Skip to main content

Posts

Showing posts from January 17, 2026

@marato_tv

@marato_tv
#sauti_ya_jamii

Waziri na Ulinzi na Jkt Akutana na Kufanya Mazungumzo na Watumishi wa Wizara ya Ulinzi na Jkt

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Dkt. Rhimo Nyansaho (Mb), tarehe 16 Januari 2026,jijini Dodoma, amekutana na kufanya mazungumzo Watumishi wa Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.  Mkutano huo wa Dkt Rhimo Nyansaho na Wafanyakazi ulikuwa na lengo la kufahamiana na kusikiliza masuala mbalimbali yahusuyo utendaji kazi wa Wafanyakazi wa Wizara ya Ulinzi na JKT, ulihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi na JKT, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Wakuu wa Idara na Vitengo, Maafisa Jenerali, Maafisa wakuu, Maafisa wadogo, Askari na Watumishi wa Umma. Katika hotuba yake kwenye kikao hicho, Waziri wa Ulinzi na JKT, alitumia fursa hiyo kuwaeleza watumishi wa Wizara ya Ulinzi na JKT Malengo na Matarajio ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa  Wizara ya Ulinzi na JKT, na akamshukuru Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kumteua ili aweze kumsaidia kuhakikisha Tanzania inakuwa salama na kuendelea ku...

Dk.Migiro Akagua Ujenzi Jengo la Ofisi za Ccm Makao Makuu Jijini Dodoma

KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt.Asha-Rose Migiro akiwa ameambatana na Naibu Katibu Mkuu Bara Ndugu John Mongella,leo Januari 17,2026 amekagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Ofisi ya Makao Makuu ya Chama hicho katika eneo la NCC jijini Dodoma.

Waziri Mkuu Aongoza Kikao Cha Ujenzi wa Mradi ya Barabara za Haraka

  Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Januari 17, 2026 ameongoza kikao cha kazi kuhusu ujenzi wa miradi ya barabara za haraka (Express Ways) kwa ubia kupitia mfumo wa PPP. Kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu, kimehudhuriwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge,  Uratibu na Wenye Ulemavu, William Lukuvi, Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, Naibu Waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile. Wengine ni Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, Dkt. James Kilabuko, Katibu Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara pamoja na watendaji wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Binafsi (PPPC), wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji, David Kafulila.

Tanzania Yashiriki Maonesho ya Utalii Nchini Finland

Ubalozi wa Tanzania nchini Sweden umeratibu na kushiriki katika Maonesho ya Kimataifa ya Utalii ya Matka yanayofanyika jijini Helsinki, Finland, kuanzia tarehe 14-18 Januari, 2026, huku ukitangaza vivutio vya utalii vya Tanzania pamoja na filamu ya Tanzania: The Royal Tour.  Maonesho hayo ni miongoni mwa maonesho makubwa barani Ulaya yakijumuisha kampuni 950 za utalii, usafiri wa ndege, vyombo vya habari, na ushauri elekezi wa utalii kutoka duniani kote ambapo katika siku ya kwanza yalipokea washiriki 56,000 wakiwemo watalii watarajiwa. Kampuni binafsi za Lifestyle Safaris & Holidays na Lifetime Safaris za Tanzania nazo zinashiriki katika maonesho hayo zikiwa na timu ya Ubalozi wa Tanzania. Nchi zingine za Afrika zinazoshiriki ni Uganda, Kenya, Ushelisheli, Namibia, Afrika Kusini, Senegal, Moroko, Tunisia na Misri. Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Mobhare Matinyi, anayeiwakilishia pia Tanzania katika nchi za Nodiki, Baltiki na Ukraina, alitumia jukwaa kuelezea namna Tanza...

Waziri Mkuu Aongoza Kikao Kuhusu Masuala ya Wafanyakazi

 Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akiongoza kikao kazi kuhusu masuala ya wafanyakazi, ofisini kwa Waziri Mkuu Mlimwa jijini Dodoma, Januari 17, 2026.  Kikao hicho kilimshirikisha Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu, William Lukuvi , Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu , Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Regina Quarry na baadhi ya Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu pamoja, Watendaji wa Wizara hizo na baadhi ya Wakuu wa Mikoa.