Mwandishi wetu ;TANGA Shirika la Environmental Management and Economic Development Organization (EMEDO)limefafanua utekelezaji wa miradi mbalimbali yenye tija katika jamii kwenye kikao cha pamoja Kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja Mashirika yasiyo ya Kiserikali kinachofanyika Jijini Tanga. Afisa Mawasiliano wa EMEDO Peter Kimisha akishiriki hatua ya awali ya kueleza mategemeo ya Shirika kwenye mkutano huo aliweka bayana kuwa EMEDO inakiona kikao hicho kuwa ni fursa ya kueleza mbele ya wadau wengine utekelezaji wa kazi zake Kwa Mwaka 2025 - 2026 pamoja na kutengeneza mahusiano mkakati na wadau wengine. Peter Pia alieleza umuhimu wa kikao hicho ni kuuelewa vyema muongozo wa mashirikiano baina ya Sekta ya Uvuvi na Asasi za Kiraia zinazofanya kazi kwenye eneo la uvuvi. Naye Bwana Edwin Soko, Mjumbe wa Bodi wa EMEDO alitoa wasilisho zuri lililoeleza shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na Shirika la EMEDO kwenye eneo la uchumi na mazingira ndani ya se...
Marato tv - Sauti ya Jamii