto katika sekta ya habari.

RC Batlida azindua mbio za magari zinazoitwa "𝗗𝗔𝗥 𝗧𝗧 𝗗𝗥𝗔𝗚 𝗥𝗔𝗖𝗘

  Na Mashaka Mhando, Muheza  Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dkt. Batilda Burian, amezindua mashindano ya mbio za magari maarufu kama Dar TT Drag Race katika eneo la Kigombe, Wilaya ya Muheza. . Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mashindano hayo, Balozi Dkt. Batilda ameipongeza timu ya Dar TT kwa kuichagua Tanga kuwa mwenyeji wa mashindano hayo, akisema kuwa hatua hiyo itafungua fursa za kiuchumi kupitia sekta ya michezo. Balozi Dkt. Batilda amewakaribisha waratibu na wanamichezo wa mashindano ya aina hiyo kuendelea kuitumia barabara ya Tanga–Pangani kwa shughuli zao, akibainisha kuwa Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza fedha nyingi katika ujenzi wa barabara hiyo kama sehemu ya kukuza uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Tanga Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Zainabu Abdallah, amempongeza Mkuu wa Mkoa kwa kujitoa na kushirikiana kikamilifu katika kuendeleza michezo, hatua ambayo inaonesha dhamira ya dhati ya kumuunga mkono Rais Dkt. Samia...

Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ametuletea Benki ya Ushirika vijijini nchini Tanzania

  Chigaitan mapinduzi vijijini  Katika mapinduzi ya kimaendeleo nchini Tanzania Mh.Rais Dkt Samia Suluhu Hassan amewapelekea benk ya ushirika  watanzania vijijini. Anasema Dkt Samia Suluhu Hassan katika uzinduzi wa benki ya Ushirika "Benki ya ushirika ni kichocheo cha maendeleo hasa ya kilimo vijijini" Kwa mtaji wa zaidi ya Bilion 50 benki ya Ushirika imezinduliwa haya ni mapinduzi ya kihistoria katika historia ya ushirika nchini Tanzania Kwa mujibu wa chigaitan mapinduzi vijijini.  Taifa lolote lenye ushirika na makampuni imara ndiyo nguzo kuu ya uchumi wa taifa. Leo nchini Tanzania waziri mkuu Kasimu Majaliwa,  Waziri kijana Hussein Bashe(Mb)  akishirikiana na  Abdulmajid Mussa Nsekela, Mwenyekiti wa Kamisheni ya Tume ya Maendeleo ya Ushirika Tanzania wameongoza mapinduzi anayohubiri mwandishi mahiri wa mapinduzi vijijini nchini Tanzania CHIGAITAN Uchumi wa ushirika ni njia kuu ya mafanikio ya uchumi wa hasa watu wa vijijini nchini Tanzania.

Serikali yatatua mgogoro wa mwekezaji na wachimbaji wadogo Ifumbo Chunya - Mbeya

  ▪️Ni maelekezo ya Rais Dkt. Samia kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huo ▪️ Waziri Mavunde aelekeza Wanakijiji kupewa Leseni kuhalalisha uchimbaji wao ▪️Mwekezaji aruhusiwa kuendelea na uwekezaji kwa Leseni za eneo la Lupa Market ▪️Uchimbaji wa Eneo la Ifumbo wasimamishwa mpaka vibali vya Mazingira ▪️Naibu Waziri Khamis Chilo asisitiza utunzaji wa mazingira wa Mto Zira. 📍 Chunya, Mbeya. Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde ameeleza kuwa wananchi wa Kata ya Ifumbo Wilayani Chunya watapewa leseni 2 kati ya 14 za uchimbaji madini zinazomilikiwa na Kampuni ya G & I  katika bonde la Mto Zira na kutambulika rasmi kama wachimbaji halali ili wafanye shughuli za uchimbaji bila usumbufu ikiwa ni hatua ya utatuzi wa mgogoro baina  ya wananchi hao na mwekezaji. Amesema hayo jana Aprili 28, 2025 wakati akizungumza katika Mkutano wa hadhara na wananchi wa Kata na Kijiji cha Ifumbo Wilayani Chunya akiwa ameambatana na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe....

Wananchi wa Bwiregi wampongeza Sagini kwa Bil.15 iliyotumika kwenye miradi ya maendeleo

  Wananchi wa Kata ya Bwiregi wamempongeza Mbunge wa Jimbo la Butiama na Naibu Waziri Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini kwa kufanikisha Bilioni 1.5 ambayo ilitumika katika miradi mbalimbali ya maendeleo. Akizungumza kwenye mkutano na wajumbe wa CCM na wananchi katika Ziara ya Mbunge kwenye Vijiji vya Kitasakwa, Ryamisanga, Kamgendi na Masurura Diwani wa Kata ya Bwiregi Nyagheti Adam amesema kuwa ni muda wa kumpongeza mbunge kwa yale mema aliyofanya kwenye kata hiyo. "Wananchi hawa wameazimia kuwa Mhe. Sagini upewe maua yako uliahidi na ukaleta fedha nami nikawa kiungo muhimu katika kusukuma maendeleo hivyo naamini utarudi tena kwenye ubunge sioni kitu kinachokwamisha, niwaombe watu msirithi uadui wa mtu na ogopeni matapeli wanaokuja kukuambia Sagini na Nyagheti wamefanya nini wewe muulize pia amefanya nini," amesema Diwani Nyagheti. Naye Mbunge wa Jimbo la Butiama ambaye pia ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini amewashukuru wananchi na kuwaomba kuendelea...

Mbunge Ghati Chomete achangisha milioni 10 harambee kikundi cha wanawake Nyamongo

  Na Shomari Binda-Tarime MBUNGE wa viti maalum mkoa wa Mara Ghati Chomete amefanikisha kuchangisha zaidi ya milioni 10 kwenye harambee ya kikundi cha wanawake wajasiliamali Nyansembe kilichopo Nyamongo. Harambee hiyo imefanyika jana aprili 27,2025 huku ikihudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo wanaofanya kazi na kikundi hicho kutoka mgodi wa Barrick North Mara. Akizungumza na wana kikundi hao Mara baada ya kufanikisha kiasi hicho cha fedha amesema kiende kiwasaidie sehemu ya malengo yao waliyoyakusudia. Amesema ili kufikia malengo waliyoyakusudia wanapaswa kushirikiana zaidi na kufanya kazi kwa bidii ili kujiongezea kipato. Ghati amesema kwa kuwa lengo la kukusanya milioni 30 halikuweza kutimia wanapaswa kuandaa harambee nyingine na kuwaalika watu mbalimbali ili waweze kuwachangia. " Niwapongeze kwa hiki ambacho kimepatikana leo kwa malengo yenu mliyoyakusudia mnapaswa kuandaa harambee nyingine. " Lakini hiki ambacho kimepatikana leo kiende kikaongeze nguvu kwenye kazi zenu n...

Serikali ya Rais Samia kinara utoaji wa fedha za ruzuku kwenye kilimo - Waziri Bashe.

  Waziri wa Kilimo nchini Tanzania Mhe. Hussein Bashe ameitaja Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kama serikali kinara kwa ukanda wa kusini mwa Afrika kwa kutoa fedha nyingi za ruzuku kwenye sekta ya kilimo cha mazao mbalimbali ya kibiashara. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Benki ya Taifa ya Ushirika leo Jumatatu Aprili 28, 2025 Jijini Dodoma, Waziri Bashe ametaja kuwa serikali ya Rais Samia kwa mwaka 2024/25 pekee imetoa ruzuku ya takribani Shilingi bilioni 99.5 kwenye zao la Pamba, sambamba na Bilioni nyingine 21 zilizotolewa kwenye zao la tumbaku kwa mwaka 2024/2025 Aidha Serikali ya Rais Samia pia kwa mwaka wa fedha 2024/25 imetoa jumla ya Shilingi Bilioni 281 kwaajili ya pembejeo na miche ambayo wakulima wamekuwa wakipewa bure suala ambalo limewezesha sekta ya Korosho kuwa na uzalishaji mkubwa zaidi wa tani 520,000 ambazo hazikuwahi kufikiwa tangu kupatikana kwa uhuru suala ambalo limewezesha wakulima kuuza mazao ya shilingi 1.8 kwa mwaka 2024...